Demokrasia: Tanzania ya 12 Afrika??

Big Dady

Member
Joined
Nov 10, 2009
Posts
59
Reaction score
2
Licha ya kuongoza Afrika Mashariki, Tanzania inashika nafasi ya 12 katika ya nchi 50 za barani Afrika na nafasi 97 duniani kati ya mataifa 167. (Nukuu gazeti la mwananchi leo).

Pamoja na mbembwe zote za watawala wetu kwamba nchi hii ina demokrasia, kumbe inashika nafasi ya 12 katika Afrika na ya 97 duniani. Nafasi ya 97 ni zaidi ya nusu ya nchi za dunia hii. Ina maana kidunia hata asilimia 50 ya kuwa na demokrasia Tanzania haijafika. Sasa mbwembwe zote zi wapi?

Bahati mbaya sana watawala wetu wanapenda tafiti za akina Mkangara ambao husifia tu watawala ili kuwajengea uhalali wa kutawala millele. Najua utafiti huu hawataupenda maana unaeleza ukweli ambao wao hawaupendi. Wanapenda kusikia tu eti JK anashinda kwa kishindo, kimbunga nk.

Poleni sana, kumbe demokrasia hapa nchini ni feki sana.
 
Hata hiyo bado haistaili, angali katika chaguzi ndogo mambo yanayofanyika kukandamiza demokrasia nenda na katika uchaguzi mkuu wenyewe, ingiza na sheria mpya ya fedha za uchaguzi utaniambia sasa tena kwa hakika kuwa lazima itashika nafasi ya 35.
 
Hiyo taasisi imefanya research, so at least they know what is happening in other countries,,, sasa wewe mwenzangu na mimi unayejua yanayotokea Tanzania tu na huenda Dar es Salaam tu... Una haki gani ya ku-dispute... hiyo research.

Kasheshe
 
Lakini tupo vizuri compared to other countries in Africa. Ina maana nchi 38 za Africa ziko chini yetu na inamaana kuwa Afrika inachangia 90% ya wale waliochini ya 100. Terrible!!!!! Kama TZ tuijuavyo ni ya 12 Africa, sasa fikiria hizo nchi nyingine tuliowazidi zitakuwaje? bado njia ni ndefu sana!
 
Tatizo za hizo tafiti huwa zinaangalia sana sheria....so in papers we are very democratic but on ground and real life nothing is implemented.....tuna utawala wa sheria lakini hatutumii sheria zetu vizuri.....
 


Mkuu aliyekuambia Tanzania kuna demokrasia ni nani?? Huyo kakudanganya, tena sana kama vile mtoto!!! Tena mbona nafasi ya 97 duniani ni nzuri? inastahili iwe ya mwisho kabisa?

Demokrasia ni pomoja na haki pia? Je kule migodini North Mara- Barrick Gold, kule Mbagala, kule Kipawa, kule kwingineko ambako watanzania hawana haki ya maamuzi je? Yaani kule ambako.... nikitaja hapa list ni ndefu!!!

Hapa ni udikteta tu!!! Tusubiri demokrasia ifufuke toka kuzimu, pengine kipindi hiki cha pasaka itafufuka na bwana.
 
This is good news kwetu na inaonyesha kwamba hali li shwari kwa wenzetu... ila pia tutumie fursa hii kutenganisha demokrasia na utawala bora... ni vitu viwili tofauti
 
Leon Bahati


TANZANIA inaongoza kwa kuwa utawala wa kidemokrasia katika ukanda wa Afrika Mashariki, kwa mujibu wa ripoti ya matokeo ya utafiti.

Licha ya kuongoza Afrika Mashariki, Tanzania inashika nafasi ya 12 katika ya nchi 50 za barani Afrika na nafasi 97 duniani kati ya mataifa 167.

Utafiti huo umetolewa hivi karibuni na Wataalamu wa Taasisi ya Kimataifa wa Utafiti na Ushauri wa Kiintelijensia (EIU) uliochunguza mienendo ya tawala zote zilizochaguliwa kidemokrasia duniani hadi kufikia mwaka 2008.

Nchi nyingine zinazoifuatia Tanzania katika ukanda wa Afrka Mashariki pamoja na nafasi inazoshikilia Afrika na dunia ni Uganda (Afrika 16, dunia 101), Kenya (Afrika 17, dunia 103), Burundi (Afrika 19, dunia 106) na ya mwisho ni Rwanda (Afrika 26, dunia 121).

EIU, ambayo makao yake makuu yapo jijini London, Uingereza inaeleza katika utafiti huo kwamba nchi 10 kumi bora kwa demokrasia barani Afrika ni Mauritus, ambayo inaongoza na kufuatiwa na Afrika Kusini, Botswana, Guinea, Namibia, Lesotho, Benin, Mali, Madagascar, Msumbiji wakati Ghana ni ya 11.

Tawala zilizoonyesha demokrasia hafifu zaidi barani Afrika ni Chad, ikifuatiwa na Jamhuri ya Afrika Kati, Guinea-Bissau, Libya, Guinea, Guinea ya Ikweta, Jamhuri ya Demokrasia ya Congo (DRC), Eritrea, Djibuti na Togo.

Ripoti hiyo inaonyesha nchi inayoongoza duniani kwa kuwa na demokrasia ni Sweeden ambayo inafuatiwa na Norway, Iceland, Uholanzi, Denmark, Finland, New Zealand, Uswisi, Luxembourg, Australia na Canada.

Licha ya mataifa makubwa kama Marekani, Uingereza, Ujerumani na Ufaranza kuonekana kuwa vimbelembele wa kuhimiza demokrasia duniani, hayamo kwenye kumi bora ya orodha hiyo.
Ujerumani inashika nafasi ya 1), Marekani (18), Uingereza (21) na Ufaransa (24).

Tawala zinazoshika mkia duniani kwa demokrasia hafifu ni Korea ya Kaskazini, Chad, Turkmenistan, Uzbekistan, Myanmar, Jamhuri ya Afrika Kati, Saudi Arabia, Guinea Bissau, Libya, Laos, Syria, Guinea ya Ikweta na DRC.

Kwenye ripoti hiyo, EIU imegawanya demokrasia katika makundi makuu manne; demokrasia iliyokomaa; demokrasia inayokua; demokrasia ya mchanganyiko inayotokana na matakwa ya watu lakini inayoaandamana na vitendo vya kutumia dola katika kujiimarisha; na kundi la mwisho ni la demokrasia inayotokana na utawala wa mabavu.

Ukiachia kundi la kwanza la demokrasia iliyokomaa, kundi la pili na la tatu linaelezewa na EIU kuwa tawala zake zinaendeshwa kiubabaishaji kwa maana kwamba hazizingatii misingi ya demokrasia. Ingawa kundi la nne lipo katika tawala za mabavu, kuna aina fulani ya utekelezaji wa demokrasia.

Katika mchanganuo huo, EIU inaeleza kwamba ni asilimia 14 tu ya watu duniani wanaoishi katika demokrasia iliyokomaa wakati asilimia 50 wanaishi katika demokrasia ya kiubabaishaji.

Tanzania kwenye mchanganua huo ipo katika kundi la tatu la demokrasia mchanganyiko ambayo ni ya utawala ambao licha ya kutumia demokrasia ina kiasi fulani cha kutumia dola katika kujiimarisha madarakani.

Nchi nyingine za Afrika Mashariki zilizo kwenye kundi hilo ni Uganda, Kenya na Burundi. Rwanda ipo kwenye kundi la nne, ambalo ni la utawala unaotumia nguvu katika kujiimarisha.
Katika Afrika ni Mauritus pekee iliyopo kwenye kundi la demokrasia iliyokomaa.

Afrika Kusini Botswana, Namibia, Lesotho na Benin zimewekwa katika kundi la demokrasia inayokua.

Mataifa makubwa kama vile Ujerumani, Marekani, Uingereza, Ufaransa, Japan, Italia na Canada hazipo kwenye nchi kumi bora katika kundi la demokrasia iliyokomaa.

Utafiti huo unaweka wazi kwamba karibu nusu ya nchi zote duniani zinaendeshwa kwa demokrasia, lakini tawala nyingi hazizingatii mfumo huo kwa umakini.
Kwenye mchanganua huo, Iran na Sudan zipo katika kundi la tawala za serikali zinazoongozwa kimabavu, Iraq na Palestina ziko katika kundi la tatu la demokrasia ya mchanganyiko wakati Israeli imo kwenye kundi la demokrasia inayokua. Somalia haikuwekwa kwenye kundi lolote kutokana na kutokuwa na serikali inayoeleweka.
 
TZ kwa demokrasia ipi ???? kama demokrasia ya woga hapo nakubaliana na huyo aliyefanya hiyo risechi.....kazi kwelikweli
 
Ati ya 12, hawa wazungu wameshindwa kufanya kazi kwenye nchi zao wanatuvamia sisi Afrika kwa maresearch uchwara. Watuache bwana Kha! Hawawezi kutulia kwao hadi walete vijimaneno vyao.
 
TANZANIA inaongoza kwa kuwa utawala wa kidemokrasia katika ukanda wa Afrika Mashariki, kwa mujibu wa ripoti ya matokeo ya utafiti.

Licha ya kuongoza Afrika Mashariki, Tanzania inashika nafasi ya 12 katika ya nchi 50 za barani Afrika na nafasi 97 duniani kati ya mataifa 167.

Utafiti huo umetolewa hivi karibuni na Wataalamu wa Taasisi ya Kimataifa wa Utafiti na Ushauri wa Kiintelijensia (EIU) uliochunguza mienendo ya tawala zote zilizochaguliwa kidemokrasia duniani hadi kufikia mwaka 2008.

Nchi nyingine zinazoifuatia Tanzania katika ukanda wa Afrka Mashariki pamoja na nafasi inazoshikilia Afrika na dunia ni Uganda (Afrika 16, dunia 101), Kenya (Afrika 17, dunia 103), Burundi (Afrika 19, dunia 106) na ya mwisho ni Rwanda (Afrika 26, dunia 121).

EIU, ambayo makao yake makuu yapo jijini London, Uingereza inaeleza katika utafiti huo kwamba nchi 10 kumi bora kwa demokrasia barani Afrika ni Mauritus, ambayo inaongoza na kufuatiwa na Afrika Kusini, Botswana, Guinea, Namibia, Lesotho, Benin, Mali, Madagascar, Msumbiji wakati Ghana ni ya 11.

Tawala zilizoonyesha demokrasia hafifu zaidi barani Afrika ni Chad, ikifuatiwa na Jamhuri ya Afrika Kati, Guinea-Bissau, Libya, Guinea, Guinea ya Ikweta, Jamhuri ya Demokrasia ya Congo (DRC), Eritrea, Djibuti na Togo.

Ripoti hiyo inaonyesha nchi inayoongoza duniani kwa kuwa na demokrasia ni Sweeden ambayo inafuatiwa na Norway, Iceland, Uholanzi, Denmark, Finland, New Zealand, Uswisi, Luxembourg, Australia na Canada.

Licha ya mataifa makubwa kama Marekani, Uingereza, Ujerumani na Ufaranza kuonekana kuwa vimbelembele wa kuhimiza demokrasia duniani, hayamo kwenye kumi bora ya orodha hiyo.
Ujerumani inashika nafasi ya 1), Marekani (18), Uingereza (21) na Ufaransa (24).

Tawala zinazoshika mkia duniani kwa demokrasia hafifu ni Korea ya Kaskazini, Chad, Turkmenistan, Uzbekistan, Myanmar, Jamhuri ya Afrika Kati, Saudi Arabia, Guinea Bissau, Libya, Laos, Syria, Guinea ya Ikweta na DRC.

Kwenye ripoti hiyo, EIU imegawanya demokrasia katika makundi makuu manne; demokrasia iliyokomaa; demokrasia inayokua; demokrasia ya mchanganyiko inayotokana na matakwa ya watu lakini inayoaandamana na vitendo vya kutumia dola katika kujiimarisha; na kundi la mwisho ni la demokrasia inayotokana na utawala wa mabavu.

Ukiachia kundi la kwanza la demokrasia iliyokomaa, kundi la pili na la tatu linaelezewa na EIU kuwa tawala zake zinaendeshwa kiubabaishaji kwa maana kwamba hazizingatii misingi ya demokrasia. Ingawa kundi la nne lipo katika tawala za mabavu, kuna aina fulani ya utekelezaji wa demokrasia.

Katika mchanganuo huo, EIU inaeleza kwamba ni asilimia 14 tu ya watu duniani wanaoishi katika demokrasia iliyokomaa wakati asilimia 50 wanaishi katika demokrasia ya kiubabaishaji.

Tanzania kwenye mchanganua huo ipo katika kundi la tatu la demokrasia mchanganyiko ambayo ni ya utawala ambao licha ya kutumia demokrasia ina kiasi fulani cha kutumia dola katika kujiimarisha madarakani.

Nchi nyingine za Afrika Mashariki zilizo kwenye kundi hilo ni Uganda, Kenya na Burundi. Rwanda ipo kwenye kundi la nne, ambalo ni la utawala unaotumia nguvu katika kujiimarisha.
Katika Afrika ni Mauritus pekee iliyopo kwenye kundi la demokrasia iliyokomaa.

Afrika Kusini Botswana, Namibia, Lesotho na Benin zimewekwa katika kundi la demokrasia inayokua.

Mataifa makubwa kama vile Ujerumani, Marekani, Uingereza, Ufaransa, Japan, Italia na Canada hazipo kwenye nchi kumi bora katika kundi la demokrasia iliyokomaa.

Utafiti huo unaweka wazi kwamba karibu nusu ya nchi zote duniani zinaendeshwa kwa demokrasia, lakini tawala nyingi hazizingatii mfumo huo kwa umakini.

Kwenye mchanganua huo, Iran na Sudan zipo katika kundi la tawala za serikali zinazoongozwa kimabavu, Iraq na Palestina ziko katika kundi la tatu la demokrasia ya mchanganyiko wakati Israeli imo kwenye kundi la demokrasia inayokua. Somalia haikuwekwa kwenye kundi lolote kutokana na kutokuwa na serikali inayoeleweka.


http://www.mwananchi.co.tz/newsrids.asp?id=18711
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…