Demokrasia ya Korea Kusini inashangaza

Demokrasia ya Korea Kusini inashangaza

Mi mi

JF-Expert Member
Joined
Jul 14, 2024
Posts
2,748
Reaction score
5,112
Hii demokrasia ya Korea kusini inashangaza kweli.

Baada ya Rais aliyetolewa madarakani kwa kura za wabunge za kutokuwa na imani naye bwana Yoon Suk Yeol baada ya kutoa amri ya nchi kuwa chini ya sheria za kijeshi ili kudhibiti wakomunisti wa China na Korea Kaskazini kujipenyeza katika siasa za Korea kusini kwa mujibu wake yeye.

Sasa mahakama huko Korea kusini ilitoa amri huyu bwana kukamatwa na kufunguliwa mashitaka na polisi wa huko SK wakapewa kibali cha kutekeleza amri hiyo ila jambo la kushangaza polisi zaidi ya 100 hapo jana walishindwa kutekeleza amri hiyo ya kumkamata huyu bwana baada kukutana na kizuizi cha wanajeshi walinzi wa huyu Rais katika makazi ya Rais pamoja na baadhi ya wafuasi wa huyu bwana.

Inakuwaje hawa maafisa wanaweka kizuizi kwa amri ya kimahakama kutekelezwa na polisi wa SK na wao kuendelea kumkingia kifua huyu former president hii demokrasia yao SK ni ya namna gani hii ? Inashangaza

N.b
Katika historia ya SK jeshi lina ushawishi mkubwa sana wa kimaamuzi na kubadili kabisa taswira nzima ya nchi kwa kipindi kirefu SK iliwahi kuishi chini ya amri za kijeshi.
 
Hii demokrasia ya Korea kusini inashangaza kweli.

Baada ya Rais aliyetolewa madarakani kwa kura za wabunge za kutokuwa na imani naye bwana Yoon Suk Yeol baada ya kutoa amri ya nchi kuwa chini ya sheria za kijeshi ili kudhibiti wakomunisti wa China na Korea Kaskazini kujipenyeza katika siasa za Korea kusini kwa mujibu wake yeye.

Sasa mahakama huko Korea kusini ilitoa amri huyu bwana kukamatwa na kufunguliwa mashitaka na polisi wa huko SK wakapewa kibali cha kutekeleza amri hiyo ila jambo la kushangaza polisi zaidi ya 100 hapo jana walishindwa kutekeleza amri hiyo ya kumkamata huyu bwana baada kukutana na kizuizi cha wanajeshi walinzi wa huyu Rais katika makazi ya Rais pamoja na baadhi ya wafuasi wa huyu bwana.

Inakuwaje hawa maafisa wanaweka kizuizi kwa amri ya kimahakama kutekelezwa na polisi wa SK na wao kuendelea kumkingia kifua huyu former president hii demokrasia yao SK ni ya namna gani hii ? Inashangaza

N.b
Katika historia ya SK jeshi lina ushawishi mkubwa sana wa kimaamuzi na kubadili kabisa taswira nzima ya nchi kwa kipindi kirefu SK iliwahi kuishi chini ya amri za kijeshi.
Kuna demokrasia kubwa sana SK, ila inaonekana rais anatumia watu wake binafsi kutaka kupindisha demokrasia. Angalau demokrasia hii kuliko ile ya hapa nchini ambayo imekufa mazima.
 
Hii kauli ya kudhibiti wakomunisti wa China na Korea Kaskazini wasiweze kuleta madhara SK, ndio iliyombeba na kumpa uzalendo uliotukuka.
Kumbuka SK kuna kambi za kijeshi za US zenye malengo ya kulinda maslai ya SK & US.​
 
Hii kauli ya kudhibiti wakomunisti wa China na Korea Kaskazini wasiweze kuleta madhara SK, ndio iliyombeba na kumpa uzalendo uliotukuka.
Kumbuka SK kuna kambi za kijeshi za US zenye malengo ya kulinda maslai ya SK & US.​
Kama ni mzalendo kwa nini walipiga kura nyingi za kumuondoa ?

Je, hao wabunge wengine wa SK hawaogopi hilo tishio la wakomunisti wa NK na CHN ?
 
Kuna demokrasia kubwa sana SK, ila inaonekana rais anatumia watu wake binafsi kutaka kupindisha demokrasia. Angalau demokrasia hii kuliko ile ya hapa nchini ambayo imekufa mazima.
Kwa kufuatilia kwangu Rais yule hakukosea, wala sio kwamba alikurupuka ila tu demokrasia ya South Korea ina deko sana.

Korea Kusini ina tabia ya kuamini kila Rais ni mkosefu haijalishi awe nani, ndio maana Marais wastaafu wa ile nchi ama huwa wanajiua au wanafungwa. Ni mmoja tu mstaafu ambaye hana kesi. Meanwhile majirani wa Korea, maadui na marafiki zake kama hao Marekani hakuna Rais anachukuliwa kwa chuki kama South Korea.

Kuna elements za destabilization ndani ya South Korea tena kwa muda mrefu. Ukifuatilia huyo Rais hana kesi ya rushwa, ubadhirifu, hana performance mbaya kiuongozi.
Yani South Korea mpinzani anashinda madaraka anamfunga Rais aliyepita, naye anatoka madarakani anafungwa na serikali inayofuata, nayo Rais wake anashtakiwa na inayofuata anajiua. Kama sio upuuzi ni nini.
 
Back
Top Bottom