Denis phombeah kwa ufupi

Denis phombeah kwa ufupi

Mohamed Said

JF-Expert Member
Joined
Nov 2, 2008
Posts
21,967
Reaction score
32,074
DENIS PHOMBEAH KWA UFUPI

WanaMajlis,
Kuna mwenzetu mmoja kaniletea ujumbe huo hapo chini anataka
nimpe historia ya Denis Phombeah:

smarte_r said:
mzee wangu mohamed said itakuwa vyema kama utamuelezea kiundani huyo mnyasa hapa jf.

binafsi nataka sana kumfahamu vizuri na kufahamu uhusika wake katika harakati za kisiasa ndani ya tanganyika.

niwie radhi kwa ombi langu maana siku hizi nimekuwa sivutiwi kusoma magazeti ya hapa nyumbani hususani gazeti la raia mwema.

Jibu langu hilo hapo chini:

Smarte,
Sina taarifa nyingi kuhusu Denis Phombeah.

1566358042547.png

Denis Phombeah

1566357983865.png

Phombeah kwa mara ya kwanza nimemsoma katika kitabu, ''The Making of Tanganyika,''
Chato and Windus, London 1965.

Kitabu hiki kiliandikwa na Judith Listowel na alipokuja Tanganyika kufanya utafiti wake mwenyeji wake alikuwa Ally Sykes kupitia kwa Peter Colmore, Nairobi.

Kitabu hiki ndicho pekee katika vitabu vilivyoandikwa kuhusu historia ya TANU na harakati za kudai uhuru ambacho kimekaribia sana kusema kweli.

Ndani ya kitabu hiki Listowel anahadithia uchaguzi wa mwaka 1953 Ukumbi wa Arnautoglo kati ya Abdul Sykes na Julius Nyerere kuwania urais wa TAA.

Kuna kisa cha kueleza vipi Nyerere aliingizwa katika uongozi wa TAA kushindana na Abdul Sykes mwenyeji wake.

Kisa hiki nishakieleza hapa Majlis mara kadhaa naanimi unakijua.

Sasa kwa kuwa Denis Phombeah hakuwa anajua mipango iliyopangwa baina ya Abdul, Hamza Mwapachu na Ali Mwinyi Tambwe, yeye akitaka sana Nyerere ashinde uchaguzi ule akawa anawapitia wapiga kura kuwashawishi wamchague Nyerere.

Katika uchaguzi ule Nyerere alimshinda Abdul Sykes kwa shida sana kwa hiyo akawa Rais wa TAA.

Uongozi wa TAA 1953 kuelekea kuundwa kwa TANU 1954 ulikuwa kama hivi:

Viongozi hawa ni: J.K. Nyerere, President; Abdulwahid Sykes, Vice-President:
J.P. Kasella Bantu, General Secretary; Alexander M. Tobias and Waziri Dossa Aziz, Joint Minuting Secretary; John Rupia, Treasurer na Ally K. Sykes - Assistant Treasurer. Committee members Dr. Michael Lugazia, Hamisi Diwani, Tewa Said, Denis Phombeah, Z. James, Dome Okochi, C. Ongalo na Patrick Aoko.

Huyu Phombeah alikuwa mmoja kati ya vijana wa Dar es Salaam wa wakati ule ambao walikuwa katika siasa za TAA ingawa yeye alikuwa anatokea Nyasaland.

Kadi ya TANU ya Denis Phombeah ni no. 5.

Baada ya kifo cha Chihota kutoka Rhodesia ambae alikuwa meneja wa Arnautoglo Hall nafasi ile ikashikwa na Phombeah Mnyasa.

Chihota alifariki Uingereza mwanzoni mwa miaka ya 1950.
Phombeah rafiki yake mkubwa alikuwa Oscar Kambona.

Baada ya Oscar Kambona kwenda uhamishoni Uingereza mwaka wa 1967 Phombeah na yeye akamfuata huko.
 
Ina maana na yeye alileta chokochoko,hivyo ikabidi asepe, maana tumesikia kuwa Kambona alikua mpima upepo huko uingereza, kwa kuwa miaka hiyo Marais wengi walikuwa wanapinduliwa na koloni Mama, so Kambona alikuwa planted kule ili kuusoma mchezo
 
Huwezi kuongea mengi kwa vile siyo mwislam
Njinjo,
Ahmed Rashad Ali alikuwa akinambia kuwa mara nyingi alikuwa
akimuomba Abdul Sykes ambae alikuwa rafiki yake toka 1939 hadi
Abdul alipofariki 1968 aeleze mchango wake katika kuasisi TANU
1954.

Abdul alikuwa akimkatalia akimjibu kuwa kuna baadhi ya watu ndani
ya TANU wangependa wao ndiyo wawe watu waliounda chama hicho
yeye asingependa kuingia katika mjadala wa hilo.

Uhuru mwaka wa 1961 ulikuja na changamoto zake.

Baada ya uhuru kulijitokeza juhudi za kushusha hadhi ya TAA kwa
kukiita, ''chama cha starehe.''

Maana ya maneno haya ni kuwa ikiwa TAA ni chama cha starehe basi
hata viongozi wake hawakuwa watu wa maana wa kuandikwa katika
historia ya uhuru wa Tanganyika.

Mimi historia ya TANU ni historia ya wazee wangu na kwa kweli naijua
kukushinda kwani ni historia ya baba zangu na shangazi zangu.

Kama vile Abdul Sykes alivyokaa kimya wakati mwingine huwa naona
sina haja ya kubishana kwa jambo lililo dhahiri.

Kufanya hivi ni moja ya mafunzo katika Uislam.

Ila nitakuambia kitu kimoja.

Katika wasomi wa hapa nyumbani ambao walitaabishwa sana na historia
ya Abdul Sykes, uhusiano wake na Julius Nyerere na kuundwa kwa TANU
ni marehemu Prof. Haroub Othman wa Chuo Kikuu Cha Dar es Salaam.

Prof. Haroub alizungumza na mimi baada ya kusoma kitabu changu lakini
alikwenda pia kuzungumza na Ahmed Rashad Ali na mwisho na Mwalimu
Nyerere
mwenyewe kuhusu historia ya TANU.

1566360329251.png

Kushoto ni Prof. Haroub Othman, Ahmed Rashad Ali na Shekh Ahmed Islam
Uwanja wa Ndege wa Dar es Salaam, 1997
 
Ukweli uko pale pale Julius Nyerere ndio founder na baba Wa Tanzania,hayo mengine mbwembwe tu
Gitarijosenga,
Laiti ningeliandika kitabu cha historia ya TANU kwa nia ya kushusha mchango
wa Mwalimu Nyerere katika uhuru wa Tanganyika ningepuuzwa na wote.

Kitabu cha Abdul Sykes kinachoeleza historia ya TANU mbayo kabisa haikuwa
inafahamika na wengi kimepata umaarufu kwa kule kuja na elimu mpya kuhusu
historia ya uhuru wa Tanganyika historia ambayo inarudi nyuma hadi 1929 pale
African Association ilipoasisiwa Dar es Salaam na kutoka na chama hiki TANU
ikaja kuundwa mwaka wa 1954.

Wasomaji kupitia kitabu hiki wamejifunza mengi kuhusu wazalendo wengine na
hiki ndicho kilichokuwa kimepungua katika historia ya TANU.
 
Nyerere anaitwa Baba wa Taifa, sio Baba.
Shindana na biblia. Hata ujitetee vipi huwezi shindana na huu mstari. Kasome "context" nakuwekea tena "reference".

Sikushangai kwani wengi mnaisoma biblia lakini kila mmoja wenu anatafsiri apendavyo. Mkiambiwa msimle nguruwe. Nyie mnasema kiingiacho halali. Hahahahaha, ndiyo maana kule Vatikano kuna 70% ya wanaotumia viingiavyo hata kwenye pakutokea. Si mmehalalisha viingiavyo?

Hatuwashangai kwa kuikana biblia kwa hili la "baba". Mna kila aina ya baba licha ya kukatazwa na biblia.

FaizaFoxy said:
Mathayo 23:9
Wala msimwite mtu yeyote 'Baba' hapa duniani ...


kwa kukujuza tu.
 
Shindana na biblia. Hata ujitetee vipi huwezi shindana na huu mstari. Kasome "context" nakuwekea tena "reference".

Sikushangai kwani wengi mnaisoma biblia lakini kula mmoja wenu anatafsiri apendavyo. Mkiambiwa msimle nguruwe. Nyie mnasema kiingiacho halali. Hahahahaha, ndiyo maana kule Vatikano kuna 70% ya wanaotumia viingiavyo hata kwenye pakutokea. Si mmehalalisha viingiavyo?

Hatuwashangai kwa kuikana biblia kwa hili la "baba". Mna kila aina ya baba licha ya kukatazwa na biblia.

FaizaFoxy said:
Mathayo 23:9
Wala msimwite mtu yeyote 'Baba' hapa duniani ...


kwa kukujuza tu.
Mfuasi wa yule babu mbakaji.
 
Acha wenge wew Paulo alikuwa na mtoto anamwita mwanangu Thimotheo ,biblia haisomwi kama gazeti LA kufungia chapati ,boya wew
Sikushangai. Ungekuwa hauna huo "ujinga" usingebaki ulipo.

Unapewa darsa la "baba" unaleta hoja ya "mtoto".

Shindana na biblia. Hata ujitetee vipi huwezi shindana na huu mstari. Kasome "context" nakuwekea tena "reference".

Sikushangai kwani wengi mnaisoma biblia lakini kila mmoja wenu anatafsiri apendavyo. Mkiambiwa msimle nguruwe. Nyie mnasema kiingiacho halali. Hahahahaha, ndiyo maana kule Vatikano kuna 70% ya wanaotumia viingiavyo hata kwenye pakutokea. Si mmehalalisha viingiavyo?

Hatuwashangai kwa kuikana biblia kwa hili la "baba". Mna kila aina ya baba licha ya kukatazwa na biblia.

FaizaFoxy said:
Mathayo 23:9
Wala msimwite mtu yeyote 'Baba' hapa duniani ...
 
Namkumbuka tu Gray Phombeah mtangazaji wa BBC Swahili Service miaka ya 90
 
Kinachokatazwa hapo ni lile tendo la kumfanya mtu kuwa tumaini lako yaani huwezi kufanya kitu bila yeye ukipata shida,tatizo au changamoto unakimbilia kwake yaani hata habari ya wokovu wako unategemea yeye badala ya kumtegemea Baba aliye mbinguni hiki ndicho kinachokatazwa hapo maana watu wameenda mbali sana siku hizi wana Baba Mtakatifu (Papa) wana daddy zao mitume kina nabii Bushiri, Mwamposa nk wakiwaona hao ndiyo wamebeba kila kitu chao hawamtazami Mungu wao ni hao viongozi wa kiroho

Lakini hilo fungu au aya haikatazi habari ya kumuita mzazi wako Baba wala Nyerere kuwa Baba wa taifa maana haina athari yoyote
Shindana na biblia. Hata ujitetee vipi huwezi shindana na huu mstari. Kasome "context" nakuwekea tena "reference".

Sikushangai kwani wengi mnaisoma biblia lakini kula mmoja wenu anatafsiri apendavyo. Mkiambiwa msimle nguruwe. Nyie mnasema kiingiacho halali. Hahahahaha, ndiyo maana kule Vatikano kuna 70% ya wanaotumia viingiavyo hata kwenye pakutokea. Si mmehalalisha viingiavyo?

Hatuwashangai kwa kuikana biblia kwa hili la "baba". Mna kila aina ya baba licha ya kukatazwa na biblia.

FaizaFoxy said:
Mathayo 23:9
Wala msimwite mtu yeyote 'Baba' hapa duniani ...


kwa kukujuza tu.
 
Shindana na biblia. Hata ujitetee vipi huwezi shindana na huu mstari. Kasome "context" nakuwekea tena "reference".

Sikushangai kwani wengi mnaisoma biblia lakini kila mmoja wenu anatafsiri apendavyo. Mkiambiwa msimle nguruwe. Nyie mnasema kiingiacho halali. Hahahahaha, ndiyo maana kule Vatikano kuna 70% ya wanaotumia viingiavyo hata kwenye pakutokea. Si mmehalalisha viingiavyo?

Hatuwashangai kwa kuikana biblia kwa hili la "baba". Mna kila aina ya baba licha ya kukatazwa na biblia.

FaizaFoxy said:
Mathayo 23:9
Wala msimwite mtu yeyote 'Baba' hapa duniani ...


kwa kukujuza tu.

Uzuri Biblia imetukataza mabishano ya kipuuzi na kwa vile huu sio uzi wa dini, nisiharibu mada.

Ukristo ni wa wakristo.
 
Uzuri Biblia imetukataza mabishano ya kipuuzi na kwa vile huu sio uzi wa dini, nisiharibu mada.

Ukristo ni wa wakristo.

Umenena vyema kabisa. Kumbe kufundishana bibilia ni "upuuzi"?

Ikiwa maana ya mkristo ni kumfata Yesu alayhi salaam basi Muislam ni Mkristo bora kabisa kuliko yeyote yule.

Muislam anatawadha kama alivyotawadha Yesu alayhi salaam, anaswali kama alivyoswali Yesu alayhi salaam, anaamini Mungu mmoja kama alivyoamini Yesu alayhi salaam.

Ushahidi wote ndani ya biblia. Ukipenda anzisha mada.
 
Umenena vyema kabisa. Kumbe kufundishana bibilia ni "upuuzi"?

Ikiwa maana ya mkristo ni kumfata Yesu alayhi salaam basi Muislam ni Mkristo bora kabisa kuliko yeyote yule.

Muislam anatawadha kama alivyotawadha Yesu alayhi salaam, anaswali kama alivyoswali Yesu alayhi salaam anaamini Mungu mmoja kama wanavyoamini Waislam.

Ushahidi wote ndani ya biblia. Ukipenda anzisha mada.

Narudia tena ukristo ni wa wakristo.
Na uislam wa waislam.
 
Narudia tena ukristo ni wa wakristo.
Na uislam wa waislam.

Narudia na nnaongezea Uislam maana nawe umeongeza na Uislam...

Ikiwa maana ya mkristo ni kumfata Yesu alayhi salaam basi Muislam ni Mkristo bora kabisa kuliko yeyote yule.

Muislam anatawadha kama alivyotawadha Yesu alayhi salaam, anaswali kama alivyoswali Yesu alayhi salaam anaamini Mungu mmoja kama wanavyoamini Waislam.

Ushahidi wote ndani ya biblia. Ukipenda anzisha mada.

Unafahamu maana ya neno Uislam?

Nini maana ya neno Uislam?

Nini maana ya neno Ukristo?

Hapa patamu sana.
 
Narudia na nnaongezea Uislam maana nawe umeongeza na Uislam...

Ikiwa maana ya mkristo ni kumfata Yesu alayhi salaam basi Muislam ni Mkristo bora kabisa kuliko yeyote yule.

Muislam anatawadha kama alivyotawadha Yesu alayhi salaam, anaswali kama alivyoswali Yesu alayhi salaam anaamini Mungu mmoja kama wanavyoamini Waislam.

Ushahidi wote ndani ya biblia. Ukipenda anzisha mada.

Unafahamu maana ya neno Uislam?

Nini maana ya neno Uislam?

Nini maana ya neno Ukristo?

Hapa patamu sana.
Unapenda mabishano ya dini kuliko kumpenda mmeo
 
Back
Top Bottom