Depression-Recession-Bail out

Jafar

JF-Expert Member
Joined
Nov 3, 2006
Posts
1,136
Reaction score
54
Bandugu kuuliza si ujinga. Nimekuwa nikisikia/kusoma maneno haya (Economic Recession, Depression, Bail out) hasa siku hizi ambapo uchumi wa dunia unayumba. Je nini hasa maana ya maneno haya kwenye uchumi wa nchi? Kama bail-out ni kutoa mapesa kwa makampuni ya uzalishaji ili kujikwamua kama wanavyofanya USA, je Tanzania iko imejiandaaje kwa hili?
 

Economic Recession; Ni pale shughuli za kiuchumi zinapopungua kupita kiasi. Haswa pale ambapo uchumi badala ya kukua, au kudumaa unapungua kabisa. Nadhani, huwa unapimwa kwa kipindi cha miezi sita (miezi mitatu (Quarterly) miwili).

Depression, ni pale Hali hiyo ya recession inapokuwa imekithiri.

Bail-out: kama ulivyosema.

Kwa upande wa Tanzania kwa kweli ni wabahatishaji tu. Hatujui nini kinachoendelea ama cha kufanya.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…