Elections 2015 Deusdedit Kahangwa atangaza nia ya kugombea ubunge jimbo la Karagwe kwa tiketi ya CHADEMA

Elections 2015 Deusdedit Kahangwa atangaza nia ya kugombea ubunge jimbo la Karagwe kwa tiketi ya CHADEMA

Sodium

JF-Expert Member
Joined
Feb 14, 2014
Posts
754
Reaction score
404
KAHANGWA: NAGOMBEA TENA UBUNGE WA KARAGWE 2015

Deusdedit Jovin Kahangwa utagombea tenaubunge Wilayani Karagwe? Naulizwa swali hilikila kukicha kutoka kila kona ya Tanzania. Hivyo, kupitia ukurasa huu, nimeamua kulijibu.

Natangaza rasmi kwamba, ifikapo Oktoba 2015, nitagombea tena ubunge wa Karagwe, kupitia Chadema. Tangazo langu lina msingi wake katika mambo sita: Kanuni, Wasifu, Ajenda, Timu,Utajiri, na Akiba ya Kura (KWATUA).

KANUNI ZA KIKATIBA ZINANIRUHUSU

Sifa za kikatiba kama zinavyotajwa katika ibara ya 67 ya Katiba ya Tanzania (1977) ninazo. Mimi ni raia wa Tanzania kwa kuzaliwa; ninao umri zaidi ya miaka ishirini na moja; najua kusoma na kuandika Kiswahili na Kiingereza; ni mwanachama wa chama cha siasa kiitwacho CHADEMA; na katika kipindi cha miaka mitano kuanzia tarehe ya uchaguzi kurudi nyuma nitakuwa sijawahi kutiwa hatiani katika mahakama yoyote kwa kosa lolote la kukwepakulipa kodi yoyote ya Serikali.

Pia, mimi sina ugonjwa wa akili; katika kipindi cha miaka mitano kabla ya uchaguzi nitakuwa sijapata kuhukumiwa na kupewa adhabu ya kifungo kwa kosa linaloambatana na utovu wa uaminifu; sikusudii kugombea kiti cha ubunge na Rais kwa mpigo; na kuna yamkini kubwa kwamba nitapendekezwa na CHADEMA kupeperusha bendera ya ubunge.

WASIFU WANGU UNAVUTIA

Kifamilia, nilizaliwa Aprili 16, 1972. Baba ni Jovin Kahangwa na mama Matilda Zimbeiya. Makazi ya familia yetu ni Kitongoji Katamobwa, Kijiji Kibona, Kata Kanoni, Wilayani Karagwe. Wazazi wangu ni raia wa Tanzania kwa kuzaliwa.

Katika familia hii, kuna watoto 11, wote tuko hai, na kila mmoja ameanzisha familia yake, isipokuwa watoto watatu wa mwisho.

Kielimu, nimesomea taasisi zifuatazo:

Shule ya Msingi Kibona, Karagwe (1981-87); Seminari ya Katoke, Biharamulo (1988-91); Sekondari ya Tambaza, Dar es Salaam (1992-94); na Chuo Kikuu Dar es Salaam (1995-98).

Tambaza nilisomea Fizikia, Kemia na Hisabati (PCM). Na Chuo Kikuu nilisomea shahada ya Tekinolojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA).

Kiajira, nimefanya kazi zifuatazo:

Ualimu katika Shule ya Mtakatifu Anthony, Dar es Salaam (1999); Usanifu wa Programu za Kompyuta katika kampuni ya CATS (T) Ltd, Dar es Salaam(2000); Ualimu katika Shule ya Shaaban Robert(2001); Uhadhiri katika Chuo cha LearnIT, Dar esSalaam (2002-03); Usanifu wa Programu za Kompyuta katika kampuni ya Simu (TTCL), Dar es Salaam (2003-2008); Uhadhiri katika Chuo cha IIT, Dar es Salaam (2009-10); na Ualimu katika Shule ya Karaseco, Karagwe (2013-14).

Kiuongozi, tangu 2007 nimekuwa Mkurugenzi wa Hexadecalogue Ltd ya Dar es Salaam. Kampuni hii inajishughulisha na ushauri, utafiti, upangaji,uendeshaji, na usimamizi wa miradi ya TEHAMA.

Pia, kwa miaka 10 iliyopita nimekuwa mjumbe wa Bodi ya Taasisi ya Umoja wa Mataifa Tawi la Tanzania (UNA Tanzania) yenye ofisi zake Dar es Salaam.

Kidini, mimi ni Mkatoliki kwa kuzaliwa. Nilibatizwa, kupata kumunio, kipaimara na kurudia maagano ndani ya Parokia ya Rwambaizi, Jimbo la Kayanga.

Nilipokuwa kidato cha tano Tambaza, nilikuwa Katibu wa TYCS katika Jimbo Kuu la Dar es Salaam. Nilipokuwa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam nilikuwa Katibu wa IMCS Kanda y aTanzania. Na tangu wakati huo nimekuwa natekeleza utume wangu kama Mlei kupiti chama cha kitume cha CPT.

Kiuandishi, tangu 2003 nimekuwa mwandishi wa magazeti ya Tumaini Letu, Rai, Mtanzania, Tanzania Daima, na sasa Mawio. Pia nimeandika vitabu viwili, “Ilani ya Uchaguzi inayojali(1995)” na “An Empowerment Election Manifesto (1995)” kupita kampuni ya uchapaji ya Ruvu Publishers,Dar es Salaam.

AJENDA INAYOGUSA MAISHA YA WATU

Kisera, ajenda yangu kuhusu Karagwe Mpya inavyo vipaumbele vitano muhimu. Napigania afya bora, elimu bora, itikadi ya ubinadamu ambayo ni msingi wa utawala bora, oikonomia bora, na uchumi bora. Hii ni ajenda inayoongelea “Afya, Elimu, Itikadi, Oikonomia, na Uchumi.” Vokali tano za “a-e-i-o-u” ni njia rahisi ya kuvikumbuka vipaumbele hivi.

Neno “oikonomia” linahitaji ufafanuzi. Kwa mujibu wa Mkusanyiko wa Mafundisho ya Kanisa Kuhusu Jamii(2006), kifungu cha 248, neno“ oikonomia” linamaanisha “usimamizi wa mambo ya nyumbani.”

Msimamo wangu ni kwamba, hatua za makusudi za kisera lazima zichukuliwe ili kukuza na kuhami haki za familia, taasisi ambayo ni kikonyo cha taifa zima.

TIMU NZURI YA KAMPENI

Ninayo timu ya kampeni ya ushindi. Chadema ya Karagwe tayari imeenea kama taasisi kuanzia wilayani, katani, vijijini mpaka vitongojini. Kuna vijana, wanawake, na wazee walio tayari kukifia chama kila kona.

Kwa sehemu kubwa, Kamati za Utendaji wilayani na katani, haziyumbishwi na upepo wa siasa za tumboni. Red Brigedi nayo sasa ni imara. Karagwe hatusemani kwa mafumbo, hatupakani matope wala kupikiana majungu. Tunao “umoja wa roho” ambayo ni silaha ya ushindi.

UTAJIRI WA KUENDESHEA KAMPENI UPO

Uendeshaji wa kampeni unahitaji rasilimali zikiwemo fedha. Kuhusu jambo hili, tayari wapiga kura wangu 30,000 walionikubali mwaka 2010 wameahidi kunichangia “buku buku” kila mmoja.

Wasomaji wa makala zangu magazetini wameahidi kunichangia. Watu niliosoma nao Kibona, Katoke, Tambaza, na Chuo Kikuu wako nami bega kwa bega. Wana TYCS wote hawawezi kunitelekeza. Hata wafanyakazi wenzangu katika Kampuni ya Simu(TTCL) wananiombea usiku na mchana. Familia yangu nayo iko tayari kunichangia.

Hivyo, endapo nitateuliwa na chama changu kugombea ubunge, uwezo wa kuchangia gharama za kuendesha kampeni kwa wastani wa 33% ninao. Sehemu inayobaki chama kitamalizia.

AKIBA YA KURA ZA MWAKA 2010

Mbali na sababu zilizotangulia, kuna ukweli kwamba mwaka 2010 nilipata zaidi ya 30,000 ya kura zote. Hii ni sababu muhimu katika uamuzi wangu kwani kura hizi bado ziko hai. Kura zote zilihesabiwa kwa zaidi ya siku tatu. Mabomu na risasi za moto vikapigwa.

Hatimaye zikatangazwa 36% kama kura zangu. Mimi na wapiga kura wangu hatukuridhishwa na tangazo hili. Tuliibiwa. Kwa sababu ya uchungu wa kuibiwa ushindi, watoto wengi waliozaliwa siku hiyo waliitwa “Kahangwa.” Leo kuna “Kahangwa Watoto” wengi Karagwe. Hivyo, jina “Kahangwa” tayari limejisimika mioyoni mwa wapiga kura wengi wa Karagwe.

Kutokana na yaliyosemwa hapo juu ni wazi kwamba, kama uchaguzi ni nyumba, basi Kahangwa nimekwisha fika kwenye linta wakati wenzangu ndio wanachimba msingi. Kama uchaguzi ni riadha, basi Kahangwa nimekwishafika kati kati ya uwanja wakati wenzangu ndio wanaanzia golini.

Hivyo, mapambano yaliyopo leo kati yangu na watia nia wengine ni sawa na mapambano kati ya sungura na tembo kama sio mapambano kati ya kichuguu na mlima! Watabaki ni wasindikizaji rafiki tu.

HITIMISHO
Hivyo, ni wazi kwamba, kuhusu Ubunge wa Karagwe, Mwaka 2015 ni Zamu yangu Kahangwa. Naomba uniunge mkono kwa mawazo, kwa maneno, kwa vitendo, na kwa rasilimali kupitia barua pepe deus.jovin@gmail.com na simu namba 0758-341-483.

Chanzo: Ukurasa wake wa Facebook
 
Nakushauru uwasilishe barua rasmi sehemu usika kwenye chama na tuache kampeni mpaka bunge litakapovunjwa.

Chadema Kwanza
 
Andaa kikundi cha watu wa kukufariji baada ya matokeo utalia sana wala hutaamini kitakachotokea.
 
Nakushauru uwasilishe barua rasmi sehemu usika kwenye chama na tuache kampeni mpaka bunge litakapovunjwa.

Chadema Kwanza
Mwambie pia aende kwa mtei apate baraka vinginevyo hawezi kuteuliwa bila mwenye chama kusema kitu.
 
KAHANGWA: NAGOMBEA TENA UBUNGE WA
KARAGWE 2015
Deusdedit Jovin Kahangwa utagombea tena
ubunge Wilayani Karagwe? Naulizwa swali hili
kila kukicha kutoka kila kona ya Tanzania. Hivyo,
kupitia ukurasa huu, nimeamua kulijibu.
Natangaza rasmi kwamba, ifikapo Oktoba 2015,
nitagombea tena ubunge wa Karagwe, kupitia
Chadema. Tangazo langu lina msingi wake katika
mambo sita: Kanuni, Wasifu, Ajenda, Timu,
Utajiri, na Akiba ya Kura (KWATUA).
KANUNI ZA KIKATIBA ZINANIRUHUSU
Sifa za kikatiba kama zinavyotajwa katika ibara
ya 67 ya Katiba ya Tanzania (1977) ninazo.
Mimi ni raia wa Tanzania kwa kuzaliwa; ninao
umri zaidi ya miaka ishirini na moja; najua
kusoma na kuandika Kiswahili na Kiingereza; ni
mwanachama wa chama cha siasa kiitwacho
CHADEMA; na katika kipindi cha miaka mitano
kuanzia tarehe ya uchaguzi kurudi nyuma
nitakuwa sijawahi kutiwa hatiani katika
mahakama yoyote kwa kosa lolote la kukwepa
kulipa kodi yoyote ya Serikali.
Pia, mimi sina ugonjwa wa akili; katika kipindi
cha miaka mitano kabla ya uchaguzi nitakuwa
sijapata kuhukumiwa na kupewa adhabu ya
kifungo kwa kosa linaloambatana na utovu wa
uaminifu; sikusudii kugombea kiti cha ubunge na
Rais kwa mpigo; na kuna yamkini kubwa
kwamba nitapendekezwa na CHADEMA
kupeperusha bendera ya ubunge.
WASIFU WANGU UNAVUTIA
Kifamilia, nilizaliwa Aprili 16, 1972. Baba ni
Jovin Kahangwa na mama Matilda Zimbeiya.
Makazi ya familia yetu ni Kitongoji Katamobwa,
Kijiji Kibona, Kata Kanoni, Wilayani Karagwe.
Wazazi wangu ni raia wa Tanzania kwa kuzaliwa.
Katika familia hii, kuna watoto 11, wote tuko
hai, na kila mmoja ameanzisha familia yake,
isipokuwa watoto watatu wa mwisho.
Kielimu, nimesomea taasisi zifuatazo: Shule ya
Msingi Kibona, Karagwe (1981-87); Seminari ya
Katoke, Biharamulo (1988-91); Sekondari ya
Tambaza, Dar es Salaam (1992-94); na Chuo
Kikuu Dar es Salaam (1995-98). Tambaza
nilisomea Fizikia, Kemia na Hisabati (PCM). Na
Chuo Kikuu nilisomea shahada ya Tekinolojia ya
Habari na Mawasiliano (TEHAMA).
Kiajira, nimefanya kazi zifuatazo: Ualimu katika
Shule ya Mtakatifu Anthony, Dar es Salaam
(1999); Usanifu wa Programu za Kompyuta
katika kampuni ya CATS (T) Ltd, Dar es Salaam
(2000); Ualimu katika Shule ya Shaaban Robert
(2001); Uhadhiri katika Chuo cha LearnIT, Dar es
Salaam (2002-03); Usanifu wa Programu za
Kompyuta katika kampuni ya Simu (TTCL), Dar es
Salaam (2003-2008); Uhadhiri katika Chuo cha
IIT, Dar es Salaam (2009-10); na Ualimu katika
Shule ya Karaseco, Karagwe (2013-14).
Kiuongozi, tangu 2007 nimekuwa Mkurugenzi wa
Hexadecalogue Ltd ya Dar es Salaam. Kampuni
hii inajishughulisha na ushauri, utafiti, upangaji,
uendeshaji, na usimamizi wa miradi ya TEHAMA.
Pia, kwa miaka 10 iliyopita nimekuwa mjumbe
wa Bodi ya Taasisi ya Umoja wa Mataifa Tawi la
Tanzania (UNA Tanzania) yenye ofisi zake Dar es
Salaam.
Kidini, mimi ni Mkatoliki kwa kuzaliwa.
Nilibatizwa, kupata kumunio, kipaimara na
kurudia maagano ndani ya Parokia ya
Rwambaizi, Jimbo la Kayanga.
Nilipokuwa kidato cha tano Tambaza, nilikuwa
Katibu wa TYCS katika Jimbo Kuu la Dar es
Salaam. Nilipokuwa Chuo Kikuu cha Dar es
Salaam nilikuwa Katibu wa IMCS Kanda ya
Tanzania. Na tangu wakati huo nimekuwa
natekeleza utume wangu kama Mlei kupiti
chama cha kitume cha CPT.
Kiuandishi, tangu 2003 nimekuwa mwandishi wa
magazeti ya Tumaini Letu, Rai, Mtanzania,
Tanzania Daima, na sasa Mawio. Pia nimeandika
vitabu viwili, "Ilani ya Uchaguzi inayojali(1995)"
na "An Empowerment Election Manifesto (1995)"
kupita kampuni ya uchapaji ya Ruvu Publishers,
Dar es Salaam.
AJENDA INAYOGUSA MAISHA YA WATU
Kisera, ajenda yangu kuhusu Karagwe Mpya
inavyo vipaumbele vitano muhimu.
Napigania afya bora, elimu bora, itikadi ya
ubinadamu ambayo ni msingi wa utawala bora,
oikonomia bora, na uchumi bora. Hii ni ajenda
inayoongelea "Afya, Elimu, Itikadi, Oikonomia,
na Uchumi." Vokali tano za "a-e-i-o-u" ni njia
rahisi ya kuvikumbuka vipaumbele hivi.
Neno "oikonomia" linahitaji ufafanuzi. Kwa
mujibu wa Mkusanyiko wa Mafundisho ya Kanisa
Kuhusu Jamii(2006), kifungu cha 248, neno
"oikonomia" linamaanisha "usimamizi wa mambo
ya nyumbani."
Msimamo wangu ni kwamba, hatua za makusudi
za kisera lazima zichukuliwe ili kukuza na
kuhami haki za familia, taasisi ambayo ni
kikonyo cha taifa zima.
TIMU NZURI YA KAMPENI
Ninayo timu ya kampeni ya ushindi. Chadema ya
Karagwe tayari imeenea kama taasisi kuanzia
wilayani, katani, vijijini mpaka vitongojini. Kuna
vijana, wanawake, na wazee walio tayari kukifia
chama kila kona.
Kwa sehemu kubwa, Kamati za Utendaji wilayani
na katani, haziyumbishwi na upepo wa siasa za
tumboni. Red Brigedi nayo sasa ni imara.
Karagwe hatusemani kwa mafumbo, hatupakani
matope wala kupikiana majungu. Tunao "umoja
wa roho" ambayo ni silaha ya ushindi.
UTAJIRI WA KUENDESHEA KAMPENI UPO
Uendeshaji wa kampeni unahitaji rasilimali
zikiwemo fedha. Kuhusu jambo hili, tayari
wapiga kura wangu 30,000 walionikubali mwaka
2010 wameahidi kunichangia "buku buku" kila
mmoja. Wasomaji wa makala zangu magazetini
wameahidi kunichangia.
Watu niliosoma nao Kibona, Katoke, Tambaza,
na Chuo Kikuu wako nami bega kwa bega. Wana
TYCS wote hawawezi kunitelekeza. Hata
wafanyakazi wenzangu katika Kampuni ya Simu
(TTCL) wananiombea usiku na mchana. Familia
yangu nayo iko tayari kunichangia. Hivyo,
endapo nitateuliwa na chama changu kugombea
ubunge, uwezo wa kuchangia gharama za
kuendesha kampeni kwa wastani wa 33% ninao.
Sehemu inayobaki chama kitamalizia.
AKIBA YA KURA ZA MWAKA 2010
Mbali na sababu zilizotangulia, kuna ukweli
kwamba mwaka 2010 nilipata zaidi ya 30,000 ya
kura zote. Hii ni sababu muhimu katika uamuzi
wangu kwani kura hizi badi ziko hai. Kura zote
zilihesabiwa kwa zaidi ya siku tatu. Mabomu na
risasi za moto vikapigwa. Hatimaye zikatangazwa
36% kama kura zangu. Mimi na wapiga kura
wangu hatukuridhishwa na tangazo hili.
Tuliibiwa.
Kwa sababu ya uchungu wa kuibiwa ushindi,
watoto wengi waliozaliwa siku hiyo waliitwa
"Kahangwa." Leo kuna "Kahangwa Watoto" wengi
Karagwe. Hivyo, jina "Kahangwa" tayari
limejisimika mioyoni mwa wapiga kura wengi wa
Karagwe.
Kutokana na yaliyosemwa hapo juu ni wazi
kwamba, kama uchaguzi ni nyumba, basi
Kahangwa nimekwisha fika kwenye linta wakati
wenzangu ndio wanachimba msingi. Kama
uchaguzi ni riadha, basi Kahangwa nimekwisha
fika kati kati ya uwanja wakati wenzangu ndio
wanaanzia golini. Hivyo, mapambano yaliyopo
leo kati yangu na watia nia wengine ni sawa na
mapambano kati ya sungura na tembo kama sio
mapambano kati ya kichuguu na mlima!
Watabaki ni wasindikizaji rafiki tu.
HITIMISHO
Hivyo, ni wazi kwamba, kuhusu Ubunge wa
Karagwe, Mwaka 2015 ni Zamu yangu
Kahangwa. Naomba uniunge mkono kwa
mawazo, kwa maneno, kwa vitendo, na kwa
rasilimali kupitia barua pepe deus.jovin@gmai
l.com na simu namba 0758-341-483.
Source😛age yake ya fb.

Mkuu vipi kuhusu nafasi yako ya kupita ktk mchakacho wa chama chako?
 
Andaa kikundi cha watu wa kukufariji baada ya matokeo utalia sana wala hutaamini kitakachotokea.

Mr.Kahangwa mwaka 2010 alishinda ila mchezo wa CCM ukamnyima ushindi so karagwa wanamkubari.
 
Jamaa namkubali saaana yuko smart saana,,,,,namuombea saaana apate ingawa 2010 walimfisadi hao magamba na alikuwa ameshinda sema ndo vile aliyekuwa mkuu wa wilaya kipindi kile aliwalazimisha waasimamizi wamtangaze mgombea wa magamba,,,,na Masawe akafie mbele mkuu wa wilaya wa kipindi kile wa Karagwe.
 
Jamaa namkubali saaana yuko smart saana,,,,,namuombea saaana apate ingawa 2010 walimfisadi hao magamba na alikuwa ameshinda sema ndo vile aliyekuwa mkuu wa wilaya kipindi kile aliwalazimisha waasimamizi wamtangaze mgombea wa magamba,,,,na Masawe akafie mbele mkuu wa wilaya wa kipindi kile wa Karagwe.

Kumbe unamjua sana yuko vizuri.
 
Nakushauru uwasilishe barua rasmi sehemu usika kwenye chama na tuache kampeni mpaka bunge litakapovunjwa.

Chadema Kwanza

Hizi siyo kampeni mkuu kutangaza nia unaweza ukatangaza mda wowote.
 
Nakushauru uwasilishe barua rasmi sehemu usika kwenye chama na tuache kampeni mpaka bunge litakapovunjwa.

Chadema Kwanza

Umejieleza vizuri, mimi nadhani kujipitiahapitisha si kubaya, kila anayeona ana ubavu huo ajipitishe watu waanze kumfahamu. Pale ni ngome ya CCM lazima kujizatiti ili kufanikiwa, safi sana Kahagwa anza kupiga jalamba
 
Kila la Heri Kahangwa,Tumia njia sahihi za Chama kuomba ridhaa ya kusimamishwa kugombea Ubunge Karagwe.Tupo pamoja nihesabu kwenye orodha ya supporter wako na nipo tayari kutoa pesa kidogo kwa ajili ya kampeini yako.Demokrasia ya kweli inataka washiriki kama wewe,Tumia ushawishi wako kuwaomba watu wa Karagwe wakupigie kura.Tuwasiliane wakati ukifika kwa ajili ya michango.
 
KAHANGWA: NAGOMBEA TENA UBUNGE WA
KARAGWE 2015
Deusdedit Jovin Kahangwa utagombea tena
ubunge Wilayani Karagwe? Naulizwa swali hili
kila kukicha kutoka kila kona ya Tanzania. Hivyo,
kupitia ukurasa huu, nimeamua kulijibu.
Natangaza rasmi kwamba, ifikapo Oktoba 2015,
nitagombea tena ubunge wa Karagwe, kupitia
Chadema. Tangazo langu lina msingi wake katika
mambo sita: Kanuni, Wasifu, Ajenda, Timu,
Utajiri, na Akiba ya Kura (KWATUA).
KANUNI ZA KIKATIBA ZINANIRUHUSU
Sifa za kikatiba kama zinavyotajwa katika ibara
ya 67 ya Katiba ya Tanzania (1977) ninazo.
Mimi ni raia wa Tanzania kwa kuzaliwa; ninao
umri zaidi ya miaka ishirini na moja; najua
kusoma na kuandika Kiswahili na Kiingereza; ni
mwanachama wa chama cha siasa kiitwacho
CHADEMA; na katika kipindi cha miaka mitano
kuanzia tarehe ya uchaguzi kurudi nyuma
nitakuwa sijawahi kutiwa hatiani katika
mahakama yoyote kwa kosa lolote la kukwepa
kulipa kodi yoyote ya Serikali.
Pia, mimi sina ugonjwa wa akili; katika kipindi
cha miaka mitano kabla ya uchaguzi nitakuwa
sijapata kuhukumiwa na kupewa adhabu ya
kifungo kwa kosa linaloambatana na utovu wa
uaminifu; sikusudii kugombea kiti cha ubunge na
Rais kwa mpigo; na kuna yamkini kubwa
kwamba nitapendekezwa na CHADEMA
kupeperusha bendera ya ubunge.
WASIFU WANGU UNAVUTIA
Kifamilia, nilizaliwa Aprili 16, 1972. Baba ni
Jovin Kahangwa na mama Matilda Zimbeiya.
Makazi ya familia yetu ni Kitongoji Katamobwa,
Kijiji Kibona, Kata Kanoni, Wilayani Karagwe.
Wazazi wangu ni raia wa Tanzania kwa kuzaliwa.
Katika familia hii, kuna watoto 11, wote tuko
hai, na kila mmoja ameanzisha familia yake,
isipokuwa watoto watatu wa mwisho.
Kielimu, nimesomea taasisi zifuatazo: Shule ya
Msingi Kibona, Karagwe (1981-87); Seminari ya
Katoke, Biharamulo (1988-91); Sekondari ya
Tambaza, Dar es Salaam (1992-94); na Chuo
Kikuu Dar es Salaam (1995-98). Tambaza
nilisomea Fizikia, Kemia na Hisabati (PCM). Na
Chuo Kikuu nilisomea shahada ya Tekinolojia ya
Habari na Mawasiliano (TEHAMA).
Kiajira, nimefanya kazi zifuatazo: Ualimu katika
Shule ya Mtakatifu Anthony, Dar es Salaam
(1999); Usanifu wa Programu za Kompyuta
katika kampuni ya CATS (T) Ltd, Dar es Salaam
(2000); Ualimu katika Shule ya Shaaban Robert
(2001); Uhadhiri katika Chuo cha LearnIT, Dar es
Salaam (2002-03); Usanifu wa Programu za
Kompyuta katika kampuni ya Simu (TTCL), Dar es
Salaam (2003-2008); Uhadhiri katika Chuo cha
IIT, Dar es Salaam (2009-10); na Ualimu katika
Shule ya Karaseco, Karagwe (2013-14).
Kiuongozi, tangu 2007 nimekuwa Mkurugenzi wa
Hexadecalogue Ltd ya Dar es Salaam. Kampuni
hii inajishughulisha na ushauri, utafiti, upangaji,
uendeshaji, na usimamizi wa miradi ya TEHAMA.
Pia, kwa miaka 10 iliyopita nimekuwa mjumbe
wa Bodi ya Taasisi ya Umoja wa Mataifa Tawi la
Tanzania (UNA Tanzania) yenye ofisi zake Dar es
Salaam.
Kidini, mimi ni Mkatoliki kwa kuzaliwa.
Nilibatizwa, kupata kumunio, kipaimara na
kurudia maagano ndani ya Parokia ya
Rwambaizi, Jimbo la Kayanga.
Nilipokuwa kidato cha tano Tambaza, nilikuwa
Katibu wa TYCS katika Jimbo Kuu la Dar es
Salaam. Nilipokuwa Chuo Kikuu cha Dar es
Salaam nilikuwa Katibu wa IMCS Kanda ya
Tanzania. Na tangu wakati huo nimekuwa
natekeleza utume wangu kama Mlei kupiti
chama cha kitume cha CPT.
Kiuandishi, tangu 2003 nimekuwa mwandishi wa
magazeti ya Tumaini Letu, Rai, Mtanzania,
Tanzania Daima, na sasa Mawio. Pia nimeandika
vitabu viwili, “Ilani ya Uchaguzi inayojali(1995)”
na “An Empowerment Election Manifesto (1995)”
kupita kampuni ya uchapaji ya Ruvu Publishers,
Dar es Salaam.
AJENDA INAYOGUSA MAISHA YA WATU
Kisera, ajenda yangu kuhusu Karagwe Mpya
inavyo vipaumbele vitano muhimu.
Napigania afya bora, elimu bora, itikadi ya
ubinadamu ambayo ni msingi wa utawala bora,
oikonomia bora, na uchumi bora. Hii ni ajenda
inayoongelea “Afya, Elimu, Itikadi, Oikonomia,
na Uchumi.” Vokali tano za “a-e-i-o-u” ni njia
rahisi ya kuvikumbuka vipaumbele hivi.
Neno “oikonomia” linahitaji ufafanuzi. Kwa
mujibu wa Mkusanyiko wa Mafundisho ya Kanisa
Kuhusu Jamii(2006), kifungu cha 248, neno
“oikonomia” linamaanisha “usimamizi wa mambo
ya nyumbani.”
Msimamo wangu ni kwamba, hatua za makusudi
za kisera lazima zichukuliwe ili kukuza na
kuhami haki za familia, taasisi ambayo ni
kikonyo cha taifa zima.
TIMU NZURI YA KAMPENI
Ninayo timu ya kampeni ya ushindi. Chadema ya
Karagwe tayari imeenea kama taasisi kuanzia
wilayani, katani, vijijini mpaka vitongojini. Kuna
vijana, wanawake, na wazee walio tayari kukifia
chama kila kona.
Kwa sehemu kubwa, Kamati za Utendaji wilayani
na katani, haziyumbishwi na upepo wa siasa za
tumboni. Red Brigedi nayo sasa ni imara.
Karagwe hatusemani kwa mafumbo, hatupakani
matope wala kupikiana majungu. Tunao “umoja
wa roho” ambayo ni silaha ya ushindi.
UTAJIRI WA KUENDESHEA KAMPENI UPO
Uendeshaji wa kampeni unahitaji rasilimali
zikiwemo fedha. Kuhusu jambo hili, tayari
wapiga kura wangu 30,000 walionikubali mwaka
2010 wameahidi kunichangia “buku buku” kila
mmoja. Wasomaji wa makala zangu magazetini
wameahidi kunichangia.
Watu niliosoma nao Kibona, Katoke, Tambaza,
na Chuo Kikuu wako nami bega kwa bega. Wana
TYCS wote hawawezi kunitelekeza. Hata
wafanyakazi wenzangu katika Kampuni ya Simu
(TTCL) wananiombea usiku na mchana. Familia
yangu nayo iko tayari kunichangia. Hivyo,
endapo nitateuliwa na chama changu kugombea
ubunge, uwezo wa kuchangia gharama za
kuendesha kampeni kwa wastani wa 33% ninao.
Sehemu inayobaki chama kitamalizia.
AKIBA YA KURA ZA MWAKA 2010
Mbali na sababu zilizotangulia, kuna ukweli
kwamba mwaka 2010 nilipata zaidi ya 30,000 ya
kura zote. Hii ni sababu muhimu katika uamuzi
wangu kwani kura hizi badi ziko hai. Kura zote
zilihesabiwa kwa zaidi ya siku tatu. Mabomu na
risasi za moto vikapigwa. Hatimaye zikatangazwa
36% kama kura zangu. Mimi na wapiga kura
wangu hatukuridhishwa na tangazo hili.
Tuliibiwa.
Kwa sababu ya uchungu wa kuibiwa ushindi,
watoto wengi waliozaliwa siku hiyo waliitwa
“Kahangwa.” Leo kuna “Kahangwa Watoto” wengi
Karagwe. Hivyo, jina “Kahangwa” tayari
limejisimika mioyoni mwa wapiga kura wengi wa
Karagwe.
Kutokana na yaliyosemwa hapo juu ni wazi
kwamba, kama uchaguzi ni nyumba, basi
Kahangwa nimekwisha fika kwenye linta wakati
wenzangu ndio wanachimba msingi. Kama
uchaguzi ni riadha, basi Kahangwa nimekwisha
fika kati kati ya uwanja wakati wenzangu ndio
wanaanzia golini. Hivyo, mapambano yaliyopo
leo kati yangu na watia nia wengine ni sawa na
mapambano kati ya sungura na tembo kama sio
mapambano kati ya kichuguu na mlima!
Watabaki ni wasindikizaji rafiki tu.
HITIMISHO
Hivyo, ni wazi kwamba, kuhusu Ubunge wa
Karagwe, Mwaka 2015 ni Zamu yangu
Kahangwa. Naomba uniunge mkono kwa
mawazo, kwa maneno, kwa vitendo, na kwa
rasilimali kupitia barua pepe deus.jovin@gmai
l.com na simu namba 0758-341-483.
Source😛age yake ya fb.

nimependa hii profile yajo. tutakutia nguvu kwa hali na mali
 
nimeishi karagwe na family baadhi ziko huko. nitakusapoti. nafikiri matokeo ys serikali za mitaa ni picha nzuri.zoez liwe kuamasisha uandikishaji wapga kura
 
Kamanda penye nia pana njia. Wasifu wako uko safi kabisa. Huku mtandaoni tuko wachache sana. Shuka jimboni mwaga sera nyumba hadi nyumba hicho kiti ni halali yako. Kitendo alichofanya Massawe 2010 ni cha kulaaniwa kabisa kwani hata mimi kilinigusa ingawa sitoki huko kwenu.
 
Big-up kamanda. mungu akupe nguvu, pamoja sana. Hakuna kulala mpaka kieleweke.
 
yale yale....tukisema tamaa ya ukubwa mtatutusi...kahangwa unatangaza nia na kujiamini kupita kiasi itakuwaje chama chako kikikupiga chini?
KAHANGWA: NAGOMBEA TENA UBUNGE WA
KARAGWE 2015
Deusdedit Jovin Kahangwa utagombea tena
ubunge Wilayani Karagwe? Naulizwa swali hili
kila kukicha kutoka kila kona ya Tanzania. Hivyo,
kupitia ukurasa huu, nimeamua kulijibu.
Natangaza rasmi kwamba, ifikapo Oktoba 2015,
nitagombea tena ubunge wa Karagwe, kupitia
Chadema. Tangazo langu lina msingi wake katika
mambo sita: Kanuni, Wasifu, Ajenda, Timu,
Utajiri, na Akiba ya Kura (KWATUA).
KANUNI ZA KIKATIBA ZINANIRUHUSU
Sifa za kikatiba kama zinavyotajwa katika ibara
ya 67 ya Katiba ya Tanzania (1977) ninazo.
Mimi ni raia wa Tanzania kwa kuzaliwa; ninao
umri zaidi ya miaka ishirini na moja; najua
kusoma na kuandika Kiswahili na Kiingereza; ni
mwanachama wa chama cha siasa kiitwacho
CHADEMA; na katika kipindi cha miaka mitano
kuanzia tarehe ya uchaguzi kurudi nyuma
nitakuwa sijawahi kutiwa hatiani katika
mahakama yoyote kwa kosa lolote la kukwepa
kulipa kodi yoyote ya Serikali.
Pia, mimi sina ugonjwa wa akili; katika kipindi
cha miaka mitano kabla ya uchaguzi nitakuwa
sijapata kuhukumiwa na kupewa adhabu ya
kifungo kwa kosa linaloambatana na utovu wa
uaminifu; sikusudii kugombea kiti cha ubunge na
Rais kwa mpigo; na kuna yamkini kubwa
kwamba nitapendekezwa na CHADEMA
kupeperusha bendera ya ubunge.
WASIFU WANGU UNAVUTIA
Kifamilia, nilizaliwa Aprili 16, 1972. Baba ni
Jovin Kahangwa na mama Matilda Zimbeiya.
Makazi ya familia yetu ni Kitongoji Katamobwa,
Kijiji Kibona, Kata Kanoni, Wilayani Karagwe.
Wazazi wangu ni raia wa Tanzania kwa kuzaliwa.
Katika familia hii, kuna watoto 11, wote tuko
hai, na kila mmoja ameanzisha familia yake,
isipokuwa watoto watatu wa mwisho.
Kielimu, nimesomea taasisi zifuatazo: Shule ya
Msingi Kibona, Karagwe (1981-87); Seminari ya
Katoke, Biharamulo (1988-91); Sekondari ya
Tambaza, Dar es Salaam (1992-94); na Chuo
Kikuu Dar es Salaam (1995-98). Tambaza
nilisomea Fizikia, Kemia na Hisabati (PCM). Na
Chuo Kikuu nilisomea shahada ya Tekinolojia ya
Habari na Mawasiliano (TEHAMA).
Kiajira, nimefanya kazi zifuatazo: Ualimu katika
Shule ya Mtakatifu Anthony, Dar es Salaam
(1999); Usanifu wa Programu za Kompyuta
katika kampuni ya CATS (T) Ltd, Dar es Salaam
(2000); Ualimu katika Shule ya Shaaban Robert
(2001); Uhadhiri katika Chuo cha LearnIT, Dar es
Salaam (2002-03); Usanifu wa Programu za
Kompyuta katika kampuni ya Simu (TTCL), Dar es
Salaam (2003-2008); Uhadhiri katika Chuo cha
IIT, Dar es Salaam (2009-10); na Ualimu katika
Shule ya Karaseco, Karagwe (2013-14).
Kiuongozi, tangu 2007 nimekuwa Mkurugenzi wa
Hexadecalogue Ltd ya Dar es Salaam. Kampuni
hii inajishughulisha na ushauri, utafiti, upangaji,
uendeshaji, na usimamizi wa miradi ya TEHAMA.
Pia, kwa miaka 10 iliyopita nimekuwa mjumbe
wa Bodi ya Taasisi ya Umoja wa Mataifa Tawi la
Tanzania (UNA Tanzania) yenye ofisi zake Dar es
Salaam.
Kidini, mimi ni Mkatoliki kwa kuzaliwa.
Nilibatizwa, kupata kumunio, kipaimara na
kurudia maagano ndani ya Parokia ya
Rwambaizi, Jimbo la Kayanga.
Nilipokuwa kidato cha tano Tambaza, nilikuwa
Katibu wa TYCS katika Jimbo Kuu la Dar es
Salaam. Nilipokuwa Chuo Kikuu cha Dar es
Salaam nilikuwa Katibu wa IMCS Kanda ya
Tanzania. Na tangu wakati huo nimekuwa
natekeleza utume wangu kama Mlei kupiti
chama cha kitume cha CPT.
Kiuandishi, tangu 2003 nimekuwa mwandishi wa
magazeti ya Tumaini Letu, Rai, Mtanzania,
Tanzania Daima, na sasa Mawio. Pia nimeandika
vitabu viwili, "Ilani ya Uchaguzi inayojali(1995)"
na "An Empowerment Election Manifesto (1995)"
kupita kampuni ya uchapaji ya Ruvu Publishers,
Dar es Salaam.
AJENDA INAYOGUSA MAISHA YA WATU
Kisera, ajenda yangu kuhusu Karagwe Mpya
inavyo vipaumbele vitano muhimu.
Napigania afya bora, elimu bora, itikadi ya
ubinadamu ambayo ni msingi wa utawala bora,
oikonomia bora, na uchumi bora. Hii ni ajenda
inayoongelea "Afya, Elimu, Itikadi, Oikonomia,
na Uchumi." Vokali tano za "a-e-i-o-u" ni njia
rahisi ya kuvikumbuka vipaumbele hivi.
Neno "oikonomia" linahitaji ufafanuzi. Kwa
mujibu wa Mkusanyiko wa Mafundisho ya Kanisa
Kuhusu Jamii(2006), kifungu cha 248, neno
"oikonomia" linamaanisha "usimamizi wa mambo
ya nyumbani."
Msimamo wangu ni kwamba, hatua za makusudi
za kisera lazima zichukuliwe ili kukuza na
kuhami haki za familia, taasisi ambayo ni
kikonyo cha taifa zima.
TIMU NZURI YA KAMPENI
Ninayo timu ya kampeni ya ushindi. Chadema ya
Karagwe tayari imeenea kama taasisi kuanzia
wilayani, katani, vijijini mpaka vitongojini. Kuna
vijana, wanawake, na wazee walio tayari kukifia
chama kila kona.
Kwa sehemu kubwa, Kamati za Utendaji wilayani
na katani, haziyumbishwi na upepo wa siasa za
tumboni. Red Brigedi nayo sasa ni imara.
Karagwe hatusemani kwa mafumbo, hatupakani
matope wala kupikiana majungu. Tunao "umoja
wa roho" ambayo ni silaha ya ushindi.
UTAJIRI WA KUENDESHEA KAMPENI UPO
Uendeshaji wa kampeni unahitaji rasilimali
zikiwemo fedha. Kuhusu jambo hili, tayari
wapiga kura wangu 30,000 walionikubali mwaka
2010 wameahidi kunichangia "buku buku" kila
mmoja. Wasomaji wa makala zangu magazetini
wameahidi kunichangia.
Watu niliosoma nao Kibona, Katoke, Tambaza,
na Chuo Kikuu wako nami bega kwa bega. Wana
TYCS wote hawawezi kunitelekeza. Hata
wafanyakazi wenzangu katika Kampuni ya Simu
(TTCL) wananiombea usiku na mchana. Familia
yangu nayo iko tayari kunichangia. Hivyo,
endapo nitateuliwa na chama changu kugombea
ubunge, uwezo wa kuchangia gharama za
kuendesha kampeni kwa wastani wa 33% ninao.
Sehemu inayobaki chama kitamalizia.
AKIBA YA KURA ZA MWAKA 2010
Mbali na sababu zilizotangulia, kuna ukweli
kwamba mwaka 2010 nilipata zaidi ya 30,000 ya
kura zote. Hii ni sababu muhimu katika uamuzi
wangu kwani kura hizi badi ziko hai. Kura zote
zilihesabiwa kwa zaidi ya siku tatu. Mabomu na
risasi za moto vikapigwa. Hatimaye zikatangazwa
36% kama kura zangu. Mimi na wapiga kura
wangu hatukuridhishwa na tangazo hili.
Tuliibiwa.
Kwa sababu ya uchungu wa kuibiwa ushindi,
watoto wengi waliozaliwa siku hiyo waliitwa
"Kahangwa." Leo kuna "Kahangwa Watoto" wengi
Karagwe. Hivyo, jina "Kahangwa" tayari
limejisimika mioyoni mwa wapiga kura wengi wa
Karagwe.
Kutokana na yaliyosemwa hapo juu ni wazi
kwamba, kama uchaguzi ni nyumba, basi
Kahangwa nimekwisha fika kwenye linta wakati
wenzangu ndio wanachimba msingi. Kama
uchaguzi ni riadha, basi Kahangwa nimekwisha
fika kati kati ya uwanja wakati wenzangu ndio
wanaanzia golini. Hivyo, mapambano yaliyopo
leo kati yangu na watia nia wengine ni sawa na
mapambano kati ya sungura na tembo kama sio
mapambano kati ya kichuguu na mlima!
Watabaki ni wasindikizaji rafiki tu.
HITIMISHO
Hivyo, ni wazi kwamba, kuhusu Ubunge wa
Karagwe, Mwaka 2015 ni Zamu yangu
Kahangwa. Naomba uniunge mkono kwa
mawazo, kwa maneno, kwa vitendo, na kwa
rasilimali kupitia barua pepe deus.jovin@gmai
l.com na simu namba 0758-341-483.
Source😛age yake ya fb.
 
Back
Top Bottom