Dharau ya Waarabu kwa Waafrika Zanzibar, kumbe Mwalimu Nyerere 1957 aliwaonya kwanza kabla ya kuanzisha ASP

Wanzanzibari Waafrika (wazanzibari weusi) wote ni ndugu zangu wa damu

Kamwe sitakubali kutengwa nao (kwa kuvunja muungano)

Kwanini musiwachukue kwenu mkawapa hifadhi kama munawapenda sana?
 
Kuanzisha chama cha siasa ndani ya nchi ya watu hujauona ubaya hapo?
Enzi zile za ukoloni mkuu mbona hiyo ilikuwa ni vizuri sana, sio kusaidia kuanzisha chama tu, ilikuwa pia kusaidia silaha za kivita, mbinu za kupigana, fedha n.k, ilikuwa Pan Africanism hiyo.
 
enzi zile za ukoloni mkuu mbona hiyo ilikuwa ni vizuri sana, sio kusaidia kuanzisha chama tu, ilikuwa pia kusaidia silaha za kivita, mbinu za kupigana, fedha n.k, ilikuwa pan africanism hiyo

Bado haihalalishi kuingia nchini mwawatu na kufanya uchochezi na ufisadi. Kama misaada ya kivita na silaha mpaka leo nchi zote zenye uasi Africa basi waasi wanapata sapoti kutoka nchi za jirani nayo pia tuite Pan Africanism?

Kaisome vizuri Historia ya ASP mkuu utagundua kama chama kilikua kikiendeshwa na Nyerere nyuma ya pazia.
Mapinduzi ya 64 yalifanywa na nyerere nyuma ya pazia.
Nabaadae akitimiza lengo lake la kuitawala Zanzibar.

Migogoro mikubwa ya chama yote Mwalim Nyerere alikua anamkono wake ndani yake.
Mgogoro wa Ameir Tajo 57-59
Mgogoro wa Mohammed Shamte 59-60
Mgogoro wa Othman Sharif 62-63

Shamte na Tajo walifika kuhama na kufukuzwa chama sababu ya kuhoji na kushindwa kukubali involvement ya Nyerere ndani ya Chama.

Nyerere ndie Aliempa Karume Uongozi wa Chama
Na Nyerere ndie aliemueka Karume KIongozi wa Zanzibar baada ya Mapinduzi.

SI Zanzibar tu Nyerere pia alifanya chokochoko sana kwenye nchi nyengine kama Uganda na DRC
 
Hata bila ASP kuanzishwa, utawala wa Sultan ulikuwa unakwenda kuondoshwa. Ngumu sana minority kutawala majority milele. Hata Kagame na ujanjaujanja wake huko Rwanda ipo siku atang'olewa.
 
Si nimesema enzi za ukoloni? Sasa hivi haitakiwi kuingilia siasa za nchi nyingine sababu nchi zipo hurubba hakuna anayepigania uhuru tena.

Nyerere mbona alisaidia sana nchi za kusini mwa Afrika na vyama vyao vya kudai uhuru kama ZANU, ANC, FRELIMO n.k au na huko pia alikosea?

Sent using Jamii Forums mobile app
 

Nyerere pia aliwahifadhi na kuwasaidia akina Kabila na Milton Obote pia walikuwa wadai uhuru?

Jua kutafautisha kati ya kusaidia na kuingilia.
 
Hata bila ASP kuanzishwa, utawala wa Sultan ulikuwa unakwenda kuondoshwa. Ngumu sana minority kutawala majority milele. Hata Kagame na ujanjaujanja wake huko Rwanda ipo siku atang'olewa.

Sasa hapo Sultan kahusika wapi?

Mapambanio ya Zanzibar yalikua ni baina ya ZNP na ASP mkuu. katafute data za uchaguzi za miaka ya 60 mkuu.
 
Sasa hapo Sultan kahusika wapi?

Mapambanio ya Zanzibar yalikua ni baina ya ZNP na ASP mkuu. katafute data za uchaguzi za miaka ya 60 mkuu.
Kati ya hivyo vyama kimoja kilikuwa proxy ya utawala wa Sultan. You should know that.
 
Kwa hiyo ya Zanzibar umekubali alikuwa sahihi sio?

Atakuwa sahihi vipi na ndio huo ufisadi ninaokwambia. Hakuna usahihi kwenye kuingilia mambo ya nchi zawatu. Alikua na ajenda zake na zimeonekanwa mwisho.
 
Hata ASP walikua wakijulikana kama pro Sultan kabla ya mapinduzi. Chama pekee kilochojitangaza wazi kuwa hawasapoti Usultani kilikuwa ni Umma Party.
Hawa Umma Party ndio waliosababisha Muungano nasikia... Maana Babu alikuwa tishio sana kwa Karume na alikuwa akiungwa mkono na China.
Karume akaona njia pekee ya kupona ni kuungana na bara
 
Ukitaka kujua kama sisi watu weusi bado ni watumwa basi soma au sikiliza simulizi za mabaya na mazuri tuliofanyiwa na watu weupe (wazungu na waarabu ). Yaani utaziona hasira za waarabu wa Buza na Wazungu wa Manzese wanavyo watetea watu wao. Anyway story kuwahusu Waarabu kulingana na mleta UZI sina shida nayo but ninalo tatizo kuhusu mapinduzi, Karume anakuzwa sana, hakushiriki
 
Mhuu
Mhuuu mataga...
 
It makes sense kama Nyerere alipindia serekekali halali ya Zanzibar. Sio wakwezi ni watanganyika ndio wamepindua na kuanza kuitawala Zanzibar. Inafanana kidogo na Izrael.😕
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…