Waufukweni
JF-Expert Member
- May 16, 2024
- 2,060
- 5,648
Mwanamuziki na mmiliki wa Lebo ya WCB, Naseeb Abdul ‘Diamond Platnumz’ amefafanua taarifa za msanii wake Mbwana Kilungi maarufu ‘Mbosso’ kuondoka kwenye lebo hiyo, huku akisema yeye ndiye mtoa tamko wa lebo hiyo.
Soma: Baba Levo atangaza Mbosso kuondoka WCB Wasafi na uamuzi wa Diamond
Kupitia ukurasa wake wa Instagram leo Februari 4, 2025 Diamond amesema kuwa tayari wamekamilisha mazungumzo na Mbosso kuhusu namna nzuri ya kusimamia kazi zake hivyo kwa sasa taarifa yoyote inayozungumzia jambo hilo ipuuzwe.
"Tumekuwa na mazungumzo mazuri sana na Mbosso namna ya kuanza rasmi sasa kusimamia kazi zake na tumekamilisha jambo letu vizuri sana. Tafadhali story yoyote inayozungumzwa kuhusu jambo hili la Mbosso naomba zipuuzwe mpaka mimi binafsi na Mbosso tutakapotoa tamko rasmi," ameeleza Diamond.
Utakumbua taarifa hiyo imekuja kufuatia kuwepo kwa maneno yaliyosambaa mtandaoni kuwa Mbosso amejing'oa kwenye lebo ya Wasafi.
Soma: Baba Levo atangaza Mbosso kuondoka WCB Wasafi na uamuzi wa Diamond
Kupitia ukurasa wake wa Instagram leo Februari 4, 2025 Diamond amesema kuwa tayari wamekamilisha mazungumzo na Mbosso kuhusu namna nzuri ya kusimamia kazi zake hivyo kwa sasa taarifa yoyote inayozungumzia jambo hilo ipuuzwe.
"Tumekuwa na mazungumzo mazuri sana na Mbosso namna ya kuanza rasmi sasa kusimamia kazi zake na tumekamilisha jambo letu vizuri sana. Tafadhali story yoyote inayozungumzwa kuhusu jambo hili la Mbosso naomba zipuuzwe mpaka mimi binafsi na Mbosso tutakapotoa tamko rasmi," ameeleza Diamond.
Utakumbua taarifa hiyo imekuja kufuatia kuwepo kwa maneno yaliyosambaa mtandaoni kuwa Mbosso amejing'oa kwenye lebo ya Wasafi.