Diamond apewa ardhi ya kuishi nchini Kenya

View attachment 715027

Historia inaandikwa ni heshima kubwa pia kwa mziki wetu wa Tanzania.

Viva Diamond.

Narudia tena kusema huyu ' Jamaa ' mtamsema, mtamtusi na kumdhihaki kadri muwezavyo ila matunda ya Kazi zake, Kujituma Kwake, Kuwa mbunifu na Kujipanda ndiko kila siku kunamweka na bado kutamweka Kileleni Kimafanikio. Nasib Abdul ( Diamond Platinumz ) anatupa ' Funzo ' zuri na kubwa sana akina Sisi wenye ' akili kulala ' au ' akili mlegezo ' kama si ' akili goigoi ' kupambana na kutokata tamaa katika kuyatafuta mafanikio ya kweli.

Namuombea kwa Mwenyezi Mungu ( Allah ) mafanikio zaidi na hakuna Siku ambayo nimewahi kumuombe Mtu ' baraka ' kwa Mwenyezi Mungu na asinijibie Kwake hivyo naamini Nasib Abdul ( Diamond Platinumz ) atazidi kuwa juu na juu na Sisi wengine tusichoke kumchukia, kumteta, kumdharau na kumzushia kwani yawezekana hii roho mbaya Yetu Kwake basi Maulana ndiyo anaigeuza kuwa Shani na Baraka Kwake.
 
Robo heka nayo ni ardhi ya kukaa star!garden,parking,swimming pool,courts au ndio bora kitu kuliko kukosa kitu
 
Safi kabisa wengine hata Tz hawapewi hiyo robo eka acha Jamaa ale jasho lake hadi A kusini
 
AMEN
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…