Diamond atangaza ujio wa Wasafi FM na Wasafi TV

Hamuoni kwamba hivi vituo vikianzishwa ... vituo vingine vitapunguza support kwa team ya WASAFI ?
Nilivyosoma kichwa cha hbr hili ndo likawa wazo lakwanza kuliwaza!
naona kama haijakaa njema kivile haileti chachu kwa msanii ati unaenda kuhojiwa kwenye tv yako,redio yako! si ajabu lkn aggghrrrr.. msanii kuingia kiushindani na media nyengine ni kama kujipigilia rungu mwenyewe!
 
mkuu diamond yupo vizur na anaweza wapindua hata magwiji Kama alivyo pindua labo zilizokuwa zinatamba apa mjini ila sasa WCB ndo baba lao
 
Mbona wanastudio yao naninafanya poa sana hiyo mambo za kawaida
 
Safi sana.

Piga Kazi mr,umekuwa mfano bora sana kwa vijana watafutaji.

Tupambane vijana,Maisha ni kutisha na sikutishana.
 
Tv na radio sio mkakati mzuri kwa diamond kwa kuwa itakua conflicts of interest na vyombo vingine ambavyo vinataarajiwa kucheza muziki wake
 
Ni wazo zuri sana lakini aliangalie vyema maana anaweza kujikuta anapoteza pesa yake nyingi sana......biashara ya radio na Tv ni wazi ina hitaji uwekezaji mkubwa sana na siyo kama biashara ya kuimba...
Kwenye hili napata shaka kama wanao mshauri wamemshauri vyema maana hiyo ni bishara yenye ushindani sana kuzidi muziki......leo hii atatakiwa kutafuta mbinu za kuwapora wasikilizaji Clouds fm na E-fm.........
MMMh kwa hii biashara ya radio nachelea sana kuunga mkono.
 
Tv na radio sio mkakati mzuri kwa diamond kwa kuwa itakua conflicts of interest na vyombo vingine ambavyo vinataarajiwa kucheza muziki wake

hizi ni zama za youtube na online dowload... diamond kwa alipofikia huwezi mshusha chini sababu umembania kupiga wimbo wake... maana anategemea youtube sana na ina faida kwake.... ndio maana nyimbo ikiwa kali miaka ya sasa inahit tu hata kama redio zikigoma kucheza
 
Hizo stesheni zake kabla hajazifungua nimesha ziBLOCK! kwangu, maana najua hata nikisikiliza/kutazama 24/7 sitapata wasaa wa kumsikiliza ama kumtazama msanii wangu kipenzi K 4 REAL!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…