Diamond: Clouds wameanza kushika adabu sasa.

Diamond: Clouds wameanza kushika adabu sasa.

Bilionea Asigwa

JF-Expert Member
Joined
Sep 21, 2011
Posts
16,515
Reaction score
28,506
Msanii Diamond Platinumz amewapiga dongo Clauds media kwa kile alichokiita " Taratiibu Wameanza kushika adabu yao".


"Mambo Yamekuwa Magumu hadi imebidi waombe poo na kuomba msaada kwa mlezi wetu(Paul Makonda)..
Najiuliza tu....Leo kawa sio Mvamizi tena???"

"Adabu imewakaa sasa, wanaanza kuwaheshimu na kuwakumbatia wasanii...
Hata wale walosema hawauzi sasa wanawaona wanathamani...
Eti hadi kucheza nao kikapu Manina!...
Na hii ndio Maana halisi ya Mapinduzi ya Burudani!! yani Tuheshimiane"

"Haya sasa wasanii kazi ni kwenu kuhakikisha una msimamo na hata unapotakiwa unataja dau litalowezesha kusaidia familia yako kesho na kesho kutwa...
sio tena kujipeleka halafu kesho kuleta malalamiko eti ooh umenyonywa! utakuwa ni ujinga wako..
sie tushaanza kumaliza kazi!! "

Source:
 
Watanzania tunasjikiwa akili sana, na wanajua kucheza na akili zetu haswaaa. Acha wapige hela maana wajinga ndio waliwao.
 
Clouds ni matapeli
Utapeli wao ni upi?? Media zipo nyingi, vipi mnaona ni wajibu wa clouds ku-promote wasaini wadogo??? Huu ni uzwazwa, wanafanya biashara hawa siyo Charity, wanaangalia faida sawa na mfanyabiashara mwingine yeyote. No ujinga kumwandama mtu kwenye biashara zake.

Wasafi imeanzishwa, wacha hao wasaini waende huko, hayo ndiyo maendeleo
 
Thamani ya kitu utakijua pale unapokikosa

Thamani ya Boss Ruge Mutahaba sasa inaanza kuonekana

Tangu niwafahamu Clouds kwenye Tamasha la Fiesta 1999, Safari Hii ndio Fiesta iliyo kosa msisimko Kwa ukosefu wa ubunifu wa kuja Na kitu kipya

Ugua pole Akili kubwaaz Ruge
 
Mbio za sakafuni huishia ukingoni, mwakani tutakuwa hapa tukijiuliza mbwembwe ziko wapi. Kuna mmoja uwa anamkimbiza mwizi kimya kimya kelele anapiga mwizi mwenyewe
Ayo mshayasema sanaaa mumemtabilia kuanguka toka 2011 hadi sasa bado ngojeni mtazidi kuyaona makuu
 
Back
Top Bottom