Diamond, Dbanj, Banky W na Waje kufanya remix ya wimbo wa One Campaign

Diamond, Dbanj, Banky W na Waje kufanya remix ya wimbo wa One Campaign

Kidingi

JF-Expert Member
Joined
Aug 11, 2012
Posts
1,872
Reaction score
1,832
Muimbaji wa kundi la Rock la U2 na mwanzilishi wa One Campaign, Paul David Hewson maarufu kama Bono amewakutanisha wasanii wa Afrika wakiwemo Diamond, Banky W, D'Banj, Omotola, Waje na wengine kutengeneza remix ya wimbo ‘Strong Girls' ambao ni sehemu ya kampeni hiyo.

D'Banj, Diamond na Banky, Mastaa hao wamekutana jana jijini Lagos, Nigeria. Katika post aliyoweka Banky W kwenye Instagram ameandika:

Lol.. how cool is it to be photo-bombed by BONO? Diamond platnumz, Waje big ups to one campaign for the "strong girl" remix project, we are all working on."

Awali wimbo Strong Girls uliimbwa na wasanii wa kike tu wakiwemo Yemi Alade, Waje, Vanessa Mdee na Victoria Kimani.
 
Kazi kazi ndio mwendo, oyeeeeee Chibu

nea awards zimebaki siku mbili, msisahau kupiga kura
 
Diamond yuko bize na kampeni za ccm, hiyo collabo ataifanya saa ngapi?
wakati unashangaa kwa yeye kuwepo Lagos Nigeria,na leo hii anatakiwa awepo Zanzibar Ngome Kongwe kutumbuiza na shoo inamuhusu yeye.
 
woyooooo hapa ni kazi tu!toa kitu weka kitu che che cheki hichi kitu
 
Back
Top Bottom