Hance Mtanashati
JF-Expert Member
- Sep 7, 2016
- 20,137
- 26,189
Wiki hii huko mitandaoni haswa Instagram kuna machafuko makubwa ambayo sababu kubwa ni madai kwamba Diamond Platnumz amewadhalilisha wanawake anaotembea nao ambao wanaosemwa haswa kwamba hilo dongo ni lao ni pamoja na Hamisa Mobeto na Zarina Hassan.
Mtafaruku huu kwa kiasi kikubwa umefanya baadhi ya mashabiki wa kike kuanza kususia kazi zake haswa hii Jibebe iliyotoka hivi karibuni kwa madai kwamba Diamond anawadhalilisha sana jinsia yao kutokana na maneno yake machafu ya mara kwa mara ambayo licha ya kuonywa lakini bado hasikii.
Mwanadada Rachel Temu ni mmoja ya wanawake ambao wamechukizwa sana na kauli ya diamond aliyoitoa mwanzoni mwa wiki hii kwa kumfananisha mwanamke na Kima.
Lakini kiukweli kwamba madai yote wanayoyaelekeza kwa Diamond ni batili na mengi yanafanywa na haters wa Diamond Platnumz ambao kwa namna moja au nyingine wana nia ya kumshusha kimuziki maana waswahili husema "Penye neema ya Mungu husda lazima iwepo" ila yote kwa yote aliyepewa amepewa tu hata wafanye nini hawataweza kumshusha Simbaaaa watashindana lakini hawatashinda zaidi na zaidi watajipotezea muda wao bureee.
Ukweli ni kwamba Diamond alimuita Kima yule msichana aliyejifanya anamjua jua sana kiasi kwamba anaanza kumuingia katika maisha yake binafsi badala ya muziki wake, sio kweli kwamba amewaita kima mademu zake.
Diamond ingawa mara kwa mara wanamchafua ,yeye siku zote huwa hajibu kitu ila kwa huyu msichana alivuka mipaka ndipo Diamond akaamua kumpa za uso bila huruma.
Mtafaruku huu kwa kiasi kikubwa umefanya baadhi ya mashabiki wa kike kuanza kususia kazi zake haswa hii Jibebe iliyotoka hivi karibuni kwa madai kwamba Diamond anawadhalilisha sana jinsia yao kutokana na maneno yake machafu ya mara kwa mara ambayo licha ya kuonywa lakini bado hasikii.
Mwanadada Rachel Temu ni mmoja ya wanawake ambao wamechukizwa sana na kauli ya diamond aliyoitoa mwanzoni mwa wiki hii kwa kumfananisha mwanamke na Kima.
Lakini kiukweli kwamba madai yote wanayoyaelekeza kwa Diamond ni batili na mengi yanafanywa na haters wa Diamond Platnumz ambao kwa namna moja au nyingine wana nia ya kumshusha kimuziki maana waswahili husema "Penye neema ya Mungu husda lazima iwepo" ila yote kwa yote aliyepewa amepewa tu hata wafanye nini hawataweza kumshusha Simbaaaa watashindana lakini hawatashinda zaidi na zaidi watajipotezea muda wao bureee.
Ukweli ni kwamba Diamond alimuita Kima yule msichana aliyejifanya anamjua jua sana kiasi kwamba anaanza kumuingia katika maisha yake binafsi badala ya muziki wake, sio kweli kwamba amewaita kima mademu zake.
Diamond ingawa mara kwa mara wanamchafua ,yeye siku zote huwa hajibu kitu ila kwa huyu msichana alivuka mipaka ndipo Diamond akaamua kumpa za uso bila huruma.