Diamond laana hiyo!

Nakumbuka kuna wakati Msanii Mzee Magari alifuatwa na dogo mmoja akidai Magari ni baba yake, Magari alimchimba yule dogo biti asimfuatefuate...ingawa hatujui ukweli ni upi lakini nili/tuliweza kupata picha ya Baba anayemkataa mtoto asiyemuhitaji....je yule mtoto angekuwa ni Diamond Magari angemtosa ?

Hiyo laana ni ya muandishi kwenda kwa Diamond lakini sio ya Baba kwenda kwa Diamond.
 

walewale
 

Ukwel mtupu
 

Hahahaha negatives hizi tukizichukulia kipostive nahisi mahakama zisingekwepo.na majambazi yatajitetea serikali ingetupa ajira tusingekuwa majambazi.
 
Sehemu kubwa ya changamoto wanazopitia kina mama chanzo ni wanaume, hata watoto wanaotupwa, kuuwawa au kutelekezwa mahali/mitaani ni matokeo ya mama kuachiwa mzigo wote na mwenzi wake, kuna maelfu ya kina mama waliopata watoto walemavu wamekimbiwa na wazazi wenza wa kiume.

Diamond kumsaidia huyo bwana ni jambo moja lakini kamwe tusitake kuwatunuku wazazi/wababa wa aina hiyo wasiotaka kuwajibika kwa mazao yao kana kwamba hii dunia inampa uhuru mwanaume kufanya anavyotaka.

Kama hakumuhitaji mtoto Diamond, basi tafsiri yake ni kuwa kama Diamond angefariki utotoni basi huyo mdingi angesema afadhali.

Laiti mngepata fursa kusikiliza mamia ya kina mama wanavyoelezea mateso waliyowahi kupitia baada ya kupata mimba na mwanaume anayehusika kuingia mitini kuendelea na maisha mengine...unasikiliza unatokwa machozi mtoto anaugua mama hana hata pee ya kumpeleka mtoto hospitali, wanashindia uji breakfast, lunch na dinner...alafu leo huyo baba aitwe shujaa.

Huyo bwana aombe msaada kwa Diamond kama ambavyo angeomba mtu mwingine yeyote lakini isiwe kwa kigezo tu cha kuwa yeye ndiye baba ili hali hakutaka kuwajibika.
 

Kwa hiyo na yule binti Malala Yousfazai ashukuru kuwepo kwa Taliban, kwa kumtwanga risasi ya kichwa wamemfanya akawa binti maarufu/shujaa.
 
Huyo Mzee Ateseke Tu, Me Mwenyewe Uwa Naumiaga Sana Kuona Watoto Wapo wapo Wanavaa Ovyo, Shule Hawaendi, Na Baba Zao Wapo Kazi Kulewa Tu Na Kutokujali Watoto, Na Haya Yote Yanasababishwa Na Ngono Za Ovyoovyo Mtu Mwingine Unakuta Kuipata 5000 Kwa Siku Mtihani Lakini Ana Watoto 5 Ivi Utawalea Vipi Matokeo Yake Anaona Solution Ni Kuikimbia Nyumba, Kama Wewe Mwenyewe Ela Ya Kula Kuipata Ni Mtihani, Iyo Ya Mwanamke Na Kulea Mtoto Unaipatia Wapi, Una Pesa Kaa Tulia Piga Ny_to Usitake Kuzalisha Na Wewe Uonekane Umezalisha..
 
Mzazi ni mzazi tu!
Kama humtaki baba yako badili jina uitwe la mama yako...JIPANGE
 
Mzazi ni mzazi tu!
Kama humtaki baba yako badili jina uitwe la mama yako...JIPANGE

Hilo nalo neno, baniani mbaya kiatu chake dawa, baba yake hamtaki ila jina lake anatumia si ajiite nassib sanura ***** zake mfyuu
 
hiyo laana haiwez kumpata....na iwe fundisho kwa midume inayokataa watoto

Tena wala haimpati ng'oo iyo laana hawa mababa wanachokijua ni kupachika mimba tu na kutimka nampa big up diamond asirudi nyuma wala nini uyo baba akitaka msaada aende kuchukua kwa watoto wake aliowakubali na kuwalea toka wakizaliwa shenz kabisa
 
Inataka moyo sana kukataliwa na mzaz co kitu kizuri yaan ckien ila lisikukute
Ukitaka kupata picha ya maumivu ya kukataliwa, imagine tu pale unakutana na mshikaji mahali unaanza kumshobokea halafu anakupotezea anakuambia hakujui..... n mshikaji tu huyo, lakini full maumivu!!
 
Na labda angemsomesha, huenda angekuwa ni mwanamuziki mwenye mafanikio zaidi kv angekuwa mwanamuziki msomi... sina haja ya kukumbusha kwamba kusoma si sababu ya mtu kutokuwa mwanamuziki bali kusoma kunaweza kukufanya mwanamuziki wa aina nyingine tofauti kama usingesoma!
 

NDomo alishawah kukir kuwa mziki haukuwa kwenye ndoto yake, hali ngumu ya maisha na ufukar ndiyo vilisababisha ajaribu bahat kuimba na ndio maana alianza ku rap coz alikuwa hajui kama anawez kufany ivi anavyofanya sasa

Njia za mungu ni kubwa na unpredictable mkuu so angetakiwa kushukur kwa kila kitu na ndio maana tabu zote na mateso had leo bado yupo hai mkuu its all about Gods plan nothing else. Mungu alimjua kabla na hata uko baadae so he should be thankful for all wat has happened to him
 
Binafsi siungi mkono kumtupa huyo "baba ake" hasa katika kipindi kigumu lakini vile vile siwezi kufumba macho ili nisione how Diamond feels against his own dady... haya mambo kwa mtu ambaye hayajamkuta anaweza asielewe... unaweza kuta mzima alikuwa anatolewa nduki huku anazodolewa!!! Wakati mwingine mtu unatakiwa uwe na upako kusahau kila kitu lakini ordinary human mind unaweza isihia kama anavyofanya Diamond... unaweza kukumbuka siku ulipoumwa hadi unakaribia kufa halafu m-sure hana time vile vile!!!
 
watu hawajui mamake alihangaika vipi na mtoto ..baba mtu si alimbwaga mtoto akihisi anapunguza najukumu...sasa atulie tu sio kupiga kulele hasaidiwi wakati yeye hakusaidia
Hata asipomsaidia mbele za Mungu yule ndio baba yake full stop.Hizo hasira na kelele tuu ndugu na Diamond hata kaa apate baba mwingine tena yupo 1 ndio huyo huyo.
 
Nafikiri mtu mwenye kuweza kumpatanisha diamond na baba yake ni mama wa diamond, na inaonyesha Hana dalili ya kufanya hivyo kwasabab ya upungufu wa hekima regardless ya mateso aliopitia. Hata jay z alipatanishwa na baba yake kwa busara ya mama yake! Diamond Hana father figure wa kum guide kimaisha Ukiangalia tabia na matendo yake yana vinasaba vya kike zaidi kwa vile malezi yake alilelewa na mama tu, I hope he's wise enough to reconcile with his father before he's gone for good pengine ndio atakuja kugundua kiasi gani ilikuwa muhimu kupatana na baba yake! Hakuna hata mmoja wetu anayejua kwa uhakika kwann baba yake alikimbia Mimba ya diamond kuna watu wanadai mama yake alikuwa muuza pombe za kienyeji watu wengi walikuwa wanajipigia tu kwa starehe zao, Ni wakati muafaka ajue kisa cha baba yake kukimbia na Sidhani Kama alishawahi kufanya hivyo! Zaidi ya kushibishwa maneno ya upande mmoja. Kuna mambo inabidi wakati mwingine ukubali ili yaishe ili upate Amani zaidi, visasi ni kwa watu wenye upungufu wa hekima, hata South Africa alipotoka Mandela walifanya reconciliation ya mambo yaliotokea huko nyuma.
 
Mzazi ni mzazi tu!
Kama humtaki baba yako badili jina uitwe la mama yako...JIPANGE

Ndio wazazi wengi wanafanya ivyo nakimbia majukumu nikijua mtoto atanitafuta tu huuu ni zaidi ya unyama mbona ww baba yako akukukana? Mie nampa big up diamond ningekuwa mie hata akifa sikanyagi mguuu dawa ya moto ni moto
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…