Mkumbuke, sasa, Muumba wako Mkuu katika siku za ujana wako, kabla siku zenye msiba hazijaja, au miaka iwe imefika wakati utasema: "Sipendezwi nayo"; [SUP]2[/SUP]kabla jua na nuru na mwezi na nyota havijawa na giza, na mawingu yamerudi, kisha mvua kubwa; [SUP]3[/SUP]katika siku ambayo watunzaji wa nyumba wanatetemeka, nao wanaume wenye nguvu wameinama, na wanawake wanaosaga wameacha kufanya kazi kwa sababu wamekuwa wachache, na mabibi wanaochungulia madirishani wameona giza; [SUP]4[/SUP]na milango inayoelekea barabarani imefungwa, wakati sauti ya jiwe la kusaga inaposhuka,+ naye mtu huamshwa na sauti ya ndege, na mabinti wote wa wimbo hutoa sauti ya chini.