Hakika Tanzania na Afrika mashariki kwa ujumla tunajisifu sana na uwepo wako hata wale wasiofuatilia muziki kwa juhudi, uthubutu, kujituma, na heshima yako inatoa fundisho kubwa sana.
Huyu mtu hakika ni chuo cha Bongo flavour, na haikukosewa kabisa kumuita Nembo ya Taifa la Tanzania, bado tu kutengeneza sanamu yake na kuipa barabara/shule/hospitali jina lake kumuenzi, kwani amekuwa chachu ya maendeleo ya vijana wengi hususani wanamuziki, na wengi wamekiri hili wakiwemo Joh makini, alikiba, Sauti sol, Vanessa mdee, Belle 9, Nicki wa pili, n.k.
Huwezi ukaandika mazuri ya huyu mtu afu ukamaliza kwani ni mengi mno.
Huyu jamaa ukianzia kwenye label yake tu ameonyesha heshima ya muziki wake, kwani unaendesha familia nyingi mno. Wakati wasanii wengine wakifanya mambo kienyeji, kufanya muziki ili kupata pesa kula bata mjini huku wakisahau kuwekeza zaidi kwenye kazi zao, diamond amewapa mwangaza kwenye hili.
Kuanzia kwenye management, kwa Tanzania anao mameneja si chini ya wa4 salam, babu tale, fela na ricardo momo, bado Nigeria ana manager mmoja Paulo. Ana mpiga picha wake(kifesi), ana mchukua video wake(akili), anao madancers wa kudumu zaidi ya 6, ana mlinzi wake. Bado kwenye ofisi za WCB kuna waajiliwa, akiwemo producer, msimazi wa ofisi, n.k
Kama haitoshi akatuletea Harmonize ambae kwa video yake ya kwanza tu kafanikiwa kuonekana hadi mtv base kitu ambacho wasanii kama alikiba, richi mavoko, ben pol, barnaba, hawajawahi kufanikisha,,, ila diamond kwa moyo mkunjufu kamtoa harmo mtaani alikokuwa muuza chai kariakoo, na muda mwingine kuuza mitumba karume akamuhudumia kisanaa mpaka kufikia alipo, na wiki iliyopita alikuwa anashoot video yake ya pili na God father hapa nchini pamoja na RAYMOND msanii mpya anayesimamiwa na diamond.
Diamond hakuwa wa kwanza kuanza kuwekeza kimataifa, kulikuwa na AY hapo kabla.. Ila ukijiuliza kwanini kumekuwa na kasi kubwa ya wasanii wetu kukazana kutoka kimataifa kuanzia 2015? Hii imetokana na mafanikio ya Diamond, ambaye ameifanya Tanzania itambulike kimuziki pia.. Mafanikio yake yamewafanya wasanii waone kunauwezekano wa kufanya haya na ukafanikiwa, hamasa ambayo haikuwepo hapo mwanzoni.
Ikumbukwe mengi sana amefanya huyu mtu, kipindi wasanii wanalipwa pesa ndogo sana kwenye show Diamond alianza kuwaonyesha thamani yao, ambapo 2013 mwanzoni akasema bila milioni kumi siwezi kutumbuiza kwenye show, na jinsi alivyokuwa anafanya vizuri gharama ikazidi kupanda mpaka 2014 baada ya kutoa my number one remix ikawa milioni 25, mpaka mwaka huu kuja kulipwa milioni 100 kwenye tigo kiboko yao concert pesa ambayo wasanii wengine zaidi ya kumi gharama ndio inafikia hiyo..
VIVA DIAMOND PLATNUMZ, KING OF AFROPOP
Huyu mtu hakika ni chuo cha Bongo flavour, na haikukosewa kabisa kumuita Nembo ya Taifa la Tanzania, bado tu kutengeneza sanamu yake na kuipa barabara/shule/hospitali jina lake kumuenzi, kwani amekuwa chachu ya maendeleo ya vijana wengi hususani wanamuziki, na wengi wamekiri hili wakiwemo Joh makini, alikiba, Sauti sol, Vanessa mdee, Belle 9, Nicki wa pili, n.k.
Huwezi ukaandika mazuri ya huyu mtu afu ukamaliza kwani ni mengi mno.
Huyu jamaa ukianzia kwenye label yake tu ameonyesha heshima ya muziki wake, kwani unaendesha familia nyingi mno. Wakati wasanii wengine wakifanya mambo kienyeji, kufanya muziki ili kupata pesa kula bata mjini huku wakisahau kuwekeza zaidi kwenye kazi zao, diamond amewapa mwangaza kwenye hili.
Kuanzia kwenye management, kwa Tanzania anao mameneja si chini ya wa4 salam, babu tale, fela na ricardo momo, bado Nigeria ana manager mmoja Paulo. Ana mpiga picha wake(kifesi), ana mchukua video wake(akili), anao madancers wa kudumu zaidi ya 6, ana mlinzi wake. Bado kwenye ofisi za WCB kuna waajiliwa, akiwemo producer, msimazi wa ofisi, n.k
Kama haitoshi akatuletea Harmonize ambae kwa video yake ya kwanza tu kafanikiwa kuonekana hadi mtv base kitu ambacho wasanii kama alikiba, richi mavoko, ben pol, barnaba, hawajawahi kufanikisha,,, ila diamond kwa moyo mkunjufu kamtoa harmo mtaani alikokuwa muuza chai kariakoo, na muda mwingine kuuza mitumba karume akamuhudumia kisanaa mpaka kufikia alipo, na wiki iliyopita alikuwa anashoot video yake ya pili na God father hapa nchini pamoja na RAYMOND msanii mpya anayesimamiwa na diamond.
Diamond hakuwa wa kwanza kuanza kuwekeza kimataifa, kulikuwa na AY hapo kabla.. Ila ukijiuliza kwanini kumekuwa na kasi kubwa ya wasanii wetu kukazana kutoka kimataifa kuanzia 2015? Hii imetokana na mafanikio ya Diamond, ambaye ameifanya Tanzania itambulike kimuziki pia.. Mafanikio yake yamewafanya wasanii waone kunauwezekano wa kufanya haya na ukafanikiwa, hamasa ambayo haikuwepo hapo mwanzoni.
Ikumbukwe mengi sana amefanya huyu mtu, kipindi wasanii wanalipwa pesa ndogo sana kwenye show Diamond alianza kuwaonyesha thamani yao, ambapo 2013 mwanzoni akasema bila milioni kumi siwezi kutumbuiza kwenye show, na jinsi alivyokuwa anafanya vizuri gharama ikazidi kupanda mpaka 2014 baada ya kutoa my number one remix ikawa milioni 25, mpaka mwaka huu kuja kulipwa milioni 100 kwenye tigo kiboko yao concert pesa ambayo wasanii wengine zaidi ya kumi gharama ndio inafikia hiyo..
VIVA DIAMOND PLATNUMZ, KING OF AFROPOP