Diaspora wa U.S.A wanaonekana maisha yamewapiga japo wanaishi U.S.A kwenye katiba bora duniani, nadhani si Kila jambo ni katiba

chiembe

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2015
Posts
16,859
Reaction score
28,112
Kwa kweli ukiangalia picha za hao Diaspora, unaweza kuyasoma maisha yao. Hakika wamepigika kimaisha, lakini wanaishi katika nchi yenye katiba bora kabisa, na uchumi mkubwa, nadhani tunahitaji mjadala mpana, maana Sasa hivi hata mtu tumbo likijaa gesi, unamsikia anasema solution ni katiba mpya.

Muangalie huyu mama, hata kunyoosha nguo hawezi, t-shirt chafu imejikunja kama imeliwa na ndama. Pia hata ukimsoma ni mtu mwenye matatizo ya kiuchumi. Pia inaonekana kazeekea huko U.S.A lakini hakuna alichofanikiwa kimaisha
 
Samia aliyenyoosha nguo amekimbia
 
Hii justification yako kuhusu katiba mpya kutokua na ulazima bado haijitoshelezi, tafadhali tupe sababu za msingi kama Taifa kutohitaji katiba mpya na imara kwa muongozo na dira ya Taifa!!
 
Huo mtazamo wako na hapa wazo bovu unayojaribu kulijenga ni mtazamo wako hasi dhidi ya wazo la kupatikana katiba mpya.Kukujulisha TU Hilo ni lengo kuu la Sasa na haliitaji kusubiri hata dakika Moja kutoka Sasa.Katiba mpya ni Sasa.
 
Mnatafuta justification ya kuendeleza Udikiteta na ukandamizaji lakini mwisho wenu uko karibu. Huyo aliyepigika Marekani na wewe unayeishi Kwa kutegemea kujipendekeza Kwa DC mnalingana?

Sent from my M2003J15SC using JamiiForums mobile app
Nakuvizia vizia corridor za Lumumba kupiga vizinga,SI Bora unayedai kapigika marekani
 
Unaijua lifestyle ya watu wanaokaa huko na mavazi yao yalivyo........hao watu kuvaa smart sijui mkanda nje na suti siyo priority yao. Wewe kisa hujawahi kutoka hapa tandale unafikiri lifestyle za watu zinafanana kote duniani......
 
Mnatafuta justification ya kuendeleza Udikiteta na ukandamizaji lakini mwisho wenu uko karibu. Huyo aliyepigika Marekani na wewe unayeishi Kwa kutegemea kujipendekeza Kwa DC mnalingana?

Sent from my M2003J15SC using JamiiForums mobile app
Yule wa marekani amepigika kuliko huyu wa Tanzania.
Yule kule hata mafao ya kukaa mtaani hapati kama hao wa marekani.

Pia inafikia mahali hawezi kujikimu hivyo anaishi kwa matatizo makubwa ughaibuni huku hata uwezo wa kujilipia ticket arudi nyumbani hawezi tena.

Usifikiri kuishi majuu ni raha kama mnavyochukulia.

Kule hata zile odd jobs lazima uwe na Documents halali.

Ndio chimbuko lao kulilia uraia Pacha.
 
Haraka haraka tusiwasahau hawa wafuatao, nao ni Diaspora pia; Uzalendo ukawasukuma wakaamua kurudi nyumbani otele pote mradi nao wasaudie kusukuma gurudumu la maendeleo: NYERERE, LIPUMBA, PENGO, SAMIA, BAGONZA, FATUMA (KARUME), MPANGO, BAREGU, NA LISSU. Ila huyu wa mwisho akainyea kambi akaona bora arudi majuu awe baunsa kwenye traffic packing.
 

"hata ukimsoma ni mtu mwenye matatizo ya kiuchumi" umejuaje .

Mark Zuckerberg wa facebook ana t-shirt za aina mmoja tu za $5 kwa t-shirt. Kuvaa ni utamaduni sio pesa wala nini ni ushamba tu. Kuna Masikini wengi Congo wanavaa vizuri kuliko ma billionea wa USA​










 
Diaspora wote Duniani wa nchi zote, hawalingani, wako Diaspora ambao wako njema, na kuna diaspora choka mbaya. Nikiwa US, Boston, Massachusetts, kuna Diaspora mmoja, mama wa Kitanzania, mwenye watoto wawili, alifiwa na mzazi wake huku Tanzania, watu tukamchangia, ili aje kuwahi mazishi. Kulikuwa na Mkutano mkubwa wa kimataifa wa APARC pale BU, Watanzania tuliokuja mkutanoni tukajichanga, zilipatikana pesa ndefu, huyo mama akapewa fasta ili kumwezesha yeye na wanawe kuja home kuhudhuria mazishi.

Baada ya kukabidhiwa fungu, Mama wa watu, na kuishi kote Marekani, kumbe hajawahi kushika pesa ndefu hivyo mkononi at a go!, mama akajishauri, aje na baada ya mazishi, what next?.

Akaaamua kubaki US na kulitumia lile fungu kubadili maisha. Diaspora wa New York wako OK, hata diaspora wa DMV, ila Diaspora choka mbaya pia wapo ila don't judge a book by it's cover, usikute huyo mama it's just a look but she is loaded!.
P
 
Dah ila wazalendo mnapenda shari sana. Haya yote umeyaona kwenye picha tu?😀😀
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…