Diego Simeone ni kiboko ya Jurgen Klopp

Diego Simeone ni kiboko ya Jurgen Klopp

NAMBA MOJA AJAYE NCHINI

JF-Expert Member
Joined
Oct 29, 2019
Posts
9,863
Reaction score
20,806
Hii ni mara ya pili nikishuhudia mpambano mkali kati ya Simeone na Klopp na mara zote Klopp kapoteza pambano.

Kwa mara ya kwanza mtanange wa Audi Cup fainali uliopigwa Alliance Arena jijini Munich nilimuona Klopp hana ujanja dhidi ya safu ya ulinzi ya Atletico Madrid mwisho wa mchezo Atletico lishinda kwa mikwaju ya penati! Jana nimecheki tena gemu kali kati ya miamba hii miwili na sikuona cha maana kutoka kwa Liverpool!!!hawakupiga shuti hata moja lililolenga goli!!!atl.

Walikuwa smati sana jana kina Salah, Firminho na Mane wote hawakufua dafu mbele ya safu kali ya ulinzi ya Atletico! Nadhani gemu ya marudiano pale Anfield hali itakuwa ngumu sana kama Atletico wakiwa smart kujilinda kama jana!!!

Viungo wa liverpool walikosa ubunifu wa kupenyenza mipira kuwafikia kina mane na wenzake!!!Klopp ana kazi kubwa sana kuifunga safu ya ulinzi ya Atletico Madrid na kuwazuia wasifunge pale Anfield.

Ngoja tuone. Je, bingwa mtetezi kutolewa kwenye hatua ya 16 bora?

KLOPP WATCH OUT!!!!

Diego Klopp.jpg
 
Kwani si bado mechi nyingine?
Kama ndo hivi basi simeone ni kiboko ya kila mtu..
Maana alimfunga juve home kwenda away kala kibano kapigwa na Madrid final kama 2 za UEFA..

Halafu hilo kombe la Audi nalo kombe? Si linakuwaga kipindi wachezaji wameenda likizo? So wanapanga vitoto tu..

Tusubiri mechi ya pili week zijazo apo then tutaongea..
 
Barca na Messi walifunga 3 pale camp now ila walivyokuja anfield kila mtu anajua nini kiliwakuta.
Tupo half time wameshinda kwao goli mpoja bila nasubili thread yako nyingine baada ya wiki 2 ikiisuppport hii hapa.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kuna wapumbavu bado hawaamini philosophy ya Diego au Mourinho, bila mitanange kama hiyo soka litapoteza mvuto sana.
Diego simeone anafundisha mpira ambao yeye aliucheza,kukaba mwanzo mwisho,nguvu,akili na kutokufanya makosa ya kuigarimu timu,

Ata aina ya wachezaji anawasajili ni wale watakao weza kumudu fomula yake

Sent using Jamii Forums mobile app

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom