Digital marketing Tanzania bado ni hovyo kabisa

Digital marketing Tanzania bado ni hovyo kabisa

The Evil Genius

JF-Expert Member
Joined
Mar 21, 2014
Posts
6,017
Reaction score
19,506
Habari wakuu.

Hii biashara ya kutangaza bidhaa zako kwenye mitandao naona bado haijaeleweka vizuri hapa Tanzania.

Wafanya biashara wengi bado wana uswahili mwingi sana. Mtu anatangaza biashara yake mtandaoni hasemi iko wapi, haweki bei na wala hatoi maelezo ya kueleweka.

Mimi ni mpenzi wa kununua bidhaa mitandaoni ila kwa kweli wafanya biashara wetu wengi bado hii fursa hawajaielewa.

Nenda kupatana, unakutana na bidhaa nzuri lakini muuzaji hajaweka bei, hasemi anapatikana wapi na wala hajaweka maelezo ya kutosha kuhusu bidhaa zake, hivyo hivyo zoom Tanzania. Yani anataka umpigie sim ndio umuulize bei ya bidhaa yake muanze kujadiliana.

Wengine wanafanya biashara kupitia social media kama instagram, unakuta mtu kaweka au anatangaza bidhaa au huduma yake cha ajabu account yake kaiweka private, yani hadi umfollow ndio uone anachoiuza, hovyo kabisa.

Online stores nyingine kama jumia, ebay nk wao wanaweka kila kitu ushindwe mwenyewe, watanzania lazima tubadilike, hii mambo ya kufanya biashara kwa mazoea hatuendi popote.

Ahsante.
 
Kweli kabisa Mkuu,ila kwa sasa sisi tuna platform ya kufanya manunuzi online tunaiandaa soon itakua hewani na natumai itakua bora zaidi na hizo platform nyingine maana tumeona makosa mengi waliofanya hao kina kupatana na zoom Tanzania...
 
Kweli kabisa Mkuu,ila kwa sasa sisi tuna platform ya kufanya manunuzi online tunaiandaa soon itakua hewani na natumai itakua bora zaidi na hizo platform nyingine maana tumeona makosa mengi waliofanya hao kina kupatana na zoom Tanzania...
Vizuri. Mnapotengeneza hizi platform hakikisheni kipengele cha bei ni cha lazima, kwamba tangazo haliwezi kwenda hewani bila bei. Huo ndio udhaifu mkubwa ambao kupatana na zoom wanao, kurubusu matangazo bila bei na maelezo ya kutosha, wasaidieni wafanya biashara kwa kuwalazimisha waweke bei na maelezo ya kutosha ya bidhaa au huduma zao.
 
Kuna wengine aneweka namba ila kuna matatu hapokei..,haipatikani . au anakujibu kwa ukali
Only in Tz [emoji23][emoji23]
Hahahaa, umenikumbusha mwingine niligombana nae juzi jumatano.

Kaweka namba, nimampigia mara 3 hapokei, nikamtext whatsapp hakujb, baada ya siku 3 akanipigia anauliza nani, tena kwa ukali, nikamzingua sana.

Yani hii biashara bado kabisa hainaeleweka.
 
Kidogo watu wa jijini wakosiliazi na hizi biashara za mtandao mikoani bado sana watu hawaamini kama wanaweza wakauza bidhaa mtandaoni
 
Habari wakuu.

Hii biashara ya kutangaza bidhaa zako kwenye mitandao naona bado haijaeleweka vizuri hapa Tanzania.

Wafanya biashara wengi bado wana uswahili mwingi sana. Mtu anatangaza biashara yake mtandaoni hasemi iko wapi, haweki bei na wala hatoi maelezo ya kueleweka.

Mimi ni mpenzi wa kununua bidhaa mitandaoni ila kwa kweli wafanya biashara wetu wengi bado hii fursa hawajaielewa.

Nenda kupatana, unakutana na bidhaa nzuri lakini muuzaji hajaweka bei, hasemi anapatikana wapi na wala hajaweka maelezo ya kutosha kuhusu bidhaa zake, hivyo hivyo zoom Tanzania. Yani anataka umpigie sim ndio umuulize bei ya bidhaa yake muanze kujadiliana.

Wengine wanafanya biashara kupitia social media kama instagram, unakuta mtu kaweka au anatangaza bidhaa au huduma yake cha ajabu account yake kaiweka private, yani hadi umfollow ndio uone anachoiuza, hovyo kabisa.

Online stores nyingine kama jumia, ebay nk wao wanaweka kila kitu ushindwe mwenyewe, watanzania lazima tubadilike, hii mambo ya kufanya biashara kwa mazoea hatuendi popote.

Ahsante.
Tumeshaandaa hii hapa www.teknozoo.co.tz mkubwa na kila tatizo uliloliseama humo limepatiw ufumbuzi. Tumeanza na elecronics kwa sasa..
 
Ni kweli kabisa, online marketing bado ni kitu kigeni hapa. Wanaofanya wanafanya kienyeji. Lakini pia soko la kimtandao bongo lina changamoto nyingi. Watu hawana online experience yakutosha. Haya na mengine mengi ndio yamewakimbiza Jumia wakaamua kuikimbia bongo. Ni makosa makubwa kwa biashara kufanya tu advertising na branding halafu inasahau swala la customer experience.
 
Ni kweli kabisa, online marketing bado ni kitu kigeni hapa. Wanaofanya wanafanya kienyeji. Lakini pia soko la kimtandao bongo lina changamoto nyingi. Watu hawana online experience yakutosha. Haya na mengine mengi ndio yamewakimbiza Jumia wakaamua kuikimbia bongo. Ni makosa makubwa kwa biashara kufanya tu advertising na branding halafu inasahau swala la customer experience.

Jumia hawajakimbia bongo kisa mazingira sio rafiki kwa biashara yao jaribu fatilia kilichotokea nchi nyingine za africa usilopoke kama haufatilii habari


Sent from my iPhone using JamiiForums
 
Jumia hawajakimbia bongo kisa mazingira sio rafiki kwa biashara yao jaribu fatilia kilichotokea nchi nyingine za africa usilopoke kama haufatilii habari


Sent from my iPhone using JamiiForums
I said it was among the reasons. Kama mazingira ni rafiki kwa biashara, what kind of a fool would decide to leave? By the way, have you ever bought anything online? Ile tovuti ya wasafi ya kuuza nyimbo uko wapi?
 
Back
Top Bottom