Diploma in Clinical Medicine kwenda Shahada ya Chemical and Processing Engineering

Diploma in Clinical Medicine kwenda Shahada ya Chemical and Processing Engineering

SHAIDI

JF-Expert Member
Joined
Aug 23, 2014
Posts
291
Reaction score
141
Habari ya asubuhi.

wana jf naomba kwa yeyote anaefahamu kama kuna uwezekano wa kusoma degree ya chemical and processing engeering kutoka kwenye diploma ya clinical medicine (clinical officer) naomba anijuze.

Kwa sifa za o leval certificate na diploma ya clin medicine kama kuna uwezekano.

Natanguliza shukrani.
 
Dogo haiwezekani kabisa,CPE ni pure engineering na unatakiwa uwe na foundation nzur ya phy, chemistry and mathematics, so huwez kabisa kusoma bachelor yake
 
Dogo haiwezekani kabisa,CPE ni pure engineering na unatakiwa uwe na foundation nzur ya phy,chemistry and mathematics, so huwez kabisa kusoma bachelor yake

ni kozi gani anayoweza kusoma?
 
nilikuwa nawaza niondoke kwenye faculty za medicine ni course gani nzuri yenye tija hasa za pure sciance
 
nilikuwa nawaza niondoke kwenye faculty za medicine ni course gani nzuri yenye tija hasa za pure sciance

Ndugu yng, usipotoke,usihame hyo course, ina future nzuri sana kwa maisha yako, ajira zake hazisumbui, then hata serikalini mishahara ya kada za afya si haba kabisa, komaa huko huko mkuu, hyo engineering unayotaka kwenda sana sana ufanye kazi viwandani, kwa mkemia mkuu hadi ushikwe mkono wakati hyo ya afya bila kushikwa mkono wala kimemo lazima ule shavu zuri, kazi kwako kusugua gaga kitaa au kula shavu.
 
nashukuru kwa ushahuri wana jf nitafanyia kazi mawazo yenu.
 
Habari ya asubuhi,

wana jf naomba kwa yeyote anaefahamu kama kuna uwezekano wa kusoma degree ya chemical and processing engeering kutoka kwenye diploma ya clinical medicine (clinical officer) naomba anijuze. kwa sifa za o leval certificate na diploma ya clin medicine kama kuna uwezekano.

natanguliza shukrani.

Ndugu yangu mpendwa wazo lako zuri lakini sio sahihi mtu aliyekushauri kubadili course kakupotosha kwa sababu zifuatazo.

1. sekta ya afya inalipa
2. Sekta ya afya ni rahisi kujiajili kwa lowest cost.
3. Ajira za Chemical Eng nchini ni sheeedah

Ukiachilia mbali TPDC kwingine ni kwa wahindi ambapo salary yake ni sawa na hiyo unayoipata ukiwa na CO.

4. Nakushauri kasome Pharmacy au MD ule mema ya nchi yaani ujiajili.
 
Back
Top Bottom