msemakweli10
JF-Expert Member
- Oct 14, 2013
- 229
- 46
Wana JF na wananchi wote Amani.
Nchi yetu ya Tanzania imekuwa ikisifiwa kuwa kisiwa cha Amani, watu wake ni wapole na wanyenyekevu.
Kutokana na utulivu uliodumu kwa takribani miaka 54 sasa, nchi yetu imekuwa ikikumbwa na majanga mbalimbali ya kidini na kisiasa.
Haitoshi kwa sasa nchi yetu inazoroteshwa na wachache wanaojiona wajanja na kuwaacha wananchi wakitaabika kwa matatizo yaliyo mengi ya kisiasa, kijamii na kiuchumi.
Kwa sasa iliyobaki katika nchi yetu imekuwa ni kutafuta ni nani mchawi ashugulikiwe.
Swali la msingi limekuwa, ni kweli amekuwa akitafutwa mchawi au mchawi anafahamika ila zinatumika tu propaganda za siasa ili kuendelea kuvuna kilichopo?
Viongozi wetu kwa sasa wamekuwa wajanja na wameingia kabisa kwenye viatu vya wale wasomi wa kigiriki (sophists), kukandamiza tabaka la chini na kujiimarisha wao wenyewe.
Ni lini basi tutajitambua na kufanya maamuzi yaliyo sahihi kupata viongozi adilifu?
Karibu kwa mjadala
Nchi yetu ya Tanzania imekuwa ikisifiwa kuwa kisiwa cha Amani, watu wake ni wapole na wanyenyekevu.
Kutokana na utulivu uliodumu kwa takribani miaka 54 sasa, nchi yetu imekuwa ikikumbwa na majanga mbalimbali ya kidini na kisiasa.
Haitoshi kwa sasa nchi yetu inazoroteshwa na wachache wanaojiona wajanja na kuwaacha wananchi wakitaabika kwa matatizo yaliyo mengi ya kisiasa, kijamii na kiuchumi.
Kwa sasa iliyobaki katika nchi yetu imekuwa ni kutafuta ni nani mchawi ashugulikiwe.
Swali la msingi limekuwa, ni kweli amekuwa akitafutwa mchawi au mchawi anafahamika ila zinatumika tu propaganda za siasa ili kuendelea kuvuna kilichopo?
Viongozi wetu kwa sasa wamekuwa wajanja na wameingia kabisa kwenye viatu vya wale wasomi wa kigiriki (sophists), kukandamiza tabaka la chini na kujiimarisha wao wenyewe.
Ni lini basi tutajitambua na kufanya maamuzi yaliyo sahihi kupata viongozi adilifu?
Karibu kwa mjadala