DIT&Mbeya University of Technology for what if no achievements?

Mshinga

JF-Expert Member
Joined
Feb 5, 2013
Posts
3,532
Reaction score
1,126
DIT ni chuo cha tekinolojia bila tekinolojia, kimepoteza mana na kushindwa kusadifu jina na kuwa mhimili wa tekinolojia kwenye taifa lisilo na tekinolojia hata ya kuiba, kimegeuka chuo cha kutoa wafanyakazi watoa huduma badala ya wagunduzi na ugunduzi, mbeya university of technology nayo inafata yaleyale ya DIT katika uchanga wake
 

Uko sahihi!! Na mimi naomba kuongezea....
Sio dit na MUST tu ila vyuo karibia vyote naona ni hamna jipya!!! Tukia na vyuo kama UDSM, SUA.. vyote vinayegemewa katika kuleta maendeleo ya nchi...ukianzia uhandisi...kilimo...uchumi...sheria na mengine mengi lakin mpaka leo wahandisi toka nje wanatupiga bao!!!

Ni dawa gani imegunduliwa Tz na ikatumika hata dunian kote? Mbona Mkuu wa kaya akiumwa kichwa anapelekwa india au US?? Lakin mda huo huo tuna kcmc..muhimbili na vingine vingi vimejazana tu!!!

Chuo cha usafiri dar...kinazalisha mainjia wa magari je ni gari gani limegunduliwa na likatumika hata hapa nyumbani??

SUA kwa upande wao wanazalisha wahandisi..na wanasayansi wa kilimo lakin je ..kilimo tanzania kikoje??

Juzi juzi nlisikia kuna mradi mkubwa unafanywa na makampuni ya nje wakat tunao wataalam wengi wa kudizain (achitects) kutoka ardhi...je hawa walikua hawapo???

Migodi mikubwa ...uchimbaji unafanywa na makampun ya nje je udsm ..udom..kote huko hamna hawa wataalam??

Juzi juzi gesi imegundulika je hii miradi ya uchimbwaji na uzalishaji wa gesi iko chini ya watanzania? Na mda huo huo tuna maprofesa na watalam wengi wa gesi tokea udsm...udom wamekaa tu kama hawajui!!

Kwa kifupi elimu ya tanzania bado iko chini na huu ndo ukweli...sio kuwalaum dit na must kwa kushuka kwa technolojia hili sio kosa lao!! Lazima tubadilike hasa katika mfumo wa kielim na kisiasa...
 
hatuna chuo hata kimoja kinachostahili sifa,tunahitaji education reform kuanzia chini mpaka juu,watu wanajisifia kusoma hapa ama pale,DIT haina maana kwa dhima na malengo yake.hata wanafunzi wake hawaelewi kuwa wanahitaji kugundua ama kutengeneza tekinolojia,wanaenda pale wakijua wanaenda kusomea ajira. hatari sana. vyuo vyetu lazima tuviangalie upya ili visaidie taifa tofauti na sasa vinatoa makanjanja tu
 
pelekeni stress zenu za kufeli huko.
mbona unatoa povu,hili limeingiaje kwenye mada?wewe unaona ni sawa kuwa na vyuo vya tekinolojia ambavyo havina uwezo huo?kwa taarifa yako sijawahi kufeli.
 

.
Mkuu tumia vizuri SPACE naona post zako nyingi ukifanya hiv!
.
Got 'Em Dope
 
mbona unatoa povu,hili limeingiaje kwenye mada?wewe unaona ni sawa kuwa na vyuo vya tekinolojia ambavyo havina uwezo huo?kwa taarifa yako sijawahi kufeli.

Kitendo cha kuandika huu ujinga tayari umefeli
 
Kitendo cha kuandika huu ujinga tayari umefeli
siku zote umeonyesha uwezo mdogo sana na huna uwezo wa kujenga hoja zaidi ya chuki na matusi kama kigezo cha kujilinda na uwezo wako mdogo wa kutetea unachokiamini,sioni haja ya kuendelea kujadili nje ya mjadala kwa sababu ya chuki zako.
 
Nashukuru kwa kuliona hilo
ameona nini?just a tabularasa imagination,sijawahi kufeli kama mawazo yake yalivyomtuma na kama unavyofikiria,I am very firm kila idara na kama wewe una unauwezo basi kosoa unachoona si sahihi,ila ukija na akili ya watu wasioelewa sitabishana na wewe mana kubishana na mjinga unakuwa mjinga pia
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…