Diwani wa Chadema Albert Msando amtetea wa CCM Rajab Nkya kortini

Chadema kama kweli wapo makini wasiwape hawo mawakili nafasi za uongozi katika chama chao, wabakie kama wanachama wa kawaida, mimi naona kama mchezo wa kuigiza wanafanya Chadema wanazunguka nchi nzima wanafanya maandamano huku wanataja orodha ya MAFISADI, cha kuchekesha MAFISADI wakifishwa mahakamani hao hao viongozi wa Chadema mawakili wanachukuwa pesa za MAFISADI wanawatetea mahakamani kuwa hawa sio MAFISADI, hizi ndio siasa za Tanzania utapeli mtupu
 
Kwa hiyo mie kama ni mhandisi rostam akinipa kazi ya kihandisi nisifanye? Mie nitafanya sana

Ata akitoa msaada kwenye chama chenu chukueni hamna tatizo Kiongozi, hivi Rostam Azizi kwenye orodha yenu ya UFISADI mmemuweka nafasi ya ngapi?
 
Msando and the like are hypocrites..Kwenye majukwaa unapinga ufisadi kwa nguvu zote halafu unaingia mahakani kuutetea.
 
Msando and the like are hypocrites..Kwenye majukwaa unapinga ufisadi kwa nguvu zote halafu unaingia mahakani kuutetea.

I have already said it! It's not a good look for them if they want credibility. If they want to be activists, then be just that.

Don't openly affiliate yourself with any political party. That way people won't question your sincerity in the fight against ufisadi when you take up cases involving shady characters.

Anything other than that will come across as an empty charade.
 

Well done Albert Msando. Wewe ni mwanaCDM safi, mwenye kuamini na kuzingatia misimamo ya Chama chako.

WanaCHADEMA ni ndugu na WanaCCM, na hatuwezi kuwa maadui kutokana na itikadi zetu kutofautiana. Demokrasia na uhuru wa kweli CHADEMA inayohubiri inaruhusu hata wanafamilia kuwa katika vyama vya siasa tofauti.

Kinachotakiwa ni kwamba MwanaCDM akiona haki haitendeki kwa raia yeyote, ajitolee kumsaidia kwa nguvu zake zote. Hakuna kulala, mpaka kieleweke!!!!!!!!!!!!
 
Albert Msando naelewa wewe ni mtu makini sana.
Just move forward, tuko pamoja katika mapambano dhidi ya dhuluma na uonevu.
 

jamvin kunaitaj maandaliz ya fikra na si kukurupuka
 
jamvin kunaitaj maandaliz ya fikra na si kukurupuka

Naona ndugu yangu wewe unafata mkumbo tu, wewe bado member ndio unatakiwa maandalizi ya fikra ku-Argue. usiwe na fikra mbinuko au unatafuta umaarufu kumjibu Chatu Dume
 
WanaJF,

Ni kweli namtetea Rajab Nkya ambaye anashtakiwa kwa makosa mawili. Kuhujumu uchumi na kutumia madaraka vibaya. Mazingira ya kesi hiyo (bila kuathiri mwenendo wa kesi) yana utata.

Kwa muda mrefu diwani huyo amekuwa anashutumiwa kwamba aliuza kura yake Chadema na kwamba anashirikiana na viongozi wa chadema Hai kudhoofisha CCM. Kuna chuki na fitna nyingi zinaendelea dhidi yake. Hana msaada wowote kutoka kwenye chama chake.

Kwa kumtetea mtu anayetuhumiwa ni fisadi sio kwamba natetea ufisadi. Nikimtetea muuaji sio kwamba natetea watu kuua! Nikitetea kampuni isilipe kodi iliyokuwa assessed na TRA sio kwamba natetea watu wasilipe kodi.

Inawezekana mwungine asielewe kwanini namtetea Rajab Nkya, lakini kuna kila uwezekano anaonewa. Kama kweli amehujumu uchumi mahakama itaamua. Ninachotakiwa kutetea ni HAKI itendeke. Ni jukumu langu kama ilivyo jukumu langu kupinga ufisadi. Kama viongozi wa chadema wanaotuhumiwa kuandamana bila kibali na uchochozi wanaonewa kuna uwezekano pia Rajab Nkya anaonewa. Nitatenda HAKI bila kujali itikadi, dini, kabila wala kanda. Ni wajibu wangu kama kiongozi na wakali wa kujitegemea.
 
WanaJF,

Ni kweli namtetea Rajab Nkya ambaye anashtakiwa kwa makosa mawili. Kuhujumu uchumi na kutumia madaraka vibaya. Mazingira ya kesi hiyo (bila kuathiri mwenendo wa kesi) yana utata.

Kwa muda mrefu diwani huyo amekuwa anashutumiwa kwamba aliuza kura yake Chadema na kwamba anashirikiana na viongozi wa chadema Hai kudhoofisha CCM. Kuna chuki na fitna nyingi zinaendelea dhidi yake. Hana msaada wowote kutoka kwenye chama chake.

Kwa kumtetea mtu anayetuhumiwa ni fisadi sio kwamba natetea ufisadi. Nikimtetea muuaji sio kwamba natetea watu kuua! Nikitetea kampuni isilipe kodi iliyokuwa assessed na TRA sio kwamba natetea watu wasilipe kodi.

Inawezekana mwungine asielewe kwanini namtetea Rajab Nkya, lakini kuna kila uwezekano anaonewa. Kama kweli amehujumu uchumi mahakama itaamua. Ninachotakiwa kutetea ni HAKI itendeke. Ni jukumu langu kama ilivyo jukumu langu kupinga ufisadi. Kama viongozi wa chadema wanaotuhumiwa kuandamana bila kibali na uchochozi wanaonewa kuna uwezekano pia Rajab Nkya anaonewa. Nitatenda HAKI bila kujali itikadi, dini, kabila wala kanda. Ni wajibu wangu kama kiongozi na wakali wa kujitegemea.
 

Hapo unatekeleza wajibu Albert,Good!

 

Ndiyo matatizo ya kuchanganya siasa na kazi. Kwani huwezi tu ukawa wakili wa kujitegemea bila kuwa mwanaharakati unayejihusisha na chama fulani cha kisiasa? Au huo udiwani wa CHADEMA hauna ulaji wa kutosha hivyo inabidi kuwa na side gig? Na hapo sasa sijui side gig ni ipi, udiwani au uwakili.....utajaza mwenyewe. Lakini habari ndo hiyo, kwenye siasa perception is reality. Watu wakishakuona wewe mzushi na mganga njaa hata kama si kweli, itaonekana ni kweli. It's just the nature of the beast. Na ndiyo maana kwenye litigious societies kama Marekani mawakili ni moja ya watu wanaochukiwa sana.

Rostam Aziz akija kununua huduma zako za uwakili kuhusiana na kutuhumiwa kwake na ufisadi utakubali kumwakilisha?
 
NyaniNgabu,

Siasa unayofanya wewe mimi sifanyi. Kwanza perception hazinilazimishi kufanya au kutokufanya uamuzi fulani. Endapo nitaruhusu 'wanachofikiri' watu kufanya maamuzi nitakuwa najikosea pamoja na jamii inayonizunguka.

Tuna tatizo. Wengi wanaangalia zaidi jamii inaona nini badala ya kufanya kile ambacho ni HAKI. Huo ni unafiki.

Rostam ana HAKI ya kutetewa. Msingi mmoja wa Katiba ni 'innocent until proven guilty'. Huwezi kuupinga msingi huo hata kama ni Rostam au Lowassa. Ingekuwa inawezekana basi wangekuwa jela.

Tusiwe na siasa za unafiki. Tusiogope kusimamia maamuzi ya HAKI kisa watu wataonaje.

Kuhusu uwakili na udiwani, vinaenda pamoja. Ukisema eti niache moja nibaki na moja unakosea. Kama itabidi tufanye hivyo basi wengi tutakuwa nje ya siasa....kuna msemo sikumbuki ni MwanaJF gani anautumia...'siasa isiachwe kwa watu fulani pekee...'
 

..kumtetea fisadi sio kwamba unatetea ufisadi.
..Kumtetea mtu aliyeua sio kwamba unatetea wauaji.
...kutetea kampuni isiyolipa kodi sio kwamba unatetea watu wasilipe kodi.
Mifano yako hainiingii akilini.
Tunajua unapigania haki. Na wewe kama wakili wake unajua ukweli upo wapi. Siasa sometimes ni giza huwezi kuona hadi umulikiwe. Tutaongea mengi kwa sababu bado hujataka kutumulikia.
 

Dude!.........Kwa hiyo Msando aligombea Udiwani kupitia CDM ili apate ulaji mbali na fani yake ya Uwakili!...........halafu ukiwa Diwani wa CDM hivyo wewe unawakilisha CDM tu..............hizo societies za huko Marekani (especially Tea Parties za GoP) zimekuathiri mazee...........
 
Husninyo,

Niseme hivi, Rajab Nkya sio fisadi. Naamini hivyo. Tuhuma dhidi yake ni za kisiasa kama zilivyo za Mh. Mbowe, Dr. Slaa, Lema na wengineo.

Sio kwamba sielewi mkanganyiko unaoweza kuwepo. Nililaumiwa sana kumfungulia kesi Mh. Grace na Lucy Owenya kutaka tafsiri ya mahakama kuhusu uhalali wa Mbune wa Viti Maalumu kuingia kwenye Halmashauri kisa tu anafanya kazi kwenye Halmashauri hiyo.

Atakayenihukumu kwa hilo anakosea. Jukumu langu kama wakili na diwani ni kutetea HAKI. Sio HAKI ya Chadema pekee, ni HAKI ya mtu yeyote anayestahili kutendewa HAKI. Maoni ya jumla yasituzuie kusimamia yale tunayoaamini.
 
.................Tuna tatizo. Wengi wanaangalia zaidi jamii inaona nini badala ya kufanya kile ambacho ni HAKI. Huo ni unafiki.

...................Tusiwe na siasa za unafiki. Tusiogope kusimamia maamuzi ya HAKI kisa watu wataonaje...'

Well said Mkuu.......heshima mbele......
 
NyaniNgabu,
Siasa unayofanya wewe mimi sifanyi. Kwanza perception hazinilazimishi kufanya au kutokufanya uamuzi fulani. Endapo nitaruhusu 'wanachofikiri' watu kufanya maamuzi nitakuwa najikosea pamoja na jamii inayonizunguka.

Awali ya yote, mimi sifanyi siasa hapa. Mimi naona siasa. Wewe si diwani wewe? Na kama wewe ni diwani, hicho cheo kwako si cheo cha kisiasa? '"Lawyer" puhliiiiiz

Na unachosema perception ya watu haikuzuii kufanya ni sawa kabisa. Wewe fanya kile unachoona ni sawa na watu watakuhukumu kwa matendo yako pindi utakapoomba ridhaa yao. Na hapa ndicho tunachokifanya pia. Tunakuhukumu kulingana na hayo matendo na maamuzi yako. Ni haki yetu kufanya hivyo na wewe ni haki yako kuwa vyovyote vile utakavyo.

Tuna tatizo. Wengi wanaangalia zaidi jamii inaona nini badala ya kufanya kile ambacho ni HAKI. Huo ni unafiki.
Haki ni subjective kama ilivyo unafiki. Unachoona wewe ni haki mwingine anaona dhuluma. Tunachoona sisi kuwa ni unafiki wewe unaona ni ukweli. Such is life. Deal with it.

Rostam ana HAKI ya kutetewa. Msingi mmoja wa Katiba ni 'innocent until proven guilty'. Huwezi kuupinga msingi huo hata kama ni Rostam au Lowassa. Ingekuwa inawezekana basi wangekuwa jela.
Hilo nalielewa vyema sana. Ila wewe kama huelewi concept ya court of public opinion nakushauri ukajinadi kwake ili upate kuwa wakili wake halafu 2015 ugombee ubunge kwa tiketi ya CHADEMA.

Tusiwe na siasa za unafiki. Tusiogope kusimamia maamuzi ya HAKI kisa watu wataonaje.
Then choose one; CHADEMA affiliated activist or an independent attorney. Being what you are now makes you look bad, makes you lose credibility in the fight your party is waging, and worst of it all it makes you look like a sleazeball attorney who will do anything for money unless you tell me you are representing that CCM guy pro bono.

Kuhusu uwakili na udiwani, vinaenda pamoja. Ukisema eti niache moja nibaki na moja unakosea. Kama itabidi tufanye hivyo basi wengi tutakuwa nje ya siasa....kuna msemo sikumbuki ni MwanaJF gani anautumia...'siasa isiachwe kwa watu fulani pekee...'

Kwa hiyo kwa kutumia mantiki hiyo hiyo, wewe unaona ni sawa kwa mbunge ambaye ni mtunga sheria kuwa wakili kwa wakati huo huo akiwa mbunge? Manake mtu anaweza ku argue kuwa ubunge na uwakili vinaendana kwa hiyo hakuna ubaya wowote ule kuzifanya kazi zote mbili kwa pamoja. Mweh kazi tunayo hapa.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…