Dk. Kawambwa, umeshindwa nini kuvunja mkataba wa TRL?

Magezi

JF-Expert Member
Joined
Oct 26, 2008
Posts
3,359
Reaction score
702
Watanzania bado tuna machungu ya Chenge kutuibia vijisenti na akaviwekeza ughaibuni. Kumbe mdudu huyu huyu ndiye ali-sign mkataba baina ya serikali na Rites wakati huo akiwa waziri wa miundo mbinu, tena akijigamba kuwa alikuwa makini.....sasa madudu yake tunayaona.

Sasa tatizo langu ni kwa nini Kawambwa ana kigugumizi kuhusu kuvunja mkataba na wahindi hawa?? Kawambwa wewe ni Mechanical engineer lakini nashangaa unashundwa kuelewa kuwa wahindi wanataka kuitumia TRL kukuza shirika lao la reli (Rites). Wahindi wana kiwanda sasa hivi cha kutengeneza mabehewa, engines (japo siyo nzuri) sasa wanataka wavuruge mifumo yote ya kiufundi ili tuanze kuwategemea wao ktk kila kitu. Na wahindi na dharau zao wakisha hakikisha unawategemea, basi cha moto utakiona.

Kama mafundi wameweza kutengeneza engines zetu za zamani na kuweza kuzitumia kufanya kazi wakati wahindi walishasema hazifai na wakaleta za kwao kuikodisha TRL, kawambwa huoni kwamba huo ni ujanja wananutumia?? Unashindwa nini kuvunja mkataba?? Hata kama ni kulipa fidia, mbona tulikuwa tunawalipa na bado tunawalipa IPTL??

Tafadhali kawambwa unadhalilisha uhandisi wako......kama umeshindwa si ujiuzuru??....au na wewe uko kama Hosea anayesema hawezikuacha kitumbua chake hata kama anavunja sheria??
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…