Zak Malang
JF-Expert Member
- Dec 30, 2008
- 5,404
- 239
Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Dk Charles Kimei amechaguliwa kwenye mchakato wa kumtafuta Kinara wa Benki Afrika kwa mwaka 2013.
Mchakato huo unaendeshwa na African Banker Awards chini ya African Development Bank Group.
Kinara wa benki wa mwaka, ni tuzo inayotolewa kwa viongozi (CEO`s) wa sekta ya benki na fedha barani Afrika, ambao wamepata mafanikio makubwa kwenye mashirika yao hivyo kuleta maendeleo kwenye sekta fedha na uchumi kwa nchi zao.
African Banker Awards imechagua vinara watano wa sekta ya fedha Afrika kuingia katika mchakato huo, mmoja wao ndiye atakayejitwalia tuzo hiyo.
Zaidi ya Dk Kimei, wengine waliongia kwenye mchakato huo na nchi wanazotoka kwenye mabano ni Segun Agbaje wa GTB Bank (Nigeria), Aigboje Aig wa Imoukhede-Access Bank (Nigeria), Andrew Allly wa Africa Finance Corporation (Nigeria) na Jao Figuerdo wa Unico Bank.
Dk Kimei ni Mtanzania wa kwanza kuingizwa kwenye mchakato huu tangu kuanzishwa kwa tuzo hiyo zaidi ya miaka kumi iliyopita, npia ni pekee kwenye kinyang'anyiro hicho ambacho kimekuwa kikitawaliwa na benki kutoka Nigeria na Afrika ya Kusini.
Dk Kimei ambaye ni mchumi mwenye Stashahada ya Uzamivu, amefanya kazi sekta ya fedha kwa zaidi ya miaka 30 akitokea Benki Kuu ya Tanzania (BoT), alikokuwa Mkurugenzi wa Sera na Utafiti kabla ya kujiunga CRDB mwaka 1998 kama Mkurugenzi Mkuu.
Akiwa CRDB ameiongoza kutoka benki iliyokuwa ikijiendesha kwa hasara hadi inayoongoza nchini.
Benki hiyo imefanya marekebisho mbalimbali, ambayo yameiletea mafanikio na kuwa miongoni mwa benki zinazoongoza nchini.
Chanzo: Mwananchi
My Take;
CRDB chini ya Dr Kimei ni benki ambayo imetumika kisiasa yaani imekuwa ikishirikiana na mafisadi ndani ya utawala wa CCM. Katika tukio la EPA benki hiyo inayoelezwa kuwa ni ya wazawa ilihifadhi fedha zailizochotwa (zilioibiwa) kutoka BoT na wale wezi naye akakaa kimya.
Katika ule mchoto wa Kagoda mabilioni yaliwekwa katika akaunti sita za matawi ya benki hiyo na baadaye kuchotwa na watu eti hadi leo hawajulikani hadi leo!!! Hii inawezekana kwa benki kubwa kama hiyo kutojua ilimlipa nani mabilioni hayo na zile akaunti alizifungua nani?
Pili CRDB chini ya Kimei iliisaidia sana kampuni feki ya Richmond kuwapatia guarantee ya letter of credit kuisadidia ufisadi wao.
Kwa hali hii Dr Kimei hafai kupata tuzo hiyo.
Nawasilisha.
Mchakato huo unaendeshwa na African Banker Awards chini ya African Development Bank Group.
Kinara wa benki wa mwaka, ni tuzo inayotolewa kwa viongozi (CEO`s) wa sekta ya benki na fedha barani Afrika, ambao wamepata mafanikio makubwa kwenye mashirika yao hivyo kuleta maendeleo kwenye sekta fedha na uchumi kwa nchi zao.
African Banker Awards imechagua vinara watano wa sekta ya fedha Afrika kuingia katika mchakato huo, mmoja wao ndiye atakayejitwalia tuzo hiyo.
Zaidi ya Dk Kimei, wengine waliongia kwenye mchakato huo na nchi wanazotoka kwenye mabano ni Segun Agbaje wa GTB Bank (Nigeria), Aigboje Aig wa Imoukhede-Access Bank (Nigeria), Andrew Allly wa Africa Finance Corporation (Nigeria) na Jao Figuerdo wa Unico Bank.
Dk Kimei ni Mtanzania wa kwanza kuingizwa kwenye mchakato huu tangu kuanzishwa kwa tuzo hiyo zaidi ya miaka kumi iliyopita, npia ni pekee kwenye kinyang'anyiro hicho ambacho kimekuwa kikitawaliwa na benki kutoka Nigeria na Afrika ya Kusini.
Dk Kimei ambaye ni mchumi mwenye Stashahada ya Uzamivu, amefanya kazi sekta ya fedha kwa zaidi ya miaka 30 akitokea Benki Kuu ya Tanzania (BoT), alikokuwa Mkurugenzi wa Sera na Utafiti kabla ya kujiunga CRDB mwaka 1998 kama Mkurugenzi Mkuu.
Akiwa CRDB ameiongoza kutoka benki iliyokuwa ikijiendesha kwa hasara hadi inayoongoza nchini.
Benki hiyo imefanya marekebisho mbalimbali, ambayo yameiletea mafanikio na kuwa miongoni mwa benki zinazoongoza nchini.
Chanzo: Mwananchi
My Take;
CRDB chini ya Dr Kimei ni benki ambayo imetumika kisiasa yaani imekuwa ikishirikiana na mafisadi ndani ya utawala wa CCM. Katika tukio la EPA benki hiyo inayoelezwa kuwa ni ya wazawa ilihifadhi fedha zailizochotwa (zilioibiwa) kutoka BoT na wale wezi naye akakaa kimya.
Katika ule mchoto wa Kagoda mabilioni yaliwekwa katika akaunti sita za matawi ya benki hiyo na baadaye kuchotwa na watu eti hadi leo hawajulikani hadi leo!!! Hii inawezekana kwa benki kubwa kama hiyo kutojua ilimlipa nani mabilioni hayo na zile akaunti alizifungua nani?
Pili CRDB chini ya Kimei iliisaidia sana kampuni feki ya Richmond kuwapatia guarantee ya letter of credit kuisadidia ufisadi wao.
Kwa hali hii Dr Kimei hafai kupata tuzo hiyo.
Nawasilisha.