DK,SLAA; Amani,Mshikamano na Umoja bila Katiba bora haiwezekani!!

DK,SLAA; Amani,Mshikamano na Umoja bila Katiba bora haiwezekani!!

sokoinei

JF-Expert Member
Joined
Feb 27, 2012
Posts
1,832
Reaction score
566
Katibu mkuu wa CHADEMA TAIFA Dk Wilbrod Peter Slaa amesema kuwa Amani, Umoja na mshikamano bila kuwa na katiba bora haiwezekani!

Akihutubia maelfu ya Wafuasi na Wanachama wa CHADEMA katika mji wa Karatu huku akiwa na Mabere Marando alisisitiza kwamba katiba bora na yenye kuleta usawa kwa watu wote ni ile inayomjali masikini na mtu mdogo katikka nchi hii na ambayo itatoa fursa kwa kila mtu kufaidi rasilimali ya nchi hii tofauti na sasa ambapo Matajiri na viongozi ndio wanaogawana rasilimali ya nchi huku watanzania walio wengi wakibaki katika umasikini wa kutupwa.

Dk Slaa aliyasema hayo leo ktk muendelezo wa mikutano inayofanywa na chama cha CHADEMA kutafuta maoni ya wananchi juu ya rasimu ya katiba mpya.

Source; ITV habari saa 2 usiku.
 
Baba: Mwanangu mbona umeamka alfajiri
kwenda shule, kulikoni?
Mtoto: Baba namuwahi mwalimu wa bagia.
Baba: Mjinga sana wewe, badala ya kuwahi
elimu, wewe unawahi bagia?
Mtoto: Baba, unajua kiukweli kabisa kuwa elimu
haina mwisho, ila bagia mwisho saa nne.
 
Baba: Mwanangu mbona umeamka alfajiri
kwenda shule, kulikoni?
Mtoto: Baba namuwahi mwalimu wa bagia.
Baba: Mjinga sana wewe, badala ya kuwahi
elimu, wewe unawahi bagia?
Mtoto: Baba, unajua kiukweli kabisa kuwa elimu
haina mwisho, ila bagia mwisho saa nne.

Sijakusoma mkuu! What do you mean?
 
Ni kweli umoja,amani na mshikamano ni matunda ya haki na usawa kwa taifa lolote!
 
Back
Top Bottom