Dk. Slaa: Nitaendelea kuwaumbua CCM

Dk. Slaa: Nitaendelea kuwaumbua CCM

Facts1

JF-Expert Member
Joined
Dec 23, 2009
Posts
307
Reaction score
28
Na Joseph Mwendapole
31st December 2009


headline_bullet.jpg
Asema anachunguza kama mali zote zimelipiwa kodi
headline_bullet.jpg
Aahidi kuwa baada ya hapo ataweka wazi kila kitu


Slaa%282%29.jpg

Dk. Wilbroad Slaa


Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Dk. Wilbroad Slaa, amesema kuwa ataendelea kufichua ufisadi unaofanywa na Chama Cha Mapinduzi (CCM).

Dk. Slaa ambaye pia ni Mbunge wa Karatu (Chadema) ameendelea kuwaweka tumbo joto viongozi wa CCM, baada ya kutangaza kuwa ameanza kuchunguza mali zote za chama hicho kama zililipiwa kodi na kisha ataweka mambo hadharani. Vile vile, amesema (CCM), inapaswa kulipa kodi ya Sh. bilioni sita kwa magari 200 iliyoagiza badala ya bilioni 1.7 kama ilivyotangazwa na Katibu Mkuu wa chama hicho, Yusuf Makamba.

Akizungumza na Nipashe, Dk. Slaa alisema atafuatilia hadi dakika ya mwisho kuhakikisha CCM kinalipa kodi hiyo ili iweze kuwanufaisha Watanzania wengi maskini.

“Sitaki malumbano na mtu yeyote, ninachotaka kuona ni CCM inalipa kodi yote hiyo ili shule, hospitali, barabara na huduma zingine za jamii zipatikane,” alisema Dk. Slaa.

Akiwa mkoani Tanga wakati wa operesheni Sangara iliyoendeshwa katika wilaya zote za mkoa huo pamoja na Wilaya ya Same, mkoani Kilimanjaro, Dk. Slaa alikaririwa na vyombo mbalimbali vya habari akisema kuwa CCM kimeingiza nchini magari 200 kwa ajili ya kampeni za uchaguzi mkuu wa mwakani bila kulipia ushuru wa Sh. milioni 600.

Hata hivyo, anasema kuwa alinukuriwa vibaya na kwamba kiasi sahihi cha kodi inayostahili kulipwa na chama tawala kwa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) ni Sh. bilioni sita.

Alisema kama Makamba alisema walilipa kodi ya bilioni 1.7 alipaswa kuwaeleza waandishi wa habari kiasi cha jumla ya kodi yote ya magari 200 waliyopaswa kuilipa.

Kuhusu kauli ya CCM iliyotolewa na kuwa haitamshitaki kwa kuwa aibu iliyompata mbele ya jamii kwa kusema uongo inatosha, Dk. Slaa alisema hawezi kulumbana na Katibu wa Idara ya Uchumi na Fedha ya Halmashauri kuu ya Taifa (NEC) ya CCM, Amos Makala, kwa kuwa sio saizi yake.

“Aliyeitisha mkutano na kusema maneno hayo ni Makala, sasa mimi si wa kujibishana na mtu kama huyo maana si saizi yangu,” alisema na kuongeza: “Wananchi ndio wataamua nani kapata aibu kati yangu na CCM na kwa taarifa yao nitaendelea kuchunguza ukwepaji wao kodi,” alisema Dk. Slaa, ambaye amekuwa akiibua kashfa mbalimbali za ufisadi dhidi ya Serikali.

Siku chache baada ya Makamba kumjibu Dk. Slaa akisema kuwa chama chake kimeyalipia magari hayo kodi ya Sh. bilioni 1.7 na kutishia kuwa kitamchukulia hatua za kisheria, Makala naye aliitisha mkutano wa waandishi wa habari na kusema kuwa chama hicho tawala hakina tena mpango wa kumshitaki Slaa, kwa kuwa aibu aliyoipata ya kusema uongo kwa jamii inamtosha.

Septemba 15, mwaka 2007 katika Viwanja vya Mwembe Yanga, Temeke, jijini Dar es Salaam Dk. Slaa alitaja majina ya vigogo kadhaa wa serikali na CCM kuwa ni mafisadi kwa kuwa wanahusika katika tuhuma kadha za vitendo vya ufisadi.

Baada ya kutoa tuhuma hizo, baadhi yao walitishia kumfikisha mahakamani lakini hadi leo hakuna hata kigogo mmoja miongoni mwao aliyemshitaki.

Hata hivyo, baadhi yao walikumbwa na kashfa za ufisadi na kulazimishwa kujiuzulu na wengine kufunguliwa mashitaka mahakamani huku baadhi yao wakiendelea kutuhumiwa ingawa hawajachukuliwa hatua za kisheria.


CHANZO: NIPASHE
 
Ndiyo, hiyo ni vita ya wote. Lakini si kwa kuwalenga CCM tu, bali kama wananchi wazalendo tutahakikisha kila anayetakiwa kulipa kodi anafanya hivyo. Na kama sivyo basi tukiwa na taarifa tuwashitaki kwa umma haraka iwezekanavyo. CCM kama chama tawala, wanatakiwa wawe mstari wa mbele kuhakikisha mapato ya nchi yanaongezeka kupitia ukusanyaji wa kodi mbalimbali ikiwemo ilipwayo na chama hicho.
 
Ndiyo, hiyo ni vita ya wote. Lakini si kwa kuwalenga CCM tu, bali kama wananchi wazalendo tutahakikisha kila anayetakiwa kulipa kodi anafanya hivyo. Na kama sivyo basi tukiwa na taarifa tuwashitaki kwa umma haraka iwezekanavyo. CCM kama chama tawala, wanatakiwa wawe mstari wa mbele kuhakikisha mapato ya nchi yanaongezeka kupitia ukusanyaji wa kodi mbalimbali ikiwemo ilipwayo na chama hicho.
Mchimba kisima huingia mwenyewe, Muosha huoshwa
 
Mchimba kisima huingia mwenyewe, Muosha huoshwa
 
Safi sana katika kujua na kuona kuwa kila mtu anafaidi rasilimali za taifa hili maana kuna kila haki ya kujua mali zote na vyanzo vyao
 
Na Joseph Mwendapole
31st December 2009


headline_bullet.jpg
Asema anachunguza kama mali zote zimelipiwa kodi
headline_bullet.jpg
Aahidi kuwa baada ya hapo ataweka wazi kila kitu


Slaa%282%29.jpg

Dk. Wilbroad Slaa


Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Dk. Wilbroad Slaa, amesema kuwa ataendelea kufichua ufisadi unaofanywa na Chama Cha Mapinduzi (CCM).

Dk. Slaa ambaye pia ni Mbunge wa Karatu (Chadema) ameendelea kuwaweka tumbo joto viongozi wa CCM, baada ya kutangaza kuwa ameanza kuchunguza mali zote za chama hicho kama zililipiwa kodi na kisha ataweka mambo hadharani. Vile vile, amesema (CCM), inapaswa kulipa kodi ya Sh. bilioni sita kwa magari 200 iliyoagiza badala ya bilioni 1.7 kama ilivyotangazwa na Katibu Mkuu wa chama hicho, Yusuf Makamba.

Akizungumza na Nipashe, Dk. Slaa alisema atafuatilia hadi dakika ya mwisho kuhakikisha CCM kinalipa kodi hiyo ili iweze kuwanufaisha Watanzania wengi maskini.

“Sitaki malumbano na mtu yeyote, ninachotaka kuona ni CCM inalipa kodi yote hiyo ili shule, hospitali, barabara na huduma zingine za jamii zipatikane,” alisema Dk. Slaa.

Akiwa mkoani Tanga wakati wa operesheni Sangara iliyoendeshwa katika wilaya zote za mkoa huo pamoja na Wilaya ya Same, mkoani Kilimanjaro, Dk. Slaa alikaririwa na vyombo mbalimbali vya habari akisema kuwa CCM kimeingiza nchini magari 200 kwa ajili ya kampeni za uchaguzi mkuu wa mwakani bila kulipia ushuru wa Sh. milioni 600.

Hata hivyo, anasema kuwa alinukuriwa vibaya na kwamba kiasi sahihi cha kodi inayostahili kulipwa na chama tawala kwa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) ni Sh. bilioni sita.

Alisema kama Makamba alisema walilipa kodi ya bilioni 1.7 alipaswa kuwaeleza waandishi wa habari kiasi cha jumla ya kodi yote ya magari 200 waliyopaswa kuilipa.

Kuhusu kauli ya CCM iliyotolewa na kuwa haitamshitaki kwa kuwa aibu iliyompata mbele ya jamii kwa kusema uongo inatosha, Dk. Slaa alisema hawezi kulumbana na Katibu wa Idara ya Uchumi na Fedha ya Halmashauri kuu ya Taifa (NEC) ya CCM, Amos Makala, kwa kuwa sio saizi yake.

“Aliyeitisha mkutano na kusema maneno hayo ni Makala, sasa mimi si wa kujibishana na mtu kama huyo maana si saizi yangu,” alisema na kuongeza: “Wananchi ndio wataamua nani kapata aibu kati yangu na CCM na kwa taarifa yao nitaendelea kuchunguza ukwepaji wao kodi,” alisema Dk. Slaa, ambaye amekuwa akiibua kashfa mbalimbali za ufisadi dhidi ya Serikali.

Siku chache baada ya Makamba kumjibu Dk. Slaa akisema kuwa chama chake kimeyalipia magari hayo kodi ya Sh. bilioni 1.7 na kutishia kuwa kitamchukulia hatua za kisheria, Makala naye aliitisha mkutano wa waandishi wa habari na kusema kuwa chama hicho tawala hakina tena mpango wa kumshitaki Slaa, kwa kuwa aibu aliyoipata ya kusema uongo kwa jamii inamtosha.

Septemba 15, mwaka 2007 katika Viwanja vya Mwembe Yanga, Temeke, jijini Dar es Salaam Dk. Slaa alitaja majina ya vigogo kadhaa wa serikali na CCM kuwa ni mafisadi kwa kuwa wanahusika katika tuhuma kadha za vitendo vya ufisadi.

Baada ya kutoa tuhuma hizo, baadhi yao walitishia kumfikisha mahakamani lakini hadi leo hakuna hata kigogo mmoja miongoni mwao aliyemshitaki.

Hata hivyo, baadhi yao walikumbwa na kashfa za ufisadi na kulazimishwa kujiuzulu na wengine kufunguliwa mashitaka mahakamani huku baadhi yao wakiendelea kutuhumiwa ingawa hawajachukuliwa hatua za kisheria.


CHANZO: NIPASHE

Endelea baba tuko nyuma yako.Waambue mpaka kieleweke
 
I can tell you Dr. Slaa is un-tishable to use Kiswanglish! This has really rattled CCM out it hole!
 
I can tell you Dr. Slaa is un-tishable to use Kiswanglish! This has really rattled CCM out it hole!

Makala bwana na maneno yale . Yaani aka twist oh ni magari 150 , Makamba akasema n magari 200 na ushuru umesha lipwa . Sasa kuonyesha ukweli ni kwamba Makala gawa doc zenye info sahihi za idadi ya magari na kodi iliyo lipwa maana si siri tena . Ili uweze kusema Dr.Slaa kaumbuka .Usikimbilie kusema hakuna mahakama kwa kuwa kaumbuka how ?Mkienda Mahakamani ujue itakuwa moto zaidi docs kibao zitaombwa na ukweli utakuwa kama bahari na kama CCM mnabisha nendeni hata kama Mahakama ni zenu
 
Back
Top Bottom