Uchaguzi 2020 Dkt. Charles Kimei: Changamoto za Wanavunjo zimenisukuma kugombea Ubunge

Uchaguzi 2020 Dkt. Charles Kimei: Changamoto za Wanavunjo zimenisukuma kugombea Ubunge

TAMU YA LEO

Member
Joined
Mar 26, 2020
Posts
8
Reaction score
3
Mwandishi Wetu
Vunjo

Kukosekana kwa elimu shirikishi juu ya wadau wa sekta za kifedha katika jimbo la Vunjo kumepelekea wananchi walio wengi kushindwa kunufail na mikopo hususan inayotolewa na serikali.

Dkt. Charles Kimei ambaye ni mgombea ubunge jimbo la Vunjo (CCM)alisema kazi mojawapo iliyopo mbele yake nikuona namna ya kutoa elimu kwa makundi ya vijana na akina mama ili waweze kujikwamua kiuchumi.

Alisema zipo taasisi mbalimbali za kifedha pamoja na serikali lakini walengwa haswa au wanufaika hawana uelewa wakutosha katika sekta hiyo.

Akizungumza kwenye mkutano wa hadhara kata ya Kirua Vunjo kusini eneo la Uchira alisema kipaumbele ni kuhakikisha wananchi wa Vunjo wananufaika na fursa za kiuchumi pindi zinapojitokeza.

''Kuna mfuko wa Rais,zipo fedha kwa akina mama na vijana na pia wapo wadau mbalimbali wakimaendeleo ni lazima nikaunganishe kwa pamoja ili wanavunjo waweze kunufaika''alisema

Kuhusu masoko nikuwayakiboreshwa yataweza kuvutia watalii kufanya manunuzi katika eneo la Vunjo tofauti na ilivyo sasa kuwa wanaenda jijini Arusha na maeneo mengine hivyo kufanya mzunguko wa fedha kuwa chini.

''Ukiwa na masoko ambayo ni mazuri ni dhahiri kuwa kutakuwa na muingiliano wa watu wengi na hapo ndipo ubunifu wa kibiashara unapoanzia na kuanza kukua kwa kipato''alisema

Dk Kimei alisema baada ya kushinda katika uchaguzi mkuu wa mwezi Oktoba ni lazima atumie elimu yake katika utaalamu wa fedha kuviwezesha vikundi vya vijana,walemavu,na akina mama namna yakuchangamkia fursa za mikopo.

Alisema serikali ya awamu ya tano imetilia mkazo kwa kila halmashauri kutenga asilimia kumi ya mapato yake ya ndani kwa ajili ya mkopo usiokuwa na riba lakini ni watu wachache sana wenye uelewa katika hilo.

Samwel Shao ni mgombea udiwani kata ya Mwika Kaskazini (CCM)ambapo alisema baada ya kuchaguliwa ni lazima aanze na vikundi vya vijana na wanawake ili ahakikishe nao wanafaidi keki ya taifa kama ilivyo kwa maeneo mengine.

Alisema fursa za kujikwamua kiuchumi zipo ila tatizo ni kukosa uwakilishi sahihi wenye kuwa na maono na nia njema ya mafanikio badala yake ni uwepo wa wawakilishi wenye ubinafsi.
Mwisho.
 
Moshi

Mgombea ubunge jimbo la Vunjo kupitia chama cha mapinduzi(CCM)Dkt Charles Kimei amesema hakuwa na mpango wakuingia kwenye ulingo wa siasa ila changamoto zinazowakabili wananchi wake ndizo zilizomsukuma kufanya hivyo.

Dkt Kimei alisema aliyewahi kuwa mbunge wa Vunjo kupitia CCM (2005-2010)marehemu Aloyce Kimaro ndiye alimshawishi kufanya hivyo kwa adhma yakutatua changamoto mbalimbali zilizopo.

Kwa mujibu wa Kimei ni kuwa jimbo la Vunjo lina changamoto mbalimbali na kuwa marehemu Kimaro aliweza kuzitatua kadri ya uwezo wake na alipoachia anao uwezo wa kuendelea kuzipatia ufumbuzi.

Alisema serikali ya awamu ya tano ina nia madhubuti kuleta maendeleo kwa wananchi wake ila tatizo ni pamoja na kuwapata viongozi wasiokuwa sahihi katika utatuzi wa changamoto zilizopo.

''Nimekuja kwa lengo moja kuongeza nguvu katika kutafuta suluhisho la changomoto zilizopo naomba mnitume na nawaahidi sitawaangusha''alisema Dkt Kimei

Kimei alisema changamoto zilizopo hususani maswala ya kiuchumi anao uwezo wa kuzitatua kwa utashi wake kwa ushirikiano na wadau mbalimbali hivyo anasubiria kupewa ridhaa ili kuondoa kiu ya wanavunjo.

Kuhusu miundombinu kwenye masoko alisema hairidhishi na hivyo kupelekea uendeshaji wa biashara kuwa mgumu hususan kipindi cha mvua kwani huwalazimu wafanyabiashara kutumia gharama kubwa kuhamisha bidhaa zao.

''Masoko hayajaezekwa hakuna mazingira rafiki hivyo hata mvua ikinyesha wafanyabiashara wanateseka kuhamisha bidhaa kutoka eneo moja hadi nyingine na hivyo kuongeza gharama za uendeshaji''alisema Dkt Kimei

Samwel Shao ni mgombea udiwani kata ya Mwika Kaskazini (CCM)ambapo alisema baada ya kuchaguliwa ni lazima aanze na vikundi vya vijana na wanawake ili ahakikishe nao wanafaidi keki ya taifa kama ilivyo kwa maeneo mengine.

Alisema fursa za kujikwamua kiuchumi zipo ila tatizo ni kukosa uwakilishi sahihi wenye kuwa na maono na nia njema ya mafanikio badala yake ni uwepo wa wawakilishi wenye ubinafsi.

Mwisho.
 
Huyu ana uchungu wa kweli katika kutatua changamoto za Wanavunjo
 
Mbatia hana hali gani huko vipi komu na selasini waliowahi nccr kuunga juhudi vipi presha huko,wale viti maalumu walioandikiwa barua je
 
Alikuwa wapi? Akashindwa kutoa hiyo elimu? Wampe Kura Mrema
 
Ameshakuwa MBUNGE....

Sasa apige kazi....

Maendeleo hayana vyama
 
Wangempa uwaziri ndo angetatua vizuri
Kwani waziri yuko kutatua tu changamoto za jimboni atokako?!!!

Waziri ana majukumu mengi kuliko mbunge.....

Mbunge ni mtatuzi sahihi na wa ukaribu mno jimboni kwake....
 
Back
Top Bottom