Dkt. Dotto Biteko: Mahitaji ya umeme Nchini Tanzania sio anasa bali ni jambo la lazima

Dkt. Dotto Biteko: Mahitaji ya umeme Nchini Tanzania sio anasa bali ni jambo la lazima

Nyendo

JF-Expert Member
Joined
Jun 4, 2017
Posts
1,336
Reaction score
4,731
Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dkt. Dotto Biteko amesema mahitaji ya umeme Nchini Tanzania sio anasa bali ni jambo la lazima kwasababu kuna uhusiano wa moja kwa moja wa maendeleo ya Wananchi na uwepo wa umeme.

Dkt. Biteko amesema hayo leo May 31,2024 wakati wa uzinduzi wa kituo cha kupokea, kupoza na kusambaza umeme cha Ifakara.

Biteko amesema “Mahitaji ya umeme kwenye Nchi yetu sio anasa ni jambo la lazima kwasababu Wananchi wanao uhusiano wa moja kwa moja wa maendeleo yao na nishati ya umeme, hatuna sababu yoyote ya kuja kwa Wananchi kuwaambia mipango bila kuona matokeo, Wananchi wangetamani kuona mipango inayotafsiriwa kwa thamani ya fedha lakini muhimu zaidi kwa mipango ambayo inatekelezeka”

“Kituo hiki maana yake ni kwamba mwaka jana wastani wa masaa ya umeme kukatika kwenye eneo hili ilikuwa ni masaa manane kwa mwezi, maana yake ukichukua dakika ambazo umeme umekatika utakuta hakuna mgao lakini umekatika ni masaa manane, ninafurahi kusema kwa mwezi huu ambao tunaumaliza matukio ya kukatika umeme ni dk 49 pekee yake kutoka masaa manane na hata hizi dk 49 ni kwenye laini ambazo tulikuwa na matengenezo ya kinga ambazo Wateja walipewa taarifa”
 
..huyu jamaa ndiye aliyesababisha maafa ya Rufiji kwa kulazimisha bwawa lijazwe haraka matokeo yake likazidiwa na maji.
 
Ngoja jua liwake waanze mgao tena, watupe ahadi zingine za kijinga, ccm ishatuona wananchi kama madem zao
 
Back
Top Bottom