Pre GE2025 Dkt. Emmanuel Nchimbi ateuliwa kuwa Katibu Mkuu mpya wa CCM kumrithi Daniel Chongolo

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)
Mama Samia sidhani kama atamkubali huyu Nchimbi, sababu ni nyingi sana, kwa wale CCM wakongwe tunajua, ngoja tuone..!!
Nchimbi ana ndoto za kufika mbali kisiasa.
Bila shaka atakuwa mwenye subira ili afikie malengo yake , kumbuka wanatoka kundi moja miongoni mwa makundi ndani ya CCM.
Wakishindwana wataachana.
 
Hiki cheo naona ni mahsusi kwa watu wa kusini na nyanda za juu kusini,Iringa ikiwa kinara.Hebu angalia orodha hii:-
1.Rashid M Kawawa - Ruvuma
2. Horace Kolimba - Iringa
3. Philip Mangula - Iringa
4. Daniel Chongolo - Iringa
5. John Nchimbi - Ruvuma
Hata dr Lawrence Gama ametokea Ruvuma.
Kwahiyo mkoa wa Ruvuma pekee umetoa makatibu wakuu wa CCM watatu.

Hata hivyo ukanda na ukabila havipo tena, ndiyo maana kanda ya Kaskazini imefanikiwa kutoa PM 4 . Mkoa mmoja wa Arusha kabla haujagawanywa umetoa PM 3. Yote yanawezekana na haijawahi kuwa tatizo kwenye nchi yetu
 
Tatizo kubwa la Nchimbi ni kuamini katika kuumiza washindani wake wa siasa. Mkumbuke wakati akiwa waziri wa mambo ya ndani aliangiza mashekhe waliokamatwa kwa tuhuma za ugaidi kubakwa na kuteswa. Kumbuka mwandishi wa Uhuru alivyotaka kubakwa na watu wa Nchimbi. Kuna visa vingi kama hivi ambavyo ameshiriki kuvifanya kwa miaka yote aliyokuwa UVCCM na serikalini. Ninapata wasiwasi na picha ya uchaguzi wa 2025. Anweza kuwa hatari kuliko Magufuli.
 
Nchimbi alisoma Shule ya Sekondari ya Forest Hill, Mbeya masomo ya kidato cha V na VI mwaka 1991 – 1993. Alijiunga katika Chuo cha IDM Mzumbe (Morogoro) na kuhitimu Stashahada ya Juu ya Utawala (mwaka 1994 – 1997).
Forest Hill Mbeya? ipo sehemu gani kwa miaka hiyo nafahamu advanced ilikuwa Sangu na Meta nadhani na Loleza tu
 
Kwahiyo matokeo ya uchunguzi wa kashfa ya Chongolo yanasemaje? Mbona mnatuacha njia panda?
 
Astaghfirullah, FaizaFoxy kemea haya mambo ya ufirauni.
 
Astaghfirullah, FaizaFoxy kemea haya mambo ya ufirauni.
Siwezi kuhukumu nisiyoyaelewa.

Nashangaa mtu anahukumu mitandaoni na mahakama anazijuwa.

Mpinzani Tanzania alikuwa mmoja tu niliyemkubali, akiona kasoro anakwenda mahakamani watowe jibu. Unamkumbuka?

Zingine hizi zinabaki kuwa "gutter politics" = courtesy; Sitta
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…