Richard
JF-Expert Member
- Oct 23, 2006
- 15,692
- 23,038
Moja kwa moja kwenye mada ambapo leo hii nimekusikia ukitoa tamko kwamba sasa TRA itaja na mfumo bora wa nyaraka wa kukusanya kodi kuanzia Julai 1, 2024.
Tatizo lililopo TRA ni upigaji ambapo maofisa wa TRA hujidamka mapema asubuhi kuwahi kusumbua wafanyabiashara na kugeuza usumbufu huo kuwa ni kero.
TRA haiwezi kukwepa "office automation" ambapo mifumo yake ya kutumia karatasi yabidi kubadilishwa iwe ya kidijitali , jambo linoweza kuisaidia TRA na serikali kuongeza mapato.
Ikiwezekana TRA yaweza kununua software ambazo ni za kisasa zaidi kutoka nje ya nchi ambazo zaweza kubadilisha kabisa mfumo wa kukusanya kodi khasa kwa wafanyabiashara. Kugeuza mifumo ya TRA kuwa ya kidigitali zaidi kutawezesha kuokoa muda, kuondoa makosa madogomadogo yaani errors, kuchanganyua data au data analysis na kuwezesha kupanga mipango sahihi ya kodi.
Huko mbele tuendako mfumo wa kodi ni lazima utakuwa ukizingatia zaidi "Data" ambapo ni lazima wafanyabiashara wote wasajiliwe na wajulikane. Utaratibu wa kuwasajili wafanyabiashara, wajasiliamali na wachuuzi wengine wa kutoka China ni lazima wawe na TIN na watambulike.
Kubadilisha mfumo wa kodi si tu kuhakikisha walipa kodi wafanya hivyo (compliance) lakini pia kwatoa mwanya kuwasaidia maofisa wa TRA kukusanya kodi kwa njia sahihi na za kisasa zaidi na kupata matokeo mazuri na yaso na dosari au twaita accuracy and efficiency gains.
Suala la utitiri wa kodi nalo ni la kuliangalia si tu kuleta kodi mpya kila mtu akiamka asubuhi aja na kodi au tozo. Kwa mfano wachuuzi ambao hawana visimba wawe na kodi yao tofauti na wale wenye visimba sambamba na akina mama ntilie na wauza maji ya matunda, nguo, mitumba na kadhalika.
Wafanya biashara wenye maduka wawe na kodi yao na hawa kuwa hutozwa pia kodi ya majengo au kiwanja au vinginevyo ni lazima wawe na njia sahihi ya kulipa kodi zao. Serikali yaweza kukusanya hizi kodi bila shurti kutoka kwa wafanyabiashara endapo yatumia njia sahihi, bora na zisizowasumbua hawa watu maana wao pia ni binadamu na wastahiki heshima.
TRA ni chombo kikubwa kilichoko nchi nzima na yenye chuo chake cha kodi ambacho hufunza maofisa wa kodi. Hivyo ni lazima TRA waangalie madhara ya kusababisha migomo kama mgomo uliopo sasa wa wafanyabishara. Kwanza mgomo hubababisha upotevu wa mapato kwa wafanyabiashara wenyewe na TRA. Pili migomo hii huatarisha kuwepo na uvunjifu wa amani hivyo busara yahitajika katika kushughulikia matatizo ya wafanyabiashara yanosababiswana TRA.
Mwisho but last, maeneo ya Kariakoo yamejaa sana wafanyabiashara na uwingi wao ni hatari kiafya, kimazingira na kiusalama. Tunao hata ndugu zetu wachina nao ni wachuuzi wa bidhaa hizohizo ambao watanzania nao waziuza maeneo hayo. Maoni yangu ni kwamba hawa wachina mfumo wa kodi uwe wawatoza tofauti na watanzania ili kuwasumbua (discourage) kuwafanya wapunguze kuingiza nchini bidhaa zilozo chini ya viwango na hatari kwa matumizi ya binadamu.
Pia ni jambo la uzuri endapo utafikiria kuanzisha maeneo mapya ya wafanya biashara ambayo yana visimba, umeme, vyoo na mazingira mazuri ambapo wale wafanyabishara wenye uwezo waweze kuhamia kule ili kupunguza msongamano uliopo mitaa ya Kariakoo jambo ambalo litawezesha pia serikali na TRA kupata mapato sahihi kutoka kwa wafanyabiashara hawa.
Hili la kuwatafutia wafanyabiashara wadogo waso na maduka haliwezi kuwa ni tatizo kubwa endapo serikali yatafuta maeneo na kuwasaidia hawa ambao wengi wao ni wahitimu wa hadi vyuo vikuu ambao hawawezi kutoelewa sera ya serikali ya kuwatafutia maeneo maalum.
Mheshimiwa waziri wewe ulikuwa hapa JF ukitoa maoni yako lukuki kuhusu namna ya kurekebisha siasa, uwajibikaji wa serikali na wanasiasa. Naona bado hatujafikia huko na litakuwa ni jambo la kuleta imani kuona unatumia uwezo wako na nafasi yako ukiwa waziri wa uwekezaji kuhakikisha TRA yafanya kazi zake sawa na malengo ya kuundwa kwake.
Tatizo lililopo TRA ni upigaji ambapo maofisa wa TRA hujidamka mapema asubuhi kuwahi kusumbua wafanyabiashara na kugeuza usumbufu huo kuwa ni kero.
TRA haiwezi kukwepa "office automation" ambapo mifumo yake ya kutumia karatasi yabidi kubadilishwa iwe ya kidijitali , jambo linoweza kuisaidia TRA na serikali kuongeza mapato.
Ikiwezekana TRA yaweza kununua software ambazo ni za kisasa zaidi kutoka nje ya nchi ambazo zaweza kubadilisha kabisa mfumo wa kukusanya kodi khasa kwa wafanyabiashara. Kugeuza mifumo ya TRA kuwa ya kidigitali zaidi kutawezesha kuokoa muda, kuondoa makosa madogomadogo yaani errors, kuchanganyua data au data analysis na kuwezesha kupanga mipango sahihi ya kodi.
Huko mbele tuendako mfumo wa kodi ni lazima utakuwa ukizingatia zaidi "Data" ambapo ni lazima wafanyabiashara wote wasajiliwe na wajulikane. Utaratibu wa kuwasajili wafanyabiashara, wajasiliamali na wachuuzi wengine wa kutoka China ni lazima wawe na TIN na watambulike.
Kubadilisha mfumo wa kodi si tu kuhakikisha walipa kodi wafanya hivyo (compliance) lakini pia kwatoa mwanya kuwasaidia maofisa wa TRA kukusanya kodi kwa njia sahihi na za kisasa zaidi na kupata matokeo mazuri na yaso na dosari au twaita accuracy and efficiency gains.
Suala la utitiri wa kodi nalo ni la kuliangalia si tu kuleta kodi mpya kila mtu akiamka asubuhi aja na kodi au tozo. Kwa mfano wachuuzi ambao hawana visimba wawe na kodi yao tofauti na wale wenye visimba sambamba na akina mama ntilie na wauza maji ya matunda, nguo, mitumba na kadhalika.
Wafanya biashara wenye maduka wawe na kodi yao na hawa kuwa hutozwa pia kodi ya majengo au kiwanja au vinginevyo ni lazima wawe na njia sahihi ya kulipa kodi zao. Serikali yaweza kukusanya hizi kodi bila shurti kutoka kwa wafanyabiashara endapo yatumia njia sahihi, bora na zisizowasumbua hawa watu maana wao pia ni binadamu na wastahiki heshima.
TRA ni chombo kikubwa kilichoko nchi nzima na yenye chuo chake cha kodi ambacho hufunza maofisa wa kodi. Hivyo ni lazima TRA waangalie madhara ya kusababisha migomo kama mgomo uliopo sasa wa wafanyabishara. Kwanza mgomo hubababisha upotevu wa mapato kwa wafanyabiashara wenyewe na TRA. Pili migomo hii huatarisha kuwepo na uvunjifu wa amani hivyo busara yahitajika katika kushughulikia matatizo ya wafanyabiashara yanosababiswana TRA.
Mwisho but last, maeneo ya Kariakoo yamejaa sana wafanyabiashara na uwingi wao ni hatari kiafya, kimazingira na kiusalama. Tunao hata ndugu zetu wachina nao ni wachuuzi wa bidhaa hizohizo ambao watanzania nao waziuza maeneo hayo. Maoni yangu ni kwamba hawa wachina mfumo wa kodi uwe wawatoza tofauti na watanzania ili kuwasumbua (discourage) kuwafanya wapunguze kuingiza nchini bidhaa zilozo chini ya viwango na hatari kwa matumizi ya binadamu.
Pia ni jambo la uzuri endapo utafikiria kuanzisha maeneo mapya ya wafanya biashara ambayo yana visimba, umeme, vyoo na mazingira mazuri ambapo wale wafanyabishara wenye uwezo waweze kuhamia kule ili kupunguza msongamano uliopo mitaa ya Kariakoo jambo ambalo litawezesha pia serikali na TRA kupata mapato sahihi kutoka kwa wafanyabiashara hawa.
Hili la kuwatafutia wafanyabiashara wadogo waso na maduka haliwezi kuwa ni tatizo kubwa endapo serikali yatafuta maeneo na kuwasaidia hawa ambao wengi wao ni wahitimu wa hadi vyuo vikuu ambao hawawezi kutoelewa sera ya serikali ya kuwatafutia maeneo maalum.
Mheshimiwa waziri wewe ulikuwa hapa JF ukitoa maoni yako lukuki kuhusu namna ya kurekebisha siasa, uwajibikaji wa serikali na wanasiasa. Naona bado hatujafikia huko na litakuwa ni jambo la kuleta imani kuona unatumia uwezo wako na nafasi yako ukiwa waziri wa uwekezaji kuhakikisha TRA yafanya kazi zake sawa na malengo ya kuundwa kwake.