Dkt. Magufuli asema Serikali imejipanga kulifanya eneo la Kanda ya Ziwa kuwa eneo la utalii mkubwa na aeleza kuwa utalii utainua hiyo Kanda kiuchumi

mbuga za kulazimisha hazidumu anawivu na kaskazini,jamaa hawapendi wachaga na wameru,hizo mbuga zake zitanyauka tu
 
mbuga za kulazimisha hazidumu anawivu na kaskazini,jamaa hawapendi wachaga na wameru,hizo mbuga zake zitanyauka tu
Acha Ukabila wewe...kwani wachaga na wameru wana mbuga gani za Wamyama hadi ionekane kua ana wivu na Kaskazini? Alivyoigawa Selous Game reserve kua National Park mbona hamkusema kua ana wivu na kwamba itakufa? Pathetic
 
Ina uwanja wa ndege za watalii ndani ya mbuga ,Serengeti pia wana uwanja ndani ya mbuga

kanda ya ziwa hizo mbuga tatu zinakuwa served na uwanja mmoja sababu haziko mbali mbali sana.Chato ndiko kunakuwa jirani kwao wote

..inatakiwa utengenezwe utalii ambao ni UNIQUE kwa kanda ya ziwa.

..kama anataka kuanzisha mbuga za wanyama basi utalii wa huko unatakiwa uwe ktk MSIMU tofauti na mbuga za kaskazini, na mbuga za kusini.

..ukiwa na vivutio ambavyo ni unique kwa kanda ya ziwa maana yake utaweza kupata watalii toka kanda nyingine ambazo tayari ni established kama kaskazini.

..kwa mfano, Zanzibar ni unique, hivyo mtalii akitembelea Serengeti au Ngorongoro anaweza kwenda na Zanzibar. Lakini siyo rahisi kwa mtalii kutembelea Serengeti halafu aende na Mikumi.

..Utalii wa kanda ya ziwa ukiwa ktk msimu tofauti na kanda nyingine wanaweza kufaidika na watalii ambao wanataka kuona vivutio lakini wamekosa nafasi ya kwenda kanda ya kaskazini, kusini, etc hivyo wanatafuta eneo mbadala.

..Na tukiwa na misumu zaidi ya mmoja ya utalii nchini maana yake tutakuwa tunapokea watalii year around na hiyo itasaidia sana ktk mapato ya makampuni ya utalii.
 
Acha Ukabila wewe...kwani wachaga na wameru wana mbuga gani za Wamyama hadi ionekane kua ana wivu na Kaskazini? Alivyoigawa Selous Game reserve kua National Park mbona hamkusema kua ana wivu na kwamba itakufa? Pathetic
Wivu unamsumbua
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…