Dkt. Mpango na Masauni mmekosea kunyooshea vidole baadhi ya makanisa au imani

Dkt. Mpango na Masauni mmekosea kunyooshea vidole baadhi ya makanisa au imani

Yoda

JF-Expert Member
Joined
Jul 22, 2018
Posts
48,475
Reaction score
70,102
Wiki hii makamu wa Rais na waziri wa mambo ya ndani wakiwa katika shughuli tofauti za kidini wakiwa jukwaani walizungumza mambo ambayo kwa hakika ni kuingilia uhuru wa imani za watu wengine.

Makamu wa Rais aliwanyooshea vidole viongozi wanaojilimbikizia mali pamoja na kuwaaminisha wafuasi wao kwamba wanaweza kupata maendeleo kwa miujiza, Masauni yeye katika shughuli ya makambi ya kanisa la Wasabato alikuwa anaelekeza viongozi wa dini kuhakikisha wanafuata na kuzingatia mafundisho ya kitabu cha dini ili wasije kuingia katika matatizo na serikali na akafikia hadi hatua ya kutolea mfano yaliyomkuta nabii kiboko ya wachawi.

Viongozi hawa hawako sahihi kunyooshea vidole au kutoa maangalizo dhidi ya imani au dini yote hasa inapokuwa tofauti na yao, huku ni kuingilia uhuru wa kidini au imani za wengine.

Makamu wa Rais au waziri wa mambo ya ndani hawajui imani ipi hasa ni sahihi na ya kweli isiyo na upotofu. Wao kama viongozi wanapaswa kuwa neutral ili mradi katiba na serikali vimeruhusu dini na imani zozote kufanya mambo yao kwa uhuru bila kuvunja sheria.

- Waziri Masauni asema anachofanya “Kiboko ya Wachawi” anathibitisha kuwa alikuwa anafanya utapeli
 
Makanisa ambayo si taasisi yanapaswa futwa
 
Kiboko ya wachawi alikuwa anawatapeli waTZ, serikali imefanya jambo jema sana kumfukuza.

Nimemsikiliza vizuri masauni amesisitiza taasisi za dini zifuate mafundisho kama ya dini yanavyosema kwenye vitabu na si kutapeli watu kama alivyokuwa anafanya kiboko ya wachawi.
 
Kiboko ya wachawi alikuwa anawatapeli waTZ ,serikali imefanya jambo jema sana kumfukuza.

Nimemsikiliza vizuri masauni amesisitiza taasisi za dini zifuate mafundisho kama ya dini yanavyosema kwenye vitabu na si kutapeli watu kama alivyokuwa anafanya kiboko ya wachawi.
Mbona Mwamposa hadhibitiwi na serikali??
 
Wakristo walio wengi hapa bongo akili zao sijui zimepatwa na nini[sio wote] yani mchungaji hata akimwambia yesu kanituma uje ulale na mimi anakubali,,, uzuri wa sadaka za waislam wanapelekewa walengwa moja kwa moja sio anapewa shekhe,, kama ni wagonjwa basi watu wanajikusanya mpaka hospital kila muumini anatoa alichonacho kwa mgonjwa moja kwa moja,, jifunzeni basi Wakristo kwa waislam hata haya na hayo mabaya yao waachieni wenyewe.. msikiti wa manyema kuna upotevu wa pesa kwenye account ya msikiti na kimenuka mbaya mpaka watu wametolewa uongozi, tena basi hiyo pesa yenyewe iliyopotea ni sawa na sadaka ya siku moja kwa kiboko ya wachawi,, lkn mbungi lake si mchezo
 
Back
Top Bottom