Dkt. Mpango: Wahubiri wa dini wanajilimbikizia mali

Dkt. Mpango: Wahubiri wa dini wanajilimbikizia mali

Suley2019

JF-Expert Member
Joined
Oct 7, 2019
Posts
2,203
Reaction score
5,610
1725731103455.png

Makamu wa Raisi Dkt. Philip Mipango

Makamu wa Raisi Dkt. Philip Mipango akimwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan katika kilele cha Maadhimisho ya Jubilei ya Miaka 50 ya Kanisa la New Life Outreach iliyofanyika katika kanisa hilo Sakina mkoani Arusha amegusia suala la Wahubiri wa dini kujilimbikizia mali. Akieleza kuhusu jambo hilo Dkt. Mpango amesema:

“Hivi sasa yameibuka mafundisho ya viongozi wa dini yanayowaaminisha wafuasi wao kutegemea miujiza Zaidi ili kupata maendeleo badala ya kufanya kazi kwa bidii na maarifa. Viongozi hao wanawaelekeza waamini wao kwenda kwenye nyumba zao za ibada ili wakaombewe wapate mali ikiwemo magari, nyumba, pesa wanazo zitamani, lakini pia wanaomba kutatuliwa shida zao tunashuhudia kuongezeka kwa wahubiri wanaojilimbikizia fedha na mali binafsi kutokana na sadaka na mauzo ya vitu mbalimbali vya hao watu wanyonge.
Wengi wa wahanga wa mahubiri ya aina hiyo ni wananchi wanyonge wanaokabiliwa na shida au matatizo mbalimbali ya maisha yakiwemo magonjwa, umasikini migogoro katika ndoa, ugumba kukosa ajira na kadhalika”
PIA SOMA
- Kwanini Serikali kupitia Wizara ya Nje, wasishirikiane na Wizara ya Nje ya Congo, kumkamata Tapeli alojiita Nabii kiboko ya wachawi?

- Nimeacha kutoa sadaka baada ya kusikia kauli hii ya mchungaji
 
MUNGU awasaidie hawa wachungaji wengi wao hata YESU KRISTO hawampendi
 
View attachment 3089684
Makamu wa Raisi Dkt. Philip Mipango

Makamu wa Raisi Dkt. Philip Mipango akimwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan katika kilele cha Maadhimisho ya Jubilei ya Miaka 50 ya Kanisa la New Life Outreach iliyofanyika katika kanisa hilo Sakina mkoani Arusha amegusia suala la Wahubiri wa dini kujilimbikizia mali. Akieleza kuhusu jambo hilo Dkt. Mpango amesema:

“Hivi sasa yameibuka mafundisho ya viongozi wa dini yanayowaaminisha wafuasi wao kutegemea miujiza Zaidi ili kupata maendeleo badala ya kufanya kazi kwa bidii na maarifa. Viongozi hao wanawaelekeza waamini wao kwenda kwenye nyumba zao za ibada ili wakaombewe wapate mali ikiwemo magari, nyumba, pesa wanazo zitamani, lakini pia wanaomba kutatuliwa shida zao tunashuhudia kuongezeka kwa wahubiri wanaojilimbikizia fedha na mali binafsi kutokana na sadaka na mauzo ya vitu mbalimbali vya hao watu wanyonge.
Wengi wa wahanga wa mahubiri ya aina hiyo ni wananchi wanyonge wanaokabiliwa na shida au matatizo mbalimbali ya maisha yakiwemo magonjwa, umasikini migogoro katika ndoa, ugumba kukosa ajira na kadhalika”
Ni kweli asemacho, lakini yeye pamoja na makada wenzake wa ccm ndio wanaoongoza kwa kujilimbikizia mali za wizi kupitia fedha za umma. In short hana usafi wa kunyooshea yoyote kidole.
 
Anayejiita tingatinga ametia petroli kwenye shimo, siafu wote wanakuja juu.
 
wananchi wanyonge wanaokabiliwa na shida au matatizo mbalimbali ya maisha yakiwemo magonjwa, umasikini
Hayo ni matatizoo yaliyoletwa na CCM na ndio yamefanya hao watumishi wapate mianya yakuwaburuza hao unaosema wanyongeee..
 
Uislam ulikwishalizungumza hili miaka mingi iliyopita!


يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا إِنَّ كَثِيرًا مِّنَ الْأَحْبَارِ وَالرُّهْبَانِ لَيَأْكُلُونَ أَمْوَالَ النَّاسِ بِالْبَاطِلِ وَيَصُدُّونَ عَن سَبِيلِ اللَّـهِ ۗ وَالَّذِينَ يَكْنِزُونَ الذَّهَبَ وَالْفِضَّةَ وَلَا يُنفِقُونَهَا فِي سَبِيلِ اللَّـهِ فَبَشِّرْهُم بِعَذَابٍ أَلِيمٍ﴿٣٤﴾

Enyi mlioamini! Hakika wengi katika Ahbaar (Mafuqahaa weledi wa Kiyahudi) na Ruhbaan (Monaki wa Kikristo) wanakula mali za watu kwa batili, na wanazuia Njia ya Allaah. Na wale wanaorundika dhahabu na fedha na wala hawazitoi katika Njia ya Allaah, basi wabashirie adhabu iumizayo.
-[Surat Tawba(9:34)]
 
Hasa yule aliyejiita KIBOKO !! Alikuwa mpigaji kibao !!
Sasa VP kwanini usiwataje na kuwanyanganya leseni badala ya kubwabwajika tu
 
Back
Top Bottom