Pre GE2025 Dkt. Mwinyi kawapa walimu posho ya usafiri kule Zanzibar. Rais Samia naye awafikirie

Pre GE2025 Dkt. Mwinyi kawapa walimu posho ya usafiri kule Zanzibar. Rais Samia naye awafikirie

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)

NAMBA MOJA AJAYE NCHINI

JF-Expert Member
Joined
Oct 29, 2019
Posts
9,863
Reaction score
20,806
Walimu wamekua waaminifu Kwa serikali awamu zote,kila mwaka impact yake inaonekana Kwa matokeo mazuri yanayowabeba wanasiasa majukwaani kisiasa hasa Rais na waziri wa elim,Motisha ya kuwapeleka Dubai ni kebehi na dhihaka Kwa mwalimu kwasababu Haina tija kwa mwalim Wala motisha kwake.

Dkt. Mwinyi kaweka posho ya nauli kwa kila mwalimu Zanzibar huku bara Rais wetu unasubiri nini?

Motisha zisizo na impact Kwa maisha ya mwalimu ni dhihaka na kebehi kwao!Familia ya mwalim inafaidika na nini Kwa trip za Dubai !!?posho ingekua na mantiki kuliko kituko Cha safari za Dubai!!

Hizo safari zinawafaa nyie wanasiasa wenye fedha za ziada na posho sio mwalimu ambae mshahara wake hauungi mwezi,ifike hatua wanasiasa wakemewe kutoa dhihaka Kwa walimu,taifa Bado linawategemea wao zaidi!

Rc homera akemewe hadharani ,safari za Dubai Kwa mwalimu ni dhihaka na hazina tija kwa mwalimu na familia yake!

Kama lengo ni uchaguzi was mwaka huu wasitumie majukwaa kuwakashifu walimu ambao ndio nguzo ya taifa hili!!!

Nampongeza Dr. Mwinyi Kwa kujali maslahi Yao kuliko drama zilizopo Huku Bara!

Mungu wabariki walimu na jamhuri yetu.
 
Back
Top Bottom