Pre GE2025 Dkt. Nchimbi: CCM inanadi sera zake sio matusi

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)

Waufukweni

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2024
Posts
2,060
Reaction score
5,648
Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) ambaye pia ni Mgombea Mwenza wa kiti cha Urais Tanzania Bara Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi, amesema CCM Haifanyi siasa za matusi kwani ni Chama cha Mfano katika kuhakikisha kinaheshimu utu wa watu na kufanya kazi kwa kufuata misingi yake.

Soma: Dkt. Emmanuel Nchimbi: CCM tunafanya siasa za ustaarabu na maendeleo

Balozi Dkt. Nchimbi ametoa kauli hiyo Jijini Dodoma wakati wa ufunguzi kikao cha kamati ya utekelezaji wa Jumuiya ya Umoja wa Wazazi (CCM).

Amesema CCM inaendelea kujipanga kwaajili ya kufanya vizuri kwenye uchaguzi kwa kunadi sera zake kwani kuna mambo mengi mazuri yaliyofanyika ambayo wananchi wanapaswa kuelezwa.
Your browser is not able to display this video.
 
..Dr.Mchimbi hana mvuto kabisa.

..kuvutia watu wamsikilize itabidi atumie sana wasanii.
 
Kwa hilo linajulikana mchana kweupe mbuzi anakula majani!
 
 

Attachments

  • 1edaac7a3e34dc7dbc36bb899a6e6430_1738702701936.mp4
    5.4 MB
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…