Stephano Mgendanyi
JF-Expert Member
- May 16, 2020
- 2,833
- 1,301
Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo na Mbunge wa Jimbo la Songea Mjini Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro amewataka vijana wa Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi (UVCCM) wa Manispaa ya Songea Mjini wawe waadilifu katika utekelezaji wa majukumu ya Chama na maelekezo ya viongozi ili kukiendeleza Chama hicho .
Mhe. Ndumbaro amesema hayo leo Julai 8, 2024 mkoani Ruvuma wakati wa mkutano wa Baraza la Umoja wa Vijana hao ambapo amewataka kuimarisha umoja huo kwa kuongeza idadi ya wanachama.
“Kuweni waadilifu ili kujitengenezea nafasi nzuri za kuaminiwa na chama na Serikali pia epukeni sana kutumiwa na watu kwa maslahi binafsi mnapaswa kukitumikia chama na jumuiya na si vinginevyo” amesema Mhe. Ndumbaro
Mhe. Ndumbaro ametumia fursa hiyo kuwakumbusha vijana hao wajibu wao kuelekea uchaguzi wa Serikali za mitaa ili kuhakikisha chama cha mapinduzi kinashinda katika mitaa yote 95 ya Manispaa ya Songea Mjini.
Mhe. Ndumbaro amesema hayo leo Julai 8, 2024 mkoani Ruvuma wakati wa mkutano wa Baraza la Umoja wa Vijana hao ambapo amewataka kuimarisha umoja huo kwa kuongeza idadi ya wanachama.
“Kuweni waadilifu ili kujitengenezea nafasi nzuri za kuaminiwa na chama na Serikali pia epukeni sana kutumiwa na watu kwa maslahi binafsi mnapaswa kukitumikia chama na jumuiya na si vinginevyo” amesema Mhe. Ndumbaro
Mhe. Ndumbaro ametumia fursa hiyo kuwakumbusha vijana hao wajibu wao kuelekea uchaguzi wa Serikali za mitaa ili kuhakikisha chama cha mapinduzi kinashinda katika mitaa yote 95 ya Manispaa ya Songea Mjini.