Dkt. Salim Ahmed Salim ni nani?

Dkt. Salim Ahmed Salim ni nani?

Adilinanduguze2

JF-Expert Member
Joined
Mar 11, 2014
Posts
1,386
Reaction score
1,919
DR. SALIM AHMED SALIM NI MTU WA AINA GANI?

Heri ya mwaka mpya wadau wa Uwanja wa Diplomasia.

Poleni kwa kimya kirefu.

Leo tunawaletea maelezo kuhusu mwanadiplomasia nguli wa Tanzania ambaye ni kiigizo (Role model) cha ndugu yetu Abbas Mwalimu,huyu si mwingine bali ni Dr. Salim Ahmed Salim.

Mara baada ya kuundwa kwa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania hapo mwaka 1964, Mambo ya Nje ni moja ya mambo yaliyokubalianwa kuwa yawe ya Muungano, hivyo nafasi kama za Ubalozi katika Nchi mbalimbali Washirika na Taasisi za Kimataifa ilibidi zigawanywe kati ya Watanganyika na Wazanzibari ili dhana ya Utanzania ipate kuonekana dhahiri.

Ni katika wakati husika ndipo Rais Julius Nyerere, Kama Mkuu wa Nchi na mtu mwenye Mamlaka ya Uteuzi wa Mabalaozi alipoomba majina ya wale ambao walionekana kuwa na sifa za kuteuliwa kuwa Mabalozi kutoka Zanzibar kwa Rais Abeid Amani Karume.

Miongoni mwa majina yaliyoletwa na Sheikh Karume kwa Mwalimu Nyerere ni jina la Kijana mdogo wa miaka 22 Salim Ahmed Salim, jambo ambalo lilimfanya Mwalimu Nyerere amuulize mara ya pili Rais Karume juu ya umri wa Kijana huyo, majibu aliyopewa ni kuwa huyo ni Kijana wa Zanzibar mwenye vigezo na uwezo, apewe nafasi.

Bila hiyana, Mwalimu Nyerere akamteua Kijana huyo Salim Ahmed Salim kuwa Balozi wa Tanzania katika Jamhuri ya Uarabu ya Misri, nafasi ambayo aliitumikia kwa muda wa Mwaka mmoja kati ya Mwaka 1964 na 1965 kabla ya kuteuliwa kuwa Balozi wa Tanzania Nchini India.

Unaweza kudhani kuwa Salim Ahmed Salim alipewa nafasi husika kwa upendeleo, au kwa kuwa Chama chake cha Ummah Party kilikuwa na mahusiano ya karibu na Chama cha ASP cha Karume.

Uwezo wa Dkt Salim Ahmed Salim katika kuieneza Diplomasia ya Tanzania kwa muda wa miaka 50 ya Muungano wetu unaonyesha dhana ya upendeleo isivyo na mashiko, lakini hata uzoefu na Ukindakindaki wake wakati akiteuliwa kushika nafasi hiyo pamoja na kuwa alikuwa na umri mdogo vinaonyesha kuwa aliistahili nafasi hiyo.

Dr. Salim hakuwa mgeni wa Siasa za Zanzibar, alichipukia katika Chama cha Zanzibar Nationalist Party, ZNP chini ya ulezi wa Komredi mahiri, Profesa Abdulrahman Mohammed Babu na bega kwa bega naye alishiriki katika kukiasisi Chama cha Kwanza chenye kufuata Mrengo wa Kijamaa katika Afrika, Chama cha Ummah Party, Chama ambacho kilishirikiana na Chama cha ASP katika kutekeleza Mapinduzi ya Zanzibar ya mwaka 1964 yaliyomuingiza madarakani Karume.

Ni Chama hiki cha Ummah Party ndicho kilichotoa wanamapinduzi Majemedari kama Komredi Ali Sultan Issa, Kanali Ali Mahfoudh, Komredi Sharifu Ahmed Badawyi Qullatein na wengineo ambao walikuwa chachu ya Mapinduzi ya Zanzibar. Kijana mdogo Salim Ahmed Salim alishirikiana na kulelewa na wote hao, jambo lililompa uzoefu, uwezo na mafunzo.

Mpaka leo rekodi zinamuonyesha Dkt Salim A Salim aliyezaliwa Januari 23, 1942 kuwa ndiye Mtanzania mwenye umri mdogo zaidi kuteuliwa kuwa Balozi wa Tanzania nje ya Nchi.

Dr. Salim Ahmed Salim hakuishia kuwa Balozi wa Tanzania nchini Misri tu bali alihudumu katika nchi nyingine kama vile India na China.

Pia alihudumu kama Mwakilishi wa kudumu wa Tanzania katika Umoja wa Mataifa kuanzia mwaka 1970.

Mwaka 1976 alihudumu kama Rais wa Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa kwa kingereza United Nations Security Council (UNSC) na mwaka 1979 kama Rais wa Kikao cha 34 cha Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa (Thirty-Fourth Session of the United Nations General Assembly) UNGA.

Alirejea Tanzania na kuhudumu kama Waziri Mkuu na Naibu Waziri Mkuu kati ya miaka ya 1984 na 1989.

Dr. Salim Ahmed Salim pia alihudumu kama Katibu Mkuu wa iliyokuwa Jumuiya ya Muungano wa Afrika kwa kingereza Organisation of African Unity (OAU) sasa Umoja wa Afrika (AU) kutoka mwaka 1989 mpaka 2001.

Dr Salim Ahmed Salim alihusika kimamilifu katika mabadiliko ya taasisi hii muhimu kwa Afrika kutoka OAU kwenda AU.

Akiwa Mwenyekiti wa Kamati Maalumu ya Umoja wa Mataifa ya kuondoa Ukoloni yaani United Nations Special Committee on Decolonisation (UNSCD) Dr Salim Ahmed Salim alisaidia kuweka misingi mipya ya kupatikana kwa kipindi kingine cha Uhuru wa Bara zima la Afrika.

Akiwa kiongozi wa mapambano dhidi ya ubaguzi wa rangi alihudumu kama Mwenyekiti wa Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa liliweka vikwazo dhidi ya Rhodesia kwa kingereza Chairman of the United Nations Security Council Commission on Sanctions against Rhodesia (Sasa Zimbabwe).

Pia alihudumu kama Rais wa Mkutano Mkuu wa Kimataifa ulioiwekea vikwazo nchi ya Afrika ya Kusini kwa kingereza the President of the International Conference on Sanctions against South Africa na pia kama Rais wa Mkutano wa Kimataifa wa Paris uliojadili ubaguzi wa rangi yaani President of the Paris International Conference on Apartheid.

Kwa kutambua mchango wake katika bara la Afrika, Dr. Salim Ahmed Salim alitunukiwa tuzo mbalimbali kutoka katika nchi za Togo, Rwanda na Liberia.

Kwa sasa Dr. Salim Ahmed Salim ni Mwenyekiti wa Taasisi ya Mo Ibrahim Foundation ambayo hutoa Tuzo kwa viongozi bora barani Afrika.

Uwanja wa Diplomasia.

Maelezo haya ni kwa hisani ya Mzee Mohamed Said na tovuti ya Mo Ibrahim Foundation.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Naupenda sana utulivu wake...kamwe huwezi mlinganisha na vijana wa sasa.

Vijana wa Sasa kama Wewe , Polepole(japo haeleweki ni kijana au mzee) , Bashite, Ali Happy.
 
Biography of Dr. Salim Ahmed Salim

Dr. Salim Ahmed Salim, who concluded his term of office as Secretary General of the Organization of African Unity on 17 September 2001 after serving an unprecedented three terms covering a period of twelve years, is now involved in several activities. He has functions and responsibilities at national, continental and international levels.
At the national (Tanzania) level he is serving as the Chairman of the Board of Trustees of The Mwalimu Nyerere Foundation. He is also the Chancellor of the Hubert Kairuki Memorial University.
At the continental level, following the invitation of the President of the African Development Bank, he has since March, 2002 been acting as African Water Ambassador whose responsibilities include advocacy, sensitization, and mobilization of support on African water issues. He also serves as:

Chairperson, Advisory Board, Institute of Security Studies (ISS) based in Pretoria, South Africa.

Chairperson of the International Board of Trustees, Africa Humanitarian Action (AHI) based in Addis Ababa, Ethiopia.

Member and Chairperson of the Advisory Board of Trustees of the Institute of Peace, Leadership and Governance, Africa University, Mutare, Zimbabwe.

At international level, Dr. Salim serves in the following Boards, Panels/Commission

Co-chair, Eminent Persons Group (EPG) on Small Arms and Light Weapons (Secretariat, based in Washington DC);

Member of the Board of the South Centre (Secretariat based in Geneva);

Member, Policy Advisory Commission, World Intellectual Property Organization (WIPO);

Member of the Foundation Council, Centre of Humanitarian Dialogue based in Geneva.

Previous Experience and Positions Held:
Dr. Salim Ahmed Salim was elected Secretary-General of the OAU on 27 July 1989. He formally took over on 19 September 1989. Prior to his election, Dr. Salim held public office in his country, the United Republic of Tanzania, where he served in various capacities for 27 years. He was Prime Minister from 1984 to 1985 and then served as Deputy Prime Minister and Minister of Defense and National Service from 1985 until his election to the helm of the OAU General Secretariat.
Dr. Salim also held other key positions in the Government of the United Republic of Tanzania. He served for many years in the Tanzanian diplomatic service which he also steered as Minister for Foreign Affairs for four years from 1980 to 1984. His rise to the top of Tanzania’s Foreign Service was preceded by many years of grounding in international diplomacy as Ambassador. He served as Ambassador to the Arab Republic of Egypt (1964-1965), High Commissioner (i.e. Ambassador) to India (1965-1968). He was, for one year, the Director of Africa and Middle East Division in the Ministry of Foreign Affairs in Dar-es-Salaam before his posting as Ambassador to the People’s Republic of China in 1969. In 1970, he was appointed Tanzania’s Permanent Representative to the United Nations in New York, where he remained for more than ten years. During his period at the United Nations, Dr. Salim was concurrently accredited as Ambassador to Cuba, High Commissioner to Guyana, Barbados, Jamaica and Trinidad and Tobago.
During his service at the United Nations, Dr. Salim was elected as President of the United Nations Security Council in January 1976 and went on to serve as President of the Thirty-Fourth Session of the United Nations General Assembly in September 1979. During his one year tenure of office, he also presided over the Sixth and Seventh Emergency Special Sessions of the United Nations General Assembly in January and July 1980 respectively. In September 1980, he equally presided over the Eleventh Special Session of the United Nations General Assembly.
Dr. Salim was Chairman of the United Nations Security Council Committee on Sanctions Against Rhodesia from January to December 1975, President of the International Conference on Sanctions against South Africa in 1981 as well as the Paris International Conference Against Apartheid in 1984. Between 1972 and 1980, he chaired the United Nations Special Committee on Decolonization (Committee of 24). During this period under his chairmainship, the Committee played a key role in steering many colonies and non-self governing territories to full sovereignty and independence. Dr. Salim also served on the Palme Independent Commission on International Security Issues and the Independent Commission on International Humanitarian Issues.
Dr. Salim has attended and/or chaired numerous Summits, International Conferences, Seminars, Workshops and Colloquia under the auspices of the United Nations, the Organization of African Unity, the Non-Aligned Movement and others throughout the world.
Educational Qualifications and Honorary Degrees:
Dr. Salim undertook studies at the University of Delhi, India (1965-1968) and proceeded to obtain a Masters Degree in International Affairs in January 1975 at Columbia University in New York. He holds six Doctorates (Honoris Causa) including: Doctor of Laws, the University of Philippines at Los Baños (1980), Doctor of Humanities, University of Maiduguri, Nigeria (1983), Doctor of Civil Law, University of Mauritius (1991), Doctor of Arts in International Affairs, University of Khartoum, Sudan (1995), Doctor of Philosophy in International Relations, University of Bologna, Italy (1996), and Doctor of Laws, University of Cape Town, South Africa (1998).
Honours and Decorations:
Dr. Salim holds a number of decorations/honours (including some of the highest national honours). Among them are the Star of Africa (Liberia, 1980), the Order of the United Republic of Tanzania – Nishani Ya Jamhuri Ya Muungano Wa Tanzania, 1985), Order of Mille Collines (Rwanda, 1993), Grande Croix de l’Ordre Congolais du Dévouement (Republic of Congo, 1994), Grand Officier de l’Ordre du Mérite (Central African Republic, 1994), Medal of Africa (Libya, 9.9.99), Grand Officier de l’Ordre National du Lion (Sénégal, 2000), Order of the Two Niles (Sudan, 2001), Ordre El-Athir (Algeria, 2001), Ordre du Mono (Togo, 2001), Commandant de l’Ordre National (Mali, 2001).
Born in Zanzibar on 23 January 1942, Dr. Salim Ahmed Salim is married to Amne. They have three children: Maryam, Ali and Ahmed.
Dar-es-Salaam
April 2002


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mzee salimu juzi alikuwa amelazwa baada ya kufanyiwa upasuaji. Mh. Rais alikwenda kumjulia hali sijui anaendeleaje maskini mwanadiplomasia wetu nguli kipenzi cha Mwalimu amrithi Mwinyi urais. Alimkatalia kuwa ni zamu ya bara . Mwalimu alisononeka sana akaangukia chaguo LA Pili mzee Mkapa . Baada ya Mkapa Boys to Men JK na EL. wakampakazia Mara ooh sio mtanzania, kaka yake ni brigedia Wa jeshi LA Oman na siasa taka nyingi eti alishiriki kumuua Karume. Ustaarabu Wa yule Salim is unequalled katika arena ya siasa za Tanzania .MWENYEZI MUNGU amponye haraka . kama angekuwa rais historia ya nchi ingesomeka tofauti na Leo. Tupewe update ya maendeleo ya Afya yake kiongozi mpendwa wetu.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ahsante sana kwa historia na tunamwomba Mungu amuafu
Nalog off
 
DR. SALIM AHMED SALIM NI MTU WA AINA GANI?

Heri ya mwaka mpya wadau wa Uwanja wa Diplomasia.

Poleni kwa kimya kirefu.

Leo tunawaletea maelezo kuhusu mwanadiplomasia nguli wa Tanzania ambaye ni kiigizo (Role model) cha ndugu yetu Abbas Mwalimu,huyu si mwingine bali ni Dr. Salim Ahmed Salim.

Mara baada ya kuundwa kwa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania hapo mwaka 1964, Mambo ya Nje ni moja ya mambo yaliyokubalianwa kuwa yawe ya Muungano, hivyo nafasi kama za Ubalozi katika Nchi mbalimbali Washirika na Taasisi za Kimataifa ilibidi zigawanywe kati ya Watanganyika na Wazanzibari ili dhana ya Utanzania ipate kuonekana dhahiri.

Ni katika wakati husika ndipo Rais Julius Nyerere, Kama Mkuu wa Nchi na mtu mwenye Mamlaka ya Uteuzi wa Mabalaozi alipoomba majina ya wale ambao walionekana kuwa na sifa za kuteuliwa kuwa Mabalozi kutoka Zanzibar kwa Rais Abeid Amani Karume.

Miongoni mwa majina yaliyoletwa na Sheikh Karume kwa Mwalimu Nyerere ni jina la Kijana mdogo wa miaka 22 Salim Ahmed Salim, jambo ambalo lilimfanya Mwalimu Nyerere amuulize mara ya pili Rais Karume juu ya umri wa Kijana huyo, majibu aliyopewa ni kuwa huyo ni Kijana wa Zanzibar mwenye vigezo na uwezo, apewe nafasi.

Bila hiyana, Mwalimu Nyerere akamteua Kijana huyo Salim Ahmed Salim kuwa Balozi wa Tanzania katika Jamhuri ya Uarabu ya Misri, nafasi ambayo aliitumikia kwa muda wa Mwaka mmoja kati ya Mwaka 1964 na 1965 kabla ya kuteuliwa kuwa Balozi wa Tanzania Nchini India.

Unaweza kudhani kuwa Salim Ahmed Salim alipewa nafasi husika kwa upendeleo, au kwa kuwa Chama chake cha Ummah Party kilikuwa na mahusiano ya karibu na Chama cha ASP cha Karume.

Uwezo wa Dkt Salim Ahmed Salim katika kuieneza Diplomasia ya Tanzania kwa muda wa miaka 50 ya Muungano wetu unaonyesha dhana ya upendeleo isivyo na mashiko, lakini hata uzoefu na Ukindakindaki wake wakati akiteuliwa kushika nafasi hiyo pamoja na kuwa alikuwa na umri mdogo vinaonyesha kuwa aliistahili nafasi hiyo.

Dr. Salim hakuwa mgeni wa Siasa za Zanzibar, alichipukia katika Chama cha Zanzibar Nationalist Party, ZNP chini ya ulezi wa Komredi mahiri, Profesa Abdulrahman Mohammed Babu na bega kwa bega naye alishiriki katika kukiasisi Chama cha Kwanza chenye kufuata Mrengo wa Kijamaa katika Afrika, Chama cha Ummah Party, Chama ambacho kilishirikiana na Chama cha ASP katika kutekeleza Mapinduzi ya Zanzibar ya mwaka 1964 yaliyomuingiza madarakani Karume.

Ni Chama hiki cha Ummah Party ndicho kilichotoa wanamapinduzi Majemedari kama Komredi Ali Sultan Issa, Kanali Ali Mahfoudh, Komredi Sharifu Ahmed Badawyi Qullatein na wengineo ambao walikuwa chachu ya Mapinduzi ya Zanzibar. Kijana mdogo Salim Ahmed Salim alishirikiana na kulelewa na wote hao, jambo lililompa uzoefu, uwezo na mafunzo.

Mpaka leo rekodi zinamuonyesha Dkt Salim A Salim aliyezaliwa Januari 23, 1942 kuwa ndiye Mtanzania mwenye umri mdogo zaidi kuteuliwa kuwa Balozi wa Tanzania nje ya Nchi.

Dr. Salim Ahmed Salim hakuishia kuwa Balozi wa Tanzania nchini Misri tu bali alihudumu katika nchi nyingine kama vile India na China.

Pia alihudumu kama Mwakilishi wa kudumu wa Tanzania katika Umoja wa Mataifa kuanzia mwaka 1970.

Mwaka 1976 alihudumu kama Rais wa Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa kwa kingereza United Nations Security Council (UNSC) na mwaka 1979 kama Rais wa Kikao cha 34 cha Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa (Thirty-Fourth Session of the United Nations General Assembly) UNGA.

Alirejea Tanzania na kuhudumu kama Waziri Mkuu na Naibu Waziri Mkuu kati ya miaka ya 1984 na 1989.

Dr. Salim Ahmed Salim pia alihudumu kama Katibu Mkuu wa iliyokuwa Jumuiya ya Muungano wa Afrika kwa kingereza Organisation of African Unity (OAU) sasa Umoja wa Afrika (AU) kutoka mwaka 1989 mpaka 2001.

Dr Salim Ahmed Salim alihusika kimamilifu katika mabadiliko ya taasisi hii muhimu kwa Afrika kutoka OAU kwenda AU.

Akiwa Mwenyekiti wa Kamati Maalumu ya Umoja wa Mataifa ya kuondoa Ukoloni yaani United Nations Special Committee on Decolonisation (UNSCD) Dr Salim Ahmed Salim alisaidia kuweka misingi mipya ya kupatikana kwa kipindi kingine cha Uhuru wa Bara zima la Afrika.

Akiwa kiongozi wa mapambano dhidi ya ubaguzi wa rangi alihudumu kama Mwenyekiti wa Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa liliweka vikwazo dhidi ya Rhodesia kwa kingereza Chairman of the United Nations Security Council Commission on Sanctions against Rhodesia (Sasa Zimbabwe).

Pia alihudumu kama Rais wa Mkutano Mkuu wa Kimataifa ulioiwekea vikwazo nchi ya Afrika ya Kusini kwa kingereza the President of the International Conference on Sanctions against South Africa na pia kama Rais wa Mkutano wa Kimataifa wa Paris uliojadili ubaguzi wa rangi yaani President of the Paris International Conference on Apartheid.

Kwa kutambua mchango wake katika bara la Afrika, Dr. Salim Ahmed Salim alitunukiwa tuzo mbalimbali kutoka katika nchi za Togo, Rwanda na Liberia.

Kwa sasa Dr. Salim Ahmed Salim ni Mwenyekiti wa Taasisi ya Mo Ibrahim Foundation ambayo hutoa Tuzo kwa viongozi bora barani Afrika.

Uwanja wa Diplomasia.

Maelezo haya ni kwa hisani ya Mzee Mohamed Said na tovuti ya Mo Ibrahim Foundation.

Sent using Jamii Forums mobile app
Nguli wa diplomacy huyu, 1971 moto uliwaka UN kupitia hoja nzito za huyu kamanda wakina Regan walimchukia balaa kamanda Salim na 1976 moto pia ukawaka tena Tanzania kwa sasa tunakosa vichwa bora kama hivi vya kina kamanda Salim.
 
Back
Top Bottom