Pre GE2025 Dkt. Slaa: Namuunga mkono Mbowe kushiriki chaguzi zijazo hata kama Serikali haitokuwa tayari suala la Katiba Mpya

Pre GE2025 Dkt. Slaa: Namuunga mkono Mbowe kushiriki chaguzi zijazo hata kama Serikali haitokuwa tayari suala la Katiba Mpya

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)

mwanamwana

JF-Expert Member
Joined
Aug 1, 2011
Posts
1,309
Reaction score
4,798
MWANASIASA mkongwe na Katibu Mkuu wa zamani wa Chadema, Dk. Wilbroad Slaa amesema anamuunga mkono Mwenyekiti Chadema, Freeman Mbowe kuhusu uamuzi wa kutangaza kushiriki katika chaguzi zijazo hata kama Serikali haitakuwa tayari kuwapatia Watanzania Katiba mpya.

Akizungumza na MwanaHALISI Online leo Jumatatu, Dk. Slaa amesema historia inaonesha kuwa si mara ya kwanza kudai katiba mpya na kushiriki uchaguzi ambao uliwawezesha kuambulia ushindi katika maeneo machache.

“Chadema imefanya utafiti na kuona angalau hatutamuachia bucha zima fisi, maana yake kama ukimuachia nyama yako italiwa hadi mifupa ila ukishiriki angalau mifupa yako utailinda kuna kitu utaambulia. Tumeona mwaka 2019 CCM ilichukua yote, leo Tanzania nzima inapata hasara, 2020 tumejitoa dakika za mwisho sasa tunaona hela zetu bado watazipiga na wataendelea kwa sababu hatuna wawakilishi. Hivyo lazima tufanye utafiti badala ya maneno ya kisiasa.

“Ukiuliza watu wa mitaani watakuambia tunataka katiba kwanza lakini katiba yenyewe hawaijui, watu hao hao ukiwaita kwenye maandamano hawatokei, sasa utafanya nini? Ushauri wangu wakati tunapoendelea kudai katiba, tuendelee na uchaguzi, kwa sababu kuna vyama vingi vya siasa ambavyo havina ajenda ya Katiba mpya kwenye uchaguzi jambo ambalo vinatufanya tuone vipo kumuunga mkono Rais Samia,” amesema.

Chanzo: Mwanahalisi
 
SAHIHI KABISA...KIBARAKA ZITO NA CHAMA CHAKE WAPO WANADAI KATIBA CYO LAZIMA KWAO
 
Kususa kote kule haha

Susaa wengine wanakula

Mbowe ana bahati sana kuongoza watu wenye upungufu wa fikra

Atatawala mpaka siku anaingia kaburini japo ni jiooni🎯🥤🥤
 
MWANASIASA mkongwe na Katibu Mkuu wa zamani wa Chadema, Dk. Wilbroad Slaa amesema anamuunga mkono Mwenyekiti Chadema, Freeman Mbowe kuhusu uamuzi wa kutangaza kushiriki katika chaguzi zijazo hata kama Serikali haitakuwa tayari kuwapatia Watanzania Katiba mpya.

Akizungumza na MwanaHALISI Online leo Jumatatu, Dk. Slaa amesema historia inaonesha kuwa si mara ya kwanza kudai katiba mpya na kushiriki uchaguzi ambao uliwawezesha kuambulia ushindi katika maeneo machache.

“Chadema imefanya utafiti na kuona angalau hatutamuachia bucha zima fisi, maana yake kama ukimuachia nyama yako italiwa hadi mifupa ila ukishiriki angalau mifupa yako utailinda kuna kitu utaambulia. Tumeona mwaka 2019 CCM ilichukua yote, leo Tanzania nzima inapata hasara, 2020 tumejitoa dakika za mwisho sasa tunaona hela zetu bado watazipiga na wataendelea kwa sababu hatuna wawakilishi. Hivyo lazima tufanye utafiti badala ya maneno ya kisiasa.

“Ukiuliza watu wa mitaani watakuambia tunataka katiba kwanza lakini katiba yenyewe hawaijui, watu hao hao ukiwaita kwenye maandamano hawatokei, sasa utafanya nini? Ushauri wangu wakati tunapoendelea kudai katiba, tuendelee na uchaguzi, kwa sababu kuna vyama vingi vya siasa ambavyo havina ajenda ya Katiba mpya kwenye uchaguzi jambo ambalo vinatufanya tuone vipo kumuunga mkono Rais Samia,” amesema.

Chanzo: Mwanahalisi
Hapa ndo mbowe na lissu wanatofautiana

Habari hizi zitampa homa ndugu zitto kabwe ambaye anadhani cdm ikisusasa ndo fursa pekee yeye kwa act kupata majimbo machache bara
 
Dr Slaa uko sahihi.Natamani urudi Chadema uwe hata Mshauri Mkuu yaliyopita si ndwele tugange yajayo
 
Tatizo ni watanganyika asilimia kubwa bado ni wajinga na wanafiki
Kuwatetea ili kuwakomboa ni risk kubwa kwa wanasiasa wa upinzani
 
Back
Top Bottom