Pre GE2025 Dkt. Slaa: Wananchi watazuia Uchaguzi, CHADEMA ni mhamasishaji tu!

Pre GE2025 Dkt. Slaa: Wananchi watazuia Uchaguzi, CHADEMA ni mhamasishaji tu!

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)

Waufukweni

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2024
Posts
2,060
Reaction score
5,648
Mwanasiasa mkongwe na aliyewahi kuwa Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Dkt. Wilbrod Slaa, ametoa ufafanuzi kuhusu kauli ya No Reform, No Election, akisema kuwa si msimamo wa CHADEMA kususia uchaguzi bali kuzuia uchaguzi, na ni wananchi wenyewe ndio watakaoongoza zoezi hilo iwapo hakutakuwa na mabadiliko ya msingi katika sheria za uchaguzi.

1741092570534.png
Akizungumza kupitia jukwaa la Kumekucha la mtandao wa Clubhouse, Dkt. Slaa amesema kuwa tafsiri ya mwandishi wa habari mwandamizi, Ansbert Ngurumo kuhusu msimamo wa CHADEMA inaweza kuwa na upotoshaji kwa sababu ya ukosefu wa uelewa wa kina juu ya hoja hiyo.

"Taarifa ya Ansbert ikiachiwa ilivyo inapeleka ujumbe wenye shida. Huenda hajaelewa vizuri maana ya No Reform, No Election, na ikiachwa hivyo itakuwa ni upotoshaji. Kuna watu ambao hawana chanzo kingine cha taarifa, wanategemea mitandao, kwa hiyo ukiwapelekea hiyo worries anayoitaja Ansbert kwa sababu tu hajafanya utafiti, itakuwa siyo vizuri," amesema Dkt. Slaa.

Ameeleza kuwa msingi wa kauli ya No Reform, No Election unatokana na mazingira halisi ya uchaguzi nchini, hasa baada ya uchaguzi wa Serikali za Mitaa uliofanyika miezi michache iliyopita, ambao alidai ulikumbwa na dosari nyingi.

"Tujikumbushe kwamba ni miezi mitatu tu tumetoka kwenye uchaguzi wa Serikali za Mitaa, na kwa uchafuzi tuliouona, ni mjinga tu anaweza kukubali kushiriki uchaguzi mwingine kabla ya mabadiliko ya msingi katika sheria za uchaguzi. Wenzetu wanapotosha kwa kusema kuwa marekebisho ya sheria yalifanyika mwaka jana, lakini ni wale tu ambao hawajasoma yale marekebisho ndio wanaweza kusema sheria zetu zimeboreshwa," amesema.

Soma, Pia: Lissu: Mabadiliko yakikubaliwa, Uchaguzi utaahirishwa na Bunge litarudishwa hata kama lilivunjwa

Dkt. Slaa alisisitiza kuwa Ibara ya 8 ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inatoa mamlaka yote kwa wananchi, hivyo wao ndio wenye uamuzi wa mwisho kuhusu uchaguzi.

"Kwa mara ya kwanza katika historia ya Tanzania, kupitia sheria zilizorekebishwa, wananchi ndio watakaosema No Reform, No Election, siyo CHADEMA inasusia au haitashiriki. Wananchi wenyewe ndio watakaozuia uchaguzi. Hii ni haki yao kwa mujibu wa Ibara ya 8 ya Katiba, inayoeleza kuwa mamlaka yote yatatoka kwa wananchi," amesema.
 
Mimi ni mmojawapo, sitapoteza muda wangu kwenda kupiga kura japo nimo kwenye daftari la wapigakura."No reform no election" ni kitu real, CHADEMA watafanya kama kumsukuma mlevi tu.

Hii nimeisema hata kabla ya uchaguzi wa Serikali za mitaa. Nitakakikisha wote walioko kwenye kaya yangu hawarubuniwi hata kwa pesa. Lengo sio Lissu ashinde lengo ni sheria zisipindishwe na wezi wa kura ili aliyeshinda kihalali atangazwe.
 
Mandevu karudi tena..... Hajajua kwamba yuko peke yake likimkuta LA kumkuta. Hela za Father Kitima zitamtoa roho. Father Kitima anatumia mwanya wanna "TONE TONE" Kuingiza hela za kanisa kwa mtu wao
 
Mandevu karudi tena..... Hajajua kwamba yuko peke yake likimkuta LA kumkuta. Hela za Father Kitima zitamtoa roho. Father Kitima anatumia mwanya wanna "TONE TONE" Kuingiza hela za kanisa kwa mtu wao
Anaunguruma CH kama kawa huku Chawa mkiendelea kumtisha ili mikono yenu iende kinywani.
 
Mandevu karudi tena..... Hajajua kwamba yuko peke yake likimkuta LA kumkuta. Hela za Father Kitima zitamtoa roho. Father Kitima anatumia mwanya wanna "TONE TONE" Kuingiza hela za kanisa kwa mtu wao
Tunaomba mwaka huu mjiandae kisakolojia!!Mkilazimisha uchaguzi ufanyike wale wote watakao panga mstari pamoja na wasimamizi wao tuna mpango wa kuwafurasha Kila kituo mawe ndiyo siraha yetu
 
Tunaomba mwaka huu mjiandae kisakolojia!!Mkilazimisha uchaguzi ufanyike wale wote watakao panga mstari pamoja na wasimamizi wao tuna mpango wa kuwafurasha Kila kituo mawe ndiyo siraha yetu
Siraha ndio nn wewe boya
 
Mandevu karudi tena..... Hajajua kwamba yuko peke yake likimkuta LA kumkuta. Hela za Father Kitima zitamtoa roho. Father Kitima anatumia mwanya wanna "TONE TONE" Kuingiza hela za kanisa kwa mtu wao
Punguza utoto dogo, mabadiliko hayakwepeki.
 
Back
Top Bottom