Dkt. Sulle: Mwinyi kuitwa "Mzee Ruksa" ilitokana na vurugu bucha la nguruwe Tandale 1993

Dkt. Sulle: Mwinyi kuitwa "Mzee Ruksa" ilitokana na vurugu bucha la nguruwe Tandale 1993

Yoda

JF-Expert Member
Joined
Jul 22, 2018
Posts
48,475
Reaction score
70,102
Nimeona clip moja ya Sheikh mwanaharakati, Dr Sulle akisema watu wengi hawajui au wanapotosha hayati Rais Mwinyi kuitwa Mzee Ruksa.

Akitoa historia fupi Dr Sulle anasema mwaka 1993 kulitokea vurugu kubwa Dar es Salaam baada ya msichana mmoja wa Kiislamu aliyetumwa kununua nyama kukosea na kwenda kununua kitimoto katika bucha mojawapo la Nguruwe lilikuwepo Tandale.

Baada ya habari hiyo kusambaa anasema walifanya vurugu kubwa iliyosababisha uharibifu mkubwa wa mali pamoja na kutishia amani. Ndipo hayati Rais Mwinyi alipohutubia taifa katika kutuliza hali kwa hekima na katika kuwafanya Wakristo na Waislamu waishi kwa pamoja kwa upendo baada ya kutoa nasaha nyingi akatamka katika hotuba yake nchi hii haina dini, kila mtu mwenye kutaka chake na ale, mwenye kutaka jongoo ale ruksa, mwenye kutaka panya ale ruksa, na hapo ndipo neno ruksa lilianzia.

Pamoja na hilo, Dr Sulle anasema pia Mwinyi ndiye baba wa mageuzi wa uchumi na siasa wa taifa hili na hakuna Rais aliyelitendea haki taifa hili kumzidi Mwinyi.

Mwanahistoria Mohamed Said ni kweli hayati Rais mwenye kuitwa Mzee Ruksa sio kutokana na yeye kuleta uhuru wa biashara na siasa nchini bali hilo neno liliibuka kutokana na vurugu zilizohusisha nguruwe Tandale?
 
Huyu sheikh huwa simuungi mkono abrakadabra zake za kidini lakini kwa hili la mwinyi kuitwa ruksa ni kweli lilianzia pale alipotuliza mambo kwenye vurugu za bucha za nguruwe akisema ni ruksa kula chochote mwananchi akitaka bila kubughudhiwa
 
Sule kwanza sio dokta. Then pia ana udhaifu flani hivi wa kuamini Kila alisemalo ndilo sahihi wakati Kwa namna flani huongea mitizamo tu.
Sule huigiza kwamba ni msomi mbobevu katika sayansi nk but si kweli.
Sule katika nasaha zake flani anasema huwezi kwenda peponi Kwa kutoka sadaka ya Tsh 3000 akimaanisha fedha hiyo n ndogo sana kumrudhisha mola mlezi. Wala huingii peponi Kwa kusalisali.
Wakati kiukweli uislam hausemi hivyo,
Swala la Ruksa na shekhe Mwinyi nisidanganye .
Sikuwepo
 
Nimeona clip moja ya Sheikh mwanaharakati, Dr Sulle akisema watu wengi hawajui au wanapotosha hayati Rais Mwinyi kuitwa Mzee Ruksa.

Akitoa historia fupi Dr Sulle anasema mwaka 1993 kulitokea vurugu kubwa Dar es Salaam baada ya msichana mmoja wa Kiislamu aliyetumwa kununua nyama kukosea na kwenda kununua kitimoto katika bucha mojawapo la Nguruwe lilikuwepo Tandale.

Baada ya habari hiyo kusambaa anasema walifanya vurugu kubwa iliyosababisha uharibifu mkubwa wa mali pamoja na kutishia amani. Ndipo hayati Rais Mwinyi alipohutubia taifa katika kutuliza hali kwa hekima na katika kuwafanya Wakristo na Waislamu waishi kwa pamoja kwa upendo baada ya kutoa nasaha nyingi akatamka katika hotuba yake nchi hii haina dini, kila mtu mwenye kutaka chake na ale, mwenye kutaka jongoo ale ruksa, mwenye kutaka panya ale ruksa, na hapo ndipo neno ruksa lilianzia.

Pamoja na hilo, Dr Sulle anasema pia Mwinyi ndiye baba wa mageuzi wa uchumi na siasa wa taifa hili na hakuna Rais aliyelitendea haki taifa hili kumzidi Mwinyi.

Mwanahistoria Mohamed Said ni kweli hayati Rais mwenye kuitwa Mzee Ruksa sio kutokana na yeye kuleta uhuru wa biashara na siasa nchini bali hilo neno liliibuka kutokana na vurugu zilizohusisha nguruwe Tandale?
Yupo sahihi
 
Mbona leo hii kula mchana wakati wa mfungo pendwa sio rukhsa?
angekuwa ndiye yeye anatawala angetoa tamko kuwa ni ruksa kula mchana watu wasibughudhiwe. Nipo mgahawa flani naona waislam wawili mume na mke wanakula ugali mchana kweupe bila kujificha, ingekuwa zanzibar cha moto wangekiona
 
Mimi ninachojua jina hilo limeanza pale aliporuhusu biashara huria wafanyabiashara waingize bidhaa zilizokuwa adimu kutokana na ukiritimba wa serikali wa kuhodhi kila kitu hali iliyofanya maisha ya wananchi kuwa magumu.
neno ruksa lilitamalaki baada ya kutuliza hali ya mambo kutokana na vurugu za waislam kuharibu bucha za nguruwe japo aliruhusu soko huria lakini neno ruksa hakulitaja huko nyuma. Ukijumlisha soko huria na kuwepo na uhuru wa kula unachotaka alioutoa ndi neno ruksa likashadidika na kuitwa mzee ruksa
 
neno ruksa lilitamalaki baada ya kutuliza hali ya mambo kutokana na vurugu za waislam kuharibu bucha za nguruwe japo aliruhusu soko huria lakini neno ruksa hakulitaja huko nyuma. Ukijumlisha soko huria na kuwepo na uhuru wa kula unachotaka alioutoa ndi neno ruksa likashadidika na kuitwa mzee ruksa
Siwezi kukubishia ndiyo maana nimesema ninavyojua mimi na hayo unayoyajua wewe ni yako.
 
Huwa mnapata wap muda wa kuwasikiliza watu kama hawa?...wanapatikana channel gan
 
Nimeona clip moja ya Sheikh mwanaharakati, Dr Sulle akisema watu wengi hawajui au wanapotosha hayati Rais Mwinyi kuitwa Mzee Ruksa.

Akitoa historia fupi Dr Sulle anasema mwaka 1993 kulitokea vurugu kubwa Dar es Salaam baada ya msichana mmoja wa Kiislamu aliyetumwa kununua nyama kukosea na kwenda kununua kitimoto katika bucha mojawapo la Nguruwe lilikuwepo Tandale.

Baada ya habari hiyo kusambaa anasema walifanya vurugu kubwa iliyosababisha uharibifu mkubwa wa mali pamoja na kutishia amani. Ndipo hayati Rais Mwinyi alipohutubia taifa katika kutuliza hali kwa hekima na katika kuwafanya Wakristo na Waislamu waishi kwa pamoja kwa upendo baada ya kutoa nasaha nyingi akatamka katika hotuba yake nchi hii haina dini, kila mtu mwenye kutaka chake na ale, mwenye kutaka jongoo ale ruksa, mwenye kutaka panya ale ruksa, na hapo ndipo neno ruksa lilianzia.

Pamoja na hilo, Dr Sulle anasema pia Mwinyi ndiye baba wa mageuzi wa uchumi na siasa wa taifa hili na hakuna Rais aliyelitendea haki taifa hili kumzidi Mwinyi.

Mwanahistoria Mohamed Said ni kweli hayati Rais mwenye kuitwa Mzee Ruksa sio kutokana na yeye kuleta uhuru wa biashara na siasa nchini bali hilo neno liliibuka kutokana na vurugu zilizohusisha nguruwe Tandale?
Mzee Pascal Mayalla wa kitimoto thibitisha hili....ikiwezekana tuelezee unayoyakumbuka.

Karibu..

JokaKuu
 
Back
Top Bottom