Dkt. Tax ashiriki Hafla ya Kufunga Mafunzo ya Utayari Dhidi ya Dharura za Kemikali na Mionzi

Ojuolegbha

JF-Expert Member
Joined
Sep 6, 2020
Posts
1,278
Reaction score
797

Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa Dkt. Stergomena Tax, Machi 14, 2024 ameshiriki katika hafla ya kufunga mafunzo ya utayari dhidi ya dharura za kemikali na mionzi, ambapo Mgeni rasmi alikuwa Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Kassim Majaliwa. Sambamba na Ufungaji wa Mafunzo hayo Waziri Mkuu alizindua miongozo ya Kitaifa ya namna ya kukabiliana na majanga yatokanayo na kemikali na mionzi nchini.


Mafunzo hayo yaliyofungwa na Mheshimiwa Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, yameshirikisha washiriki toka wizara mbalimbali za serikali ikiwa ni pamoja na Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa na Taasisi zake.

 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…