Doctor nisaidie

SIS DREAD

Member
Joined
Jan 3, 2013
Posts
33
Reaction score
2
Nimekuwa nikipata tatizo la kutopata choo kwa muda mrefu sana naweza kukaa hata wiki nzima bila kupata choo bt nakula vizuri kawaida milo 3 sijui hata hicho chakula kinaenda wapi nimeonana na madaktari wengi kila mmoja akinipa ushauri wake mara kunywa maji mengi nakunywa wapi, mara kula sana matunda nakula matunda katika kila mlo lakini hakuna kitu mara ushibi vizuri bt me kwa kiasi changu nakuwa nimeshiba kabisa pamoja na hayo yote nimetokewa na kitu cha ajabu safari hii nimekaa bila kupata choo hadi jana ilikuwa siku ya nane usiku nikanywa glass ya maziwa baridi sana asubuhi nimepata choo hadi nimeogopa je Doctor inamaana hayo maziwa ndo tiba yangu????
 
tafuta unga wa ubuyu..unauzwa 5000 tu..ni noma!utak*nya daily,..weka vijiko viwili vikubwa vya chakula vilivyojaa,changanya kwenye glasi ya maji ya kawaida ya kunywa..kunywa mara mbili kwa siku mpaka utakapoona unapata choo fresh,..unaweza kuumaliza wote
 
MARADHI YA KUTOPATA CHOO (CONSTIPATION): Haya ni maradhi ambayo mgonjwa huwa hapati choo kwa wepesi. Haja kubwa inaweza kutoka baada ya siku moja au mbili au zaidi na ikitoka huwa ni kigumu na hutoka kwa shida na wakati mwingine huwa kama

cha mbuzi. Wagonjwa wengine hupata maumivu wakati wa kwenda haja kubwa.
Mtu mwenye afya nzuri hupata haja kubwa kwa kiwango cha chini mara moja kwa siku. Na choo huwa laini na hutoka bila matatizo.

SABABU ZA MARADHI HUSIKA:
(1) Upungufu wa vitamini mwilini hasa vitamin B. (2) Maradhi ndani ya utumbo mpana. (3) Kula vitu vigumu na vikavu kama vile vyakula vya ngano. (4) Upungufu wa ulaji matunda na mboga. (5) Kutokunywa maji ya kutosha. (6) Upungufu wa fibre kwenye chakula zinazopatikana kwenye maganda ya mahindi. (7) Ukosefu wa kufanya mazoezi ya viungo.

TIBA: Kanuni ya kwanza:

Chukua glasi moja ya maziwa freshi baridi uchanganye na vijiko viwili vikubwa vya asali na kijiko kimoja kidogo cha mafuta ya habitsoda. Kunywa glasi moja kutwa mara mbili asubuhi na jioni. Dawa hii hufanya choo kuwa laini na kupata haja kubwa kwa wepesi.

Kanuni ya pili: Unga wa sanamaki kijiko kimoja kikubwa, Unga wa tangawizi kijiko kimoja kikubwa, Unga wa habasoda kijiko kimoja kikubwa, na Asali robo lita. Dawa hizi zote zichanganye pamoja kwa kukoroga kwa kijiko. Kula kijiko kimoja kutwa mara tatu.

Kanuni ya tatu: Asali robo lita, na Unga wa Arki susi vijiko vinne vikubwa. Kula vijiko viwili vikubwa kutwa mara mbili.

Kanuni ya nne: Kunywa kwa wingi maji ya Uvuguvugu ya kunywa ya kutosha na pia ule kwa wingi matunda na mboga.


Kanuni ya tano: Kula kila siku asubuhi tende saba kabla ya chakula cha asubuhi. Tende hufanya choo kuwa laini. Mkuu.@SIS DREAD Dawa zangu kisha unipe feedback.
 
pia ukwaju (tamarindus indica) ni dawa nzuri ya constipation/kukosa choo na imethibitishwa na tafiti mbalimbali. jitahidi uwe unatumia juisi ya ukwaju mara kwa mara.
 
Hukusema glass ya maziwa ina ujazo gani, kwa kifupi maziwa yana sukari iitwayo galactose ambayo watu wazima hawana vichocheo (enzymes) kuweza kuigeuza iwe glucose. Hivyo kusababisha upate choo laini kutokana na maji kunyonywa katika kuta za utumbo kwa sababu ya osmolarity (sijui kwa kiswahili) imekuwa kubwa kwenye utumbo kutokana na maziwa ambayo ni undigested.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…