Doctors msaada tafadhali

Doctors msaada tafadhali

Nambukwa

JF-Expert Member
Joined
Aug 5, 2009
Posts
243
Reaction score
146
Nina kauvimbe kwenye jicho, sio jipu , hauwashi wala haumi, ila unanikera sana kuungalia.
Uvimbe huu huwa unajitokeza na kupotea mara nyingi ila kwa sasa uko kwa muda mrefu. Ni zaidi ya wiki tatu na umeongezeka ukubwa.
Je uvimbe huu unasababishwa na nini??
Nilikuwa na macho masafi, meupe lakinin kwasasa yanakuwa mekundu . Nifanyaje kusafisha macho?
 

Attachments

  • photo0245_001.jpg
    photo0245_001.jpg
    75.1 KB · Views: 179
Pole bibie.@nambukwa Ningelikushauri uende Hospitali iliyo karibu na wewe ukaonana na Daktari wa macho akupe dawa ujipake ili hicho kipele kiondoke hapo kilipo. Kwani hapo kilipo ni sehemu ya hatari ya jicho usije poteza jicho fanya haraka kabla hayajakuwa matatizo makubwa.
 
Aisee! Pole sana, yaani kama askari aliyevuta bangi, no offence!
Usijali bibie, utapona. Fanya kama alivyo kuambia MziziMkavu!
 
kama sijakosea hiyo condition inaitwa eye lid scoliosis ,hako kauvimbe kwa ndani ni kagumu.Nilishawahi kupata similar condition nilipokuwa Russia na nikafanyiwa surgery haijajirudia tena.Kamuone Daktari wa macho,mara nyingi ni benign tumour na inatibika
 
Pole bibie.@nambukwa Ningelikushauri uende Hospitali iliyo karibu na wewe ukaonana na Daktari wa macho akupe dawa ujipake ili hicho kipele kiondoke hapo kilipo. Kwani hapo kilipo ni sehemu ya hatari ya jicho usije poteza jicho fanya haraka kabla hayajakuwa matatizo makubwa.

asante kwa ushauri, kwa sasa niko nchi ya Afrika ambayo iko nyuma kimaendeleo kuliko Tanzania, nitarudi nyumbani mwezi wa tatu, natamani kumuona daktari wakati niko nyumbani. ushauri kuhusu hilo tafadhali.
 
kama sijakosea hiyo condition inaitwa eye lid scoliosis ,hako kauvimbe kwa ndani ni kagumu.Nilishawahi kupata similar condition nilipokuwa Russia na nikafanyiwa surgery haijajirudia tena.Kamuone Daktari wa macho,mara nyingi ni benign tumour na inatibika

asante nacheck hiyo kitu kama inafanana na tatizo langu.
 
Agha khan kuna dr mzuri wa macho, utapata huduma ya haraka na hakuna foleni. Pole sana, kila la kheri.
 
Back
Top Bottom