#COVID19 Dodoma: Daladala zapigwa marufuku kusimamisha abiria ili kudhibiti Coronavirus

#COVID19 Dodoma: Daladala zapigwa marufuku kusimamisha abiria ili kudhibiti Coronavirus

Miss Zomboko

JF-Expert Member
Joined
May 18, 2014
Posts
4,599
Reaction score
9,532
Mkuu wa Mkoa wa Dodoma nchini Tanzania Anthony Mtaka ameagiza magari ya abiria yanayofanya na kuanzia safari zake mkoani hapo kutosimamisha abiria ikiwa ni hatua ya kupambana na corona.

Mtaka ametoa agizo hilo leo Jumamosi Julai 10, 2021 wakati Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dk Dorothy Gwajima alipofanya ziara yake katika Hospitali ya Rufaa ya Dodoma kuangalia utayari wa kupambana na ugonjwa huo.

Pia amewaagiza viongozi wa masoko kuhakikisha kuna maji tiririka katika milango ya kuingia masokoni, huku akiwataka wafanyabiashara kuvaa barakoa.

Mtaka ametoa maagizo kwa wote wanaofanya mikutano katika mkoa huo wa Dodoma kuhakikisha wanafuata taratibu za kujilinga ikiwemo kuvaa barakoa, kunawa mikono.

“Maelekezo ya waziri kila mmoja ameyasikia mwisho wa siku anayekukufa, kuugua sio serikali wala hospitali ni wewe chukua tahadhari,” amesema Mtaka.

Akizungumza Dk Gwajima amewataka watanzania kuepuka mikusanyiko isiyolazima ili kuepuka maambukizi ya ugonjwa wa corona.

“ Tuepuke misongamano isiyo ya lazima na kama ni lazima chukua tahadhari vaa barakoa nawa mikono kwa kutumia maji tiririka tumia vitakasa mikono,”amesema.

Gwajima amewataka kufanya mazoezi pamoja na kuzingatia lishe bora ili kuongeza kinga ya mwili.

Mwananchi
 
Kwendeni zenu huko na makorona yenu ya kuigiza.

Huku mtaani hakuna corona wala nini. Tuko fiti mno.

Kwanza tushasahau hizo habari potofu za corona. Tulizipuuza kama upuuzi mwingine wowote.

Kwahiyo msitake kutulazimishia magonjwa ambayo hatuna.

Kama mmekula pesa za wazungu na baba zenu ni heri mzitapike.

Tuko bize na kazi msipotezee muda!
 
Waweke lockdaown kabisa!

Si wanataka waonekane ili wapate yale mabilioni!
 
“Maelekezo ya waziri kila mmoja ameyasikia mwisho wa siku anayekukufa, kuugua sio serikali wala hospitali ni wewe chukua tahadhari,” amesema Mtaka.
Pamoja na yeye mwenyewe, mbona yeye anajtoa
 
Hii ni hatua njema. Mikusanyiko isiyokuwa na umuhimu isitishwe. Kwingine social distancing, barakoa, sabuni na maji tiririka zi zingatiwe.

Haya mkiopo na misaada piga chini kuwakata vilimilimi wenye hoja nyepesi nyepesi:

IMG_20210706_203616_157.jpg


Mbio za mwenge kokote zilizo zisimame sasa.
 
Kwendeni zenu huko na makorona yenu ya kuigiza.

Huku mtaani hakuna corona wala nini. Tuko fiti mno..
Acha watufanyie maigizo tu Ili kuwafurahisha watoa pesa miaka ya usoni itatoa majibu,watajutia uamuzi huu.

Dunia nzima inajifunza kuishi na corona hata huko Ulaya, ila wale wanaotegemea misaada wanalazimishwa waiogope I'li jamaa waendelea kuuza chanjo, mask na kutia mikopo, halafu wanatafuta msamiati wimbi la 3 😁😁😁
 
Next stop Dar es Salaam, kupambana na Corona lazima mfuate hatua zote ikiwemo lockdown, sio mnaokoteza hatua mnazopenda nyie nyingine mnaziacha, hapo inakuwa sio kupambana na Corona bali ni kucheza na Corona.
 
Pole yao sana... Mafuta juu, hesabu juu, alafu level seat...
 
Kwendeni zenu huko na makorona yenu ya kuigiza.

Huku mtaani hakuna corona wala nini. Tuko fiti mno.

Kwanza tushasahau hizo habari potofu za corona. Tulizipuuza kama upuuzi mwingine wowote.

Kwahiyo msitake kutulazimishia magonjwa ambayo hatuna.

Kama mmekula pesa za wazungu na baba zenu ni heri mzitapike.

Tuko bize na kazi msipotezee muda!
We mpuuzi sana

Sent from my SM-N960F using JamiiForums mobile app
 
Chadema wanataka Nchi iingie kwenye lockdown.
 
Kwendeni zenu huko na makorona yenu ya kuigiza.

Huku mtaani hakuna corona wala nini. Tuko fiti mno.

Kwanza tushasahau hizo habari potofu za corona. Tulizipuuza kama upuuzi mwingine wowote.

Kwahiyo msitake kutulazimishia magonjwa ambayo hatuna.

Kama mmekula pesa za wazungu na baba zenu ni heri mzitapike.

Tuko bize na kazi msipotezee muda!
Samahi comrade ni wewe na nani mnajizungumzia hapa?
 
Kusimamisha abiria ni utaratibu ambao sio rasmi... Daladala Au Basi linapewa leseni kwa idadi maalum ya siti za abiria...
Kwa usafiri wa mkoani nakubali ila kwa usafiri wa mjini naomba tutumie mazingira yetu kufanya maamuzi ya busara.

Ni kwanini mwendo kasi wanasimamisha abiria na hawana level seat?

Ni kwanini hata nchi za nje, ziwe treni za mijini au mabasi wanasimamisha abiria?

Kwa sababu Nissan Civillian imeandikwa abiria 30 ndiyo na sisi wabongo tupakie abirie 30 tu?

Ikiwa tutapakia level seat, watu watafika maofisini saa ngapi? Si makonda wataanza kuchukua rushwa ili wakulindie kiti?

Na iwapo mtaweka level seat, mnadhani huyu mfanyabiashara atapata faida wapi? Au nyie mnakuja kuchukua kodi tu?

Hebu tuacheni sheria za wakoloni.
 
Acha watufanyie maigizo tu Ili kuwafurahisha watoa pesa miaka ya usoni itatoa majibu,watajutia uamuzi huu.

Dunia nzima inajifunza kuishi na corona hata huko Ulaya, ila wale wanaotegemea misaada wanalazimishwa waiogope I'li jamaa waendelea kuuza chanjo, mask na kutia mikopo, halafu wanatafuta msamiati wimbi la 3 😁😁😁
Kujifunza kuishi na corona ndiyo huku kujifunza ustaarabu wa level sit kwenye vyombo vya umma.

Kaa kijanja corona inauwezo wa kufyeka hata rais mbabe.
 
Back
Top Bottom