KERO 'Dodoma inanuka', baadhi ya maeneo yametapakaa maji taka katikati ya Mji

Hii ni kero ambayo mwananchi ameiwasilisha JF akitaka wahusika kuchukua hatua

Nyakijooga

JF-Expert Member
Joined
Dec 9, 2018
Posts
276
Reaction score
473
Your browser is not able to display this video.

Your browser is not able to display this video.


Your browser is not able to display this video.
Jiji la Dodoma linaendeshwaje katika upande wa utunzaji wa mazingira.

Hali ilivyo naona kabisa kuna uwezekano wa kuibuka kwa magonjwa ya kuambukiza ikiwemo Kipindupindu kutokana na mfumo wa maji taka kuwa wa ovyo katika baadhi ya maeneo yakiwemo ya Mjini.

Kuna chemba ipo mbele ya Ofisi za TAKUKURU na Ofisi za Chama cha Walimu (CWT) zinazotazama na Uwanja wa Jamhuri, imefumuka inamwaga kinyesi na inavyoonekana ni suala la kawaida tu.


Chemba nyingine hii naiita “Baba Lao” ipo karibu na Soko la Machinga Complex hapa ni hatari zaidi, maana mkondo wake unafika mpaka kwenye sehemu wanayouza chakula.

Kwa ufupi nikisema Dodoma inanuka na imetapaka uchafu, ninamaanisha, hivi karibuni magonjwa yanasababishwa uchafu kama kipindupindu yataibuka kwa sisi Wananchi tunakula kinyesi.

Moja ya Chemba ipo karibu na bomba na maji safi na mkondo wake pia unaenda kwenye njia za maji safi.

Pia, soma;

√ - DUWASA: Changamoto ya kusambaa kwa majitaka Dodoma, kulikosababishwa na chemba kuziba imetatuliwa
 
O

OFISI ZAO HUZIJUI ?
 
Mkuu ushawahi kupita vingunguti? Nadhani hili tatizo lipo kila mkoa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…