Dodoma: Timu ya wawezeshaji yanolewa utaratibu mpya mikopo ya asilimia 10 kwa wanawake, vijana na watu wenye ulemavu

Dodoma: Timu ya wawezeshaji yanolewa utaratibu mpya mikopo ya asilimia 10 kwa wanawake, vijana na watu wenye ulemavu

OR TAMISEMI

Ministry
Joined
Jul 3, 2024
Posts
20
Reaction score
93
605a523c-b59e-4a41-8d18-fff391ef5b53.jpeg
Katibu Mkuu Ofisi ya Rais TAMISEMI Adolf Ndunguru amefungua mafunzo ya mikopo ya asilimia 10 kwa wawezeshaji wa Kitaifa na kuwataka washiriki hao kuhakikisha wanaelewa vema ili kwenda kufundisha wengine kwa viwango vinavyokubalika.

Akifungua mafunzo hayo kuhusu utoaji na usimamizi wa mikopo ya vikundi vya wanawake, vijana na watu wenye ulemavu kwa wawezeshaji wa Kitaifa mapema leo Julai, 9, 2024 jijini Dodoma, Ndunguru amewataka wawezeshaji hao kwenda kuwezesha mafunzo watakayoyapata ili malengo yake yaweze kutimia kwani Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan ameagiza Mikopo irudishwe na isimamiwe kikamilifu.

“Ninafahamu kuwa uandaaji wa Kanuni, Mwongozo, vitini vya mafunzo pamoja na maboresho ya Mfumo wa Kielektroniki wa utoaji na usimamizi wa mikopo kwa vikundi umekamilika, niwapongeze wote mlioshiriki kukamilisha nyenzo zitakazowezesha utoaji wa mafunzo kwa wasimamizi na vikundi kabla ya kuanza kutoa mikopo kama ilivyoelekezwa na Serikali,” alisema Katibu Mkuu Ndunguru.
 
Inamaana mnakuja na mfumo mpya wa utoaji mikopo sio ule wa mwanzo? Na ni wakinani hao wanakwenda kupewa hayo mafunzo na watahusika katika utoaji wa mikopo?
 
Inamaana mnakuja na mfumo mpya wa utoaji mikopo sio ule wa mwanzo? Na ni wakinani hao wanakwenda kupewa hayo mafunzo na watahusika katika utoaji wa mikopo?
Hapana mfumo sio mpya ila umeboreshwa marekebisho ya Sheria ya Fedha sura 29 yamefanyika pamoja na mapitio ya Kanuni za Mikopo ya asilimia 10, uandaaji wa Miongozo na Vitini vya mafunzo!
 
Back
Top Bottom