Dodoma Traffic Police na Mbinu chafu za Rushwa Barabarani

Joined
Feb 9, 2012
Posts
65
Reaction score
15
Katika Hali inayoonyesha kuzidi kukomaa kwa rushwa Tanzania na hasa ndani ya jeshi la polisi askari wa usalama Barabarani Mkoa wa Dodoma wanaonyesha waziwazi kusuka mipango ya kula hela za madereva wanapowakamata na makosa babarani bila kuwafikisha vituoni.
Tabia hii inaonekana zaidi kwa Polisi wanaosimama barabara ya Dodoma-Singida ambako rushwa imekuwa ikiombwa waziwazi kuanzia Tsh 5000 mpaka Tsh 20000 kwa makosa anayokutwa nayo dereva bila kujali idadi yake.Nasema wanasuka mipango kwa sababu mara nyingi wanajificha na tochi kwenye miti mirefu na penye msongamano wa watu au magari mabovu na wanachagua magari ya kumulika wakijua lazima wahusika watakuwa na cha kuwapa bila kufika kituoni.Sikatai kwamba wanatimiza majukumu yao ila kuna mambo yanatia shaka katika utekelezaji wa majukumu haya
  • Kwanza ni utaratibu wa kuangalia speed za magari ambapo ikizidi 50km/h unatakiwa kulipa faini ya elfu 30,tatizo hapa ni kwamba barabara husika haina kibao hata kimoja kuanzia Round about mpaka $ 4 Ways kinachoelekeza mwendo na hii ni ngumu sana kwa watu wanaotoka maeneo tofauti kujua kikomo cha mwendo barabara husika
  • Pili.Utaratibu wa askari kusimama unafanyika mara nyingi mwisho wa mwezi,siku za sikukuu na mwezi kama huu ambao watu wengi wanapeleka watoto mashuleni ikimaanisha ni wakati wanapohitaji pesa zaidi
  • Tatu.Hawatembei na dicuments zozote za sheria barabarani zinazoelezea haki na wajibu wa dereva kwani sheria za barabarani zainabadilika mara kwa mara zaidi madereva wanaadhibiwa kwa sheria wasizozijua
  • Nne.Mara nyingi wnachagua magari ya kukamata(kama nilivyosema awali),hawakamati magari ya serikali,magari yaliyochakaa na magari ya masafa marefu hata kama yako mwendo mkali sana na wakikukamata wanatoa vitisho vingi vikiwemo kukupeleka kuacha gari kituoni mpaka uligomboe,kwenda jela,kunyang'anywa gari,kulipa faini kubwa zaidi ili dereva atishike na kutoa hela anayoambiwa kiurahisi bila kubisha
Inasemekana hii ni mipango inayopangwa kuanzia kwa mabosi wao ambao nao mwisho wa siku wanapata mgao baada ya kazi na hata ukienda kushataki kuombwa rushwa ni kazi bure,kwa mfano halisi ni mimi mwenyewe niliwahi kukamatwa kwa kwenda speed ya 60Km/h na askari ambaye aliniomba tumalizane na akadai kwamba siwezi kumpa chini ya Tsh 10,000 kwa kisa eti hajakamata magari ya kutosha muda huo kutimiza hela iliyokusudiwa kwa siku hiyo.Nikajiuliza hivi kusimama barabarani siku hizi na mradi halali??
 
mkuu,kuna wala rushwa wakubwa ambao wamesababisha hata hao askari kufika hapo walipofika,mishahara ni midogo sana na pia haiji kwa wakati,cha kufanya hakikisha unatoa maoni yako kikamilifu ktk katiba ijayo kusiwe na tabaka kubwa kati ya walio nacho na wasio nacho,haya yote yatakwisha.
 
Kuna askari mmoja anaitwa Mark, anapenda rushwa na ni msumbufu balaa.Hili jeshi la police sijui lifanyweje ili wajirekebishe.Nakumbuka siku moja alinikamata nilikuwa na makosa,akataka nimpe rushwa elfu 10,nikakataa,kisha akaamua kunipeleka police,nilipofika kule nikalipa faini 20000 then nikachukua risiti yangu nikasepa.Niliona bora nilipe faini kuliko kumnufaisha mtu.Tunahitaji viongozi majasiri kulishughulikia hili,hawasikii hawa jamaa na niwaonevu kweli kweli wanajiona hii nchi kama yakwao peke yao.Wanaboa sana kwa kuendekeza umasikini.
 
hilo ndo jeshi la wanyang'anyi tz....

Hayo wanayoyafanya mbona ya kawaida sana??????

Ndo maana siku hizi wameadvance wanajihusisha na ujasiriamali wa meno ya tembo
 
Tanzania Tanzania, nakupenda kwa moyo wotee, nchi yangu Tanzania nakuependa kwa moyo wote,
Sijui nilini haki itakuwepo ikiwa mvunja haki ni mwenye kufuli la kuitunza haki hiyo? Polisi wamekuwa Tim ya mpira km chama nao wanafanya mambo kwa kushirikiana, kuanzia mkubwa hadi coplo, nchi yetu itapataje kupona?
Eee Mungu tusaidie tuweze kuiponya nchi yetu.
 
polisi, polisi wa barabarani, wana usalama, wanajeshi ahaaaaaaa .......................... malizieni mi naweza ......
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…