LGE2024 Dodoma: Wenyeviti 36 na wajumbe wa serikali za mitaa 180 waapishwa Halmashauri ya Mji Kondoa

LGE2024 Dodoma: Wenyeviti 36 na wajumbe wa serikali za mitaa 180 waapishwa Halmashauri ya Mji Kondoa

Uchaguzi wa Serikali za Mitaa 2024

Don Gorgon

Member
Joined
Nov 21, 2024
Posts
35
Reaction score
68
Wenyeviti 36 na wajumbe wa serikali ya mitaa 180 katika Halmashauri ya Mji Kondoa Mkoani Dodoma wameapishwa tayari kuanza kutekeleza majukumu yao katika serikali za mitaa.

Akizungumza baada washindi hao kula kiapo, Mkurugenzi wa Halmashauri ya Kondoa Mji, Majaliwa Said amewaasa viongozi hao kwenda kuwatumia wananchi ipasavyo bila kujali vyama vyao vya kisiasa.

Aidha, viongozi hao wapya wamepata semina maalumu iliyolenga kuelimisha kuhusu majukumu yao, ili kuwawezesha kutekeleza kazi zao kwa ufanisi na kuwa mfano bora katika utawala wa serikali za mitaa. Semina hiyo ilijumuisha masuala mbalimbali, ikiwemo sheria na taratibu za utawala, mikakati ya maendeleo, na njia bora za kushirikiana na jamii ili kufanikisha malengo ya maendeleo.
 
Wenyeviti 36 na wajumbe wa serikali ya mitaa 180 katika Halmashauri ya Mji Kondoa Mkoani Dodoma wameapishwa tayari kuanza kutekeleza majukumu yao katika serikali za mitaa.

Akizungumza baada washindi hao kula kiapo, Mkurugenzi wa Halmashauri ya Kondoa Mji, Majaliwa Said amewaasa viongozi hao kwenda kuwatumia wananchi ipasavyo bila kujali vyama vyao vya kisiasa.

Aidha, viongozi hao wapya wamepata semina maalumu iliyolenga kuelimisha kuhusu majukumu yao, ili kuwawezesha kutekeleza kazi zao kwa ufanisi na kuwa mfano bora katika utawala wa serikali za mitaa. Semina hiyo ilijumuisha masuala mbalimbali, ikiwemo sheria na taratibu za utawala, mikakati ya maendeleo, na njia bora za kushirikiana na jamii ili kufanikisha malengo ya maendeleo.
That's very great,
kazi ya kuwatumikia wanainchi ianze mara moja,

well done comrades 👍 👊
 
Back
Top Bottom