Dogo janja aacha shule,afukuzwa na Madeee na kurudishwa kwao Arusha

Dogo janja aacha shule,afukuzwa na Madeee na kurudishwa kwao Arusha

Yo Yo

JF-Expert Member
Joined
May 31, 2008
Posts
11,210
Reaction score
1,720
.
Rapper mdogo kutoka A town Dogo Janja aliekua akisoma na kuishi Dar es salaam amerudishwa kwa wazazi wake Arusha jana kutokana na kufanya mambo mbalimbali ambayo uongozi wa Tiptop Connection haujapendezwa nayo.
Tip Top ambao walikua wanasimamia kazi za muziki za Janja wamempandisha basi na kumrudisha kwao jana baada ya kuona msanii huyo hazingatii shule kama inavyotakiwa, amekua mtoro wa mara kwa mara katika shule aliyokua akisoma ya Makongo na hasikii anaporekebishwa, hiyo ndio sababu kubwa ya kumrudisha ili kukwepa lawama za baadae ambazo zingetokana na Dogo Janja kutosimamiwa vizuri kwenye swala la Elimu kwa sababu Tiptop ndio waliokabidhiwa kumsimamia.
Stori kamili ya hii ishu utaipata baadae baada ya kuzungumza na Meneja wake ambae ni Madee.

Alichokiandika Dogo Janja kwenye Facebook jana.

thanks.....http://millardayo.com/
 
Wakati mwingi Dogo Janja alikua akiongea na simu kuwaaga watu huku akiwa na furaha ya kuondoka Dar es salaam alikoishi kwa tabu, anafurahi kurudi nyumbani Arusha.

.

Dogo Janja akiagana na kaka yake mwenye T shirt ya bluu yenye mistari.

.

.

.

.

Bye bye.

.

Jana kwenye AMPLIFAYA ya CLOUDS FM Msanii Madee wa Tip Top Connection ambae ndio alikabidhiwa na wazazi kumlea na kumsimamia Dogo Janja aliamplfy kuhusu sababu za kumrudisha Dogo Janja mikononi mwa wazazi wake baada ya kudai kumshindwa.
Madee kasema "Dogo Janja aliekua form II Makongo High School kakataa kusoma kwa hiyo mimi siwezi kukaa nae wakati hataki kusoma, nilikua safarini Iringa na Mbeya ambapo baada ya kurudi mwalimu wake wa darasa alinipigia simu na kunipa pole kwa sababu Dogo Janja anaumwa, nikashtuka ikabidi nimpigie nikawa simpati kwenye simu.. nikaenda nyumbani kwa Tunda Man alipokuepo na alipojua nimekuja akajificha alikua anataka kunikimbia nikampiga sana vibao, kweli nilimpiga ambapo kesho yake baada ya kuamka nikamuuliza unataka kusoma au kuzurura mtaani? akajibu kwamba anataka kwenda kusoma Arusha ikabidi nimpigie baba yake palepale ambapo mzee wake alniomba nisimrudishe Arusha niendelee kukaa nae"
Madee ameendelea kusema kwamba "nilimwacha nyumbani baada ya kuchukua simu yake ambapo nilikuta vitu vingi sana vya kishenzi shenzi kaviandika na ninavyo mpaka leo kwa ajili ya ushahidi, vimeniumiza hasa kwa mtu kama mimi ambae najua nimemtoa wapi, kaandika kuhusu uchafu mbaya na kingine kinanihusu mimi ambacho hapaswi kusema kwa mtu kama yeye, baada ya hapo msimamo wake ulikua vilevile kwamba anataka kurudi kwenda kusoma Arusha, jioni tukakaa kikao juzi na kaka yake na watu wengine na mimi nikampa baraka zote"
Kwenye sentensi nyingine Madee amesema "kwa wiki iliyopita na wiki hii Dogo Janja alitoroka kwenda shule kwa siku tatu na hii ni mara ya pili ambapo mara ya kwanza nilimpeleka shule na kumchapa mbele ya wanafunzi wenzake, yani nilivyompeleka shule wanafunzi wenzake mpaka walikua wanamshangaa, alisingizia vitu vingi vya uongo alikua ananidanganya mimi nyumbani na siku hiyo ndio nilimkuta Ubungo Plaza alikua anaogelea na rafiki yake, walimu wake waliniambia hawajamuona shule kwa muda wa wiki moja"
 
Hapa ni conflict of interest..
Story ingenoga kama na dogo nae angefunguka.. Kifupi hawaja balance story..
 
Walugulu tunasema mlongayeka kahuma. Yaani katika kesi mtu akiongea peke yake lazima ashinde. Kwa hiyo ngoja tumsikie dogo naye
 
ndio kwanza namuona huyu mtoto, kaimba mwimbo gani kwani?
 
.
Rapper mdogo kutoka A town Dogo Janja aliekua akisoma na kuishi Dar es salaam amerudishwa kwa wazazi wake Arusha jana kutokana na kufanya mambo mbalimbali ambayo uongozi wa Tiptop Connection haujapendezwa nayo.
Tip Top ambao walikua wanasimamia kazi za muziki za Janja wamempandisha basi na kumrudisha kwao jana baada ya kuona msanii huyo hazingatii shule kama inavyotakiwa, amekua mtoro wa mara kwa mara katika shule aliyokua akisoma ya Makongo na hasikii anaporekebishwa, hiyo ndio sababu kubwa ya kumrudisha ili kukwepa lawama za baadae ambazo zingetokana na Dogo Janja kutosimamiwa vizuri kwenye swala la Elimu kwa sababu Tiptop ndio waliokabidhiwa kumsimamia.
Stori kamili ya hii ishu utaipata baadae baada ya kuzungumza na Meneja wake ambae ni Madee.

Alichokiandika Dogo Janja kwenye Facebook jana.

thanks.....Millard Ayo

Dogo Janja: Show ya
milioni, Madee alinipa laki
moja
Siku moja baada ya Dogo
Janja kudaiwa kufukuzwa
Tip Top Connection, ukweli
halisi kuhusiana na uamuzi
huo umewekwa wazi na
yeye mwenyewe.
Sababu zilizotajwa na Tip
Top Connection ni kwamba
Dogo Janja alilewa sifa na
kuwa mtoro shuleni.
Kwa mujibu wa interview
(ya pili kufanyiwa baada ya
kipindi cha Amplifaya cha
jana) tuliyofanya naye kwa
simu saa moja asubuhi leo
(June 14) akiwa stand
kurejea nyumbani, uonevu
na dhuluma ndivyo
vilivyomchosha kuishi Dar
es Salaam.
Anasema tangu aje Dar es
Salaam hajawahi
kusaidiwa chochote na
Madee zaidi ya mambo ya
muziki pekee huku kula,
malazi na ada ya shule
vikifanywa na rafiki yake
Madee aitwaye Abdallah
Doka ambaye (Dogo Janja)
alikuwa akiishi kwake.
Anasema kutokana na
ngoma zake kujipatia
umaarufu alikuwa akipata
show nyingi nchini na zote
alikuwa halipwi chini ya
milioni moja.
Kilichokuwa kinamsikitisha
anasema ni kulipwa hela
kidogo isiyozidi laki mbili
na hivyo kumfanya aishi
kwa tabu licha ya kuingiza
hela nyingi za show.
“Nilikuwa navumilia tu bro
kwasababu kila
nilipolalamika kuhusu
mambo ya hela Madee
alikuwa mkali sana,”
ameongea uchungu.
Dogo anasema ilikuwa
inafikia wakati akifanya
show za ukumbuni
hulipwa elfu hamsini au
chini ya hapo na wakati
mwingine alikuwa halipwi
kabisa.
Tamaa ilizidi kumwingia
Madee kiasi cha
kumnyang’anya kadi yake
ya benki na kuanza
kuchukua hela bila kujua
password aliipata wapi.
“Kuna wakati nilikuwa
nataka kumtumia mama
laki moja, Madee
akanikataza eti kwakuwa
watadhani nina hela sana,”
anasema.
Mpaka tunaongea naye
asubuhi hii, anasema kadi
yake imebakiwa na shilingi
25,000 tu.
Ameendelea kudai kuwa
juzi Madee alimpigia simu
na kumwambia kuwa kaka
yake wa Kibaha ameandaa
show ya CCM na atamlipa
shilingi laki moja.
“Hivi kweli bro mimi ni
mtu wa kufanya show ya
laki moja?”. Hata hivyo
aliamua kukubali ili
kuepusha lawama.
Baada ya show kumalizika
anasema yeye na back up
artist wake walirudishwa
saa saba usiku wakati
asubuhi yake alitakiwa
kwenda shuleni kuchukua
namba ya mtihani na
kuandaa dawati la kukalia.
Dogo Janja anaeleza kuwa
inamuuma sana kwakuwa
muziki haujampa chochote
licha ya Madee ambaye
huwa hapati hata show
kumtumia kimaslahi na
hadi leo hii anamalizia
kujenga nyumba yake.
“Ni kama vile Madee
alinipanda ili anivune.”
Ameendelea kusema kuwa
hiyo juzi sasa hadi kufikia
Tip Top watangaze
kumfukuza alikuwa kwa
Tundaman akipiga story na
Madee akamuita kisha
kuanza kumpiga.
Alichukua simu yake
akaondoka nayo. “Jamaa
alianza kujitumia meseji
kutoka kwenye simu
yangu kwenda kwake za
matusi ama kuwa nataka
kumroga. Jana
nimemuonesha Milard hizo
meseji na amesikitika
sana.”
Anasema simu yake
alipewa jana.
Kitendo cha kumwambia
Madee kuwa amechoka na
anataka kurudi nyumbani
ndicho kimemfanya
amfanyie yote hayo hadi
kumwambia kuwa
watahakikisha
wanambania asifanye
vizuri tena kwenye muziki.
Pia amedai kuwa Madee
aliwapigia simu wazazi
wake ili wamkataze Dogo
Janja asifanye interview na
vyombo vya habari.
“Wanajua nikiongea
wataabika sana.” http://
leotainment.blogspot.com/2012/06/
dogo-janja-show-ya-
milioni-madee.html?m=1
 
Huyu mtoto namfananisha na Justin Bieber, nadhani wanalingana kiumri, sasa hivi Bieber ni Milionea kama sio Bilionea kwa sababu ya muziki tu, hapo ndipo unapojiuliza Hivi sisi Waafrika nani katuroga??!!!... eeeeshh
 
urithi wao kutoka chama cha machangu ni ufisadi! ss hata huyo mtoto unamdhulumu ili iweje?? nways ili maandiko yatimie kuwa samaki mkubwa, humla mdogo, amen!
 
Njia ya mwongo ni fupi, km Madee alikuwa anamdhulumu dogo mambo yatakuwa hadharani, muda c mrefu. Dogo karibu nyumbani.
 
Kweli mziki bongo haulipi,dogo alivyojuu kiasi icho ana 25000 tu kwenye account yake?whats going on Tip top?kumbe huku kwenye makundi nako kuna wahindi(wanyonyaji)?kabla ya wasanii kuanza kupambana na wanyonyaji wanaowaita wahindi,wajiangalie kwanza wenyewe km wanatendeana haki?keisha alikimbia tip top,saiv dogo janja kaondoka...kuna haja ya tip top kuji-evaluate upya na kujisafisha mbele ya jamii.
 
Kuhukumu dhambi lakini kwa niwajuavyo Tip Top na hasa Madee inasikitisha hasa kwa mtoto kama huyu.Dogo Janja rudi shule focus sana na elimu lakini usikitupe kipaji chako.andika mashairi,ingia mkataba na Maproducer kutengeneza ngoma zako mkatane kwenye mapato lakini this tyme ingia mkataba rasmi na uwe mkataba wa muda mfupi mfupi ili ukishindwa huongezi mkataba.pole sana dogo kua uyaone!
 
Alijiita dongo janja, amekutana na kubwa janja. Ila, kama kweli, madee, si mpango. Dogo bado mdogo.
 
Tutadis matukio yote ya Tip Top ili kuonyesha kukataa kwetu kwa dhulma kwa wasanii watoto!!
 
dogo janja shoo zote zile anarudi na akaunti inayosoma 25000 duh.!
 
Back
Top Bottom