Mohamed Said
JF-Expert Member
- Nov 2, 2008
- 21,967
- 32,074
DOME OKOCHI BUDOHI "MAU MAU" NDANI YA TANU?
Kadi ya TANU ya Dome Budohi ni no. 6.
Dome Budohi alikuwa Mluya kutoka Kenya lakini alikuwa mwanachama na kiongozi wa TAA na hivi ndivyo alivyoweza kupata kadi hiyo no. 6.
Mimi nikimfahamu katika utoto wangu kwa jina la Dickson alipokuwa akija kwetu na kuingiliana sana na wazee wangu.
Pamoja na yeye walikuwa Wakenya wawili ambao wote niliwafahamu kwa majina yao ya kwanza tu, Maxwell na Martin.
Haukupita muda mrefu toka TANU iundwe Dome Budohi alikamatwa pamoja na Wakikuyu wengi waliokuwa Tanganyika kwa tuhuma za kuhusishwa na Mau Mau.
Wengi wa hawa Wakikuyu waliotiwa mbaroni walikuwa wafanya biashara Mwanza na sehemu nyingine ya Kanda ya Ziwa.
Martin alirudi Kenya lakini Maxwell alibaki Tanzania na mimi nilikuwa nikikutananae hadi katika miaka ya 1980.
Mara ya mwisho tulionana Mtaa wa Mafia na tulipiga picha pamoja.
Picha yangu na Mzee Maxwell hiyo hapo chini.
Ilikuwa Maxwell ndiye aliyefanya juhudi ya kunikutanisha na Dome Budohi Nairobi mwaka wa 1972 alipoona nataka sana kujua yale yaliyokuwapo Mtaa wa Kipata katika miaka ile ya kupigania uhuru.
Maxwell akiniambia kuwa Dome Budohi alikuwa mstari wa mbele katika TANU hadi mwaka wa 1955 aliposalitiwa na Martin kupitia barua iliyotoka Kenya kuja kwa Budohi barua ambayo ilimuhusisha na Mau Mau.
Budohi alikuwa akifanya kazi katika duka la muziki la Assanand lililokuwa Ring Street (sasa Mtaa wa Jamhuri) na alikuwa mmoja wa vijana wanamuziki akipiga drums katika Skylarks Band iliyokuwa ikiongozwa na Ally Sykes.
Martin alikuwa akipiga trumpet katika bendi hiyo iliyokuwa maarufu kwa vijana katika miaka ile ya 1950.
Budohi pia alikuwa muigizaji wa senema na aliigiza senema moja, "Mgeni Mwema," pamoja na Rashid Mfaume Kawawa.
Juu ya haya yote hawa vijana pamoja ya kuwa walikuwa hawapunguki katika kumbi mbili maarufu za Dar es Salaam ya wakati ule, Alexander na Arnautoglo walikuwa wapigania uhuru.
Nakumbuka kama.jana vile mazungumzo yangu na Dome Budohi nyumbani kwake Ruiru na kisha Ngei Estate alipohamia baadae.
Aliniambia kuwa alikitahidi sana kutafuta kuonana na Julius Nyerere wakumbushane enzi zao kila alipokuwa akienda Nairobi lakini hakufanikiwa.
Dome Budohi hakurudi tena Dar es Salaam hadi alipofariki.
Nimeshindwa kabisa kujua kwa uhakika kama Martin alikuwa kachero katika Special Branch au vipi.
Lakini itoshe tu kuwa katika kipindi hiki tunachokizungumza ilikuja kunidhihirikia baadae sana baada ya uhuru kuwa Ali Mwinyi Tambwe Katibu wa Al Jamiatul Islamiyya fi Tanganyika na mtu karibu sana na Abdul Sykes Secretary wa TAA alikuwa kachero wa Special Branch pamoja na Alexander Tobias.
Alexander Tobias alikuwa ameajiriwa na TAA mwaka wa 1950 kama Executive Secretary.
Picha: Kambi ya Mau Mau Kenya.
Kadi ya TANU ya Dome Budohi ni no. 6.
Dome Budohi alikuwa Mluya kutoka Kenya lakini alikuwa mwanachama na kiongozi wa TAA na hivi ndivyo alivyoweza kupata kadi hiyo no. 6.
Mimi nikimfahamu katika utoto wangu kwa jina la Dickson alipokuwa akija kwetu na kuingiliana sana na wazee wangu.
Pamoja na yeye walikuwa Wakenya wawili ambao wote niliwafahamu kwa majina yao ya kwanza tu, Maxwell na Martin.
Haukupita muda mrefu toka TANU iundwe Dome Budohi alikamatwa pamoja na Wakikuyu wengi waliokuwa Tanganyika kwa tuhuma za kuhusishwa na Mau Mau.
Wengi wa hawa Wakikuyu waliotiwa mbaroni walikuwa wafanya biashara Mwanza na sehemu nyingine ya Kanda ya Ziwa.
Martin alirudi Kenya lakini Maxwell alibaki Tanzania na mimi nilikuwa nikikutananae hadi katika miaka ya 1980.
Mara ya mwisho tulionana Mtaa wa Mafia na tulipiga picha pamoja.
Picha yangu na Mzee Maxwell hiyo hapo chini.
Ilikuwa Maxwell ndiye aliyefanya juhudi ya kunikutanisha na Dome Budohi Nairobi mwaka wa 1972 alipoona nataka sana kujua yale yaliyokuwapo Mtaa wa Kipata katika miaka ile ya kupigania uhuru.
Maxwell akiniambia kuwa Dome Budohi alikuwa mstari wa mbele katika TANU hadi mwaka wa 1955 aliposalitiwa na Martin kupitia barua iliyotoka Kenya kuja kwa Budohi barua ambayo ilimuhusisha na Mau Mau.
Budohi alikuwa akifanya kazi katika duka la muziki la Assanand lililokuwa Ring Street (sasa Mtaa wa Jamhuri) na alikuwa mmoja wa vijana wanamuziki akipiga drums katika Skylarks Band iliyokuwa ikiongozwa na Ally Sykes.
Martin alikuwa akipiga trumpet katika bendi hiyo iliyokuwa maarufu kwa vijana katika miaka ile ya 1950.
Budohi pia alikuwa muigizaji wa senema na aliigiza senema moja, "Mgeni Mwema," pamoja na Rashid Mfaume Kawawa.
Juu ya haya yote hawa vijana pamoja ya kuwa walikuwa hawapunguki katika kumbi mbili maarufu za Dar es Salaam ya wakati ule, Alexander na Arnautoglo walikuwa wapigania uhuru.
Nakumbuka kama.jana vile mazungumzo yangu na Dome Budohi nyumbani kwake Ruiru na kisha Ngei Estate alipohamia baadae.
Aliniambia kuwa alikitahidi sana kutafuta kuonana na Julius Nyerere wakumbushane enzi zao kila alipokuwa akienda Nairobi lakini hakufanikiwa.
Dome Budohi hakurudi tena Dar es Salaam hadi alipofariki.
Nimeshindwa kabisa kujua kwa uhakika kama Martin alikuwa kachero katika Special Branch au vipi.
Lakini itoshe tu kuwa katika kipindi hiki tunachokizungumza ilikuja kunidhihirikia baadae sana baada ya uhuru kuwa Ali Mwinyi Tambwe Katibu wa Al Jamiatul Islamiyya fi Tanganyika na mtu karibu sana na Abdul Sykes Secretary wa TAA alikuwa kachero wa Special Branch pamoja na Alexander Tobias.
Alexander Tobias alikuwa ameajiriwa na TAA mwaka wa 1950 kama Executive Secretary.
Picha: Kambi ya Mau Mau Kenya.